Hismastersvoice
JF-Expert Member
- Jan 26, 2013
- 23,255
- 28,414
Ninawakati mgumu ninapohitaji kununua LUKU, nilizoea kwenda kwa wakala natoa hela napata units zangu bila shida, Jumanne nilienda kwa wakala na pesa kama kawaida yangu cha ajabu nilitakiwa nimpe mshiko muuzaji ili aniuzie LUKU ikabidi nimpe sh.1,500/= ambayo haina risiti! Nikauziwa units kama mahitaji yangu yalivyokuwa. Najiuliza serikali inapata faida gani kwenye utaratibu huu wakati inasema uza toa risiti!
