GE2025 Lucy Mayenga aaminiwa na wajumbe kwa kura 7,814 jimbo la Kishapu

GE2025 Lucy Mayenga aaminiwa na wajumbe kwa kura 7,814 jimbo la Kishapu

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
3,119
Reaction score
1,428

LUCY MAYENGA AAMINIWA NA WAJUMBE KWA KURA 7,814 JIMBO LA KISHAPU

Ndugu Lucy Mayenga ameibuka kinara katika kura za maoni za Chama cha Mapinduzi (CCM) kuwania ubunge wa Jimbo la Kishapu baada ya kushinda kwa kupata kura 7,814.

Matokeo hayo yaliyotangazwa na CCM Wilaya ya Kishapu yanaonesha Mayenga akiwapiku kwa mbali wagombea wengine sita waliokuwa wakichuana naye kwenye mchakato huo.

Aliyemfuata kwa kura ni Bonda Nkinga aliyepata kura 1,730, akifuatiwa na Boniphace Butondo mwenye kura 1,290. Wengine ni Dotto Kwigema (597), George Jimisha (590), Madaha Chabba (503) na John Nhyamah (432).

Ushindi huo unampa Mayenga nafasi ya kupeperusha bendera ya CCM katika uchaguzi mkuu wa Oktoba endapo atapitishwa na vikao vya juu vya chama hicho.
 

Attachments

  • Screenshot 2025-08-06 at 15-40-03 Instagram.png
    Screenshot 2025-08-06 at 15-40-03 Instagram.png
    659.1 KB · Views: 16
Back
Top Bottom