Lowassa : Tutashinda uchaguzi 2020

Lowassa : Tutashinda uchaguzi 2020



MJUMBE wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Edward Lowassa, amesema kwa hali ilivyo na inavyoendelea nchini kuna kila dalili za chama hicho kushinda uchaguzi mkuu mwaka 2020.

Lowassa alisema hayo Dar es Salaam, wakati kuna kilio kikubwa cha wananchi wanaolia kukabiliwa na hali ngumu ya kiuchumi, huku wengi wakidhani imesababishwa na kubana matumizi kunakofanywa na Serikali.
Alisema hayo wakati akifungua semina kwa wabunge, Mameya na Madiwani wa chama hicho wa Jiji la Dar es Salaam ikilenga kujadili kazi waliyofanya ya kutumikia wananchi kwa mwaka mmoja na namna ya kupiga hatua miaka minne ijayo.

Alifafanua: ”Nimepita maeneo mengi kufanya mikutano ya ndani, kwa hali ilivyo tunakubalika mno, tuna dalili zote za kushinda uchaguzi mkuu wa 2020, tujitahidi kuwa na umoja, bila umoja hatuwezi kushinda ni muhimu sana, CCM wanajua maana ya umoja na wanaung’ang’ania, tuangalie sana maneno ya kutugawa tusiyakubali.’’

Alisema CHADEMA itapita maeneo ambayo watu wako nyuma kielimu ambayo kwa kiasi kikubwa wameipigia kura CCM, ili kuwaelewesha nia njema ya kuwaletea maendeleo na kuwapa elimu.

‘’Muda uliobaki ni mchache, tunatakiwa kuamka ili chama chetu kishinde kwa kuwa tumeshakifikisha sehemu nzuri, hatuna muda tuchangamke kila mmoja aone kwamba anapaswa kueleza namna ya kukisaidia chama kivuke,’’ alisema Lowassa.

Kuhusu mikutano ya ndani ambayo aliita ‘mitamu’ zaidi, alisema vimefanya wamekuwa imara zaidi, kwani wamezungumza na wanachama wao maeneo mengi wakiwa wanaonana kwa karibu.

‘’Tumekuwa mikoani na viongozi wenzangu, tumezunguka mikoani hali ni nzuri kwa mazungumzo tuliyofanya na wanachama wetu, vikao ni vitamu zaidi kuliko vya nje, unapata nafasi ya kuongea na wananchi ana kwa ana kwa muda mrefu, kwa mapenzi na mahaba yote,’’ alisema Lowassa.

Lowassa aliwataka Mameya na viongozi wengine wa CHADEMA jijini humo kukataa kutoa mikataba ya aina yoyote kienyeji na kushughulikia suala la maegesho, ili isifike mahali wananchi wakajuta kuichagua CHADEMA na kusema afadhali CCM.

Zabuni ya maegesho jijini Dar es Salaam imetolewa kwa kampuni ya Kenya ambayo imeongeza tozo ya kuegesha gari kutoka Sh 300 hadi Sh 500 kwa saa. Alisema kero ambayo wamekuwa wakikutana nayo katika mikutano yao ni wananchi kutaka uongozi, jambo ambalo alisema kama ingepatikana Katiba mpya zingeongezwa nafasi zaidi za kuteuliwa.
 
Ukizeeka, hata kufikiri ni kitoto kitoto tu. Lowassa mawazo yake yanazidi kurudi nyuma
 
Sio kwa kishindo ni "asubuhi". "Ninyi kazi yenu kupiga kula, kulinda niachie mimi"

.burula wanaendelea kudanganywa na wanaleta kwa ..laza wenzao.
 


MJUMBE wa Kamati Kuu ya Chadema, Edward Lowassa, amesema kwa hali ilivyo na inavyoendelea nchini kuna kila dalili za chama hicho kushinda uchaguzi mkuu mwaka 2020.
Lowassa alisema hayo Dar es Salaam, wakati kuna kilio kikubwa cha wananchi wanaolia kukabiliwa na hali ngumu ya kiuchumi, huku wengi wakidhani imesababishwa na kubana matumizi kunakofanywa na Serikali.
Alisema hayo wakati akifungua semina kwa wabunge, mameya na madiwani wa chama hicho wa Jiji la Dar es Salaam ikilenga kujadili kazi waliyofanya ya kutumikia wananchi kwa mwaka mmoja na namna ya kupiga hatua miaka minne ijayo.
Alifafanua: ”Nimepita maeneo mengi kufanya mikutano ya ndani, kwa hali ilivyo tunakubalika mno, tuna dalili zote za kushinda uchaguzi mkuu wa 2020, tujitahidi kuwa na umoja, bila umoja hatuwezi kushinda ni muhimu sana, CCM wanajua maana ya umoja na wanaung’ang’ania, tuangalie sana maneno ya kutugawa tusiyakubali.’’
Alisema Chadema itapita maeneo ambayo watu wako nyuma kielimu ambayo kwa kiasi kikubwa wameipigia kura CCM, ili kuwaelewesha nia njema ya kuwaletea maendeleo na kuwapa elimu.
‘’Muda uliobaki ni mchache, tunatakiwa kuamka ili chama chetu kishinde kwa kuwa tumeshakifikisha sehemu nzuri, hatuna muda tuchangamke kila mmoja aone kwamba anapaswa kueleza namna ya kukisaidia chama kivuke,’’ alisema Lowassa.
Kuhusu mikutano ya ndani ambayo aliita ‘mitamu’ zaidi, alisema vimefanya wamekuwa imara zaidi, kwani wamezungumza na wanachama wao maeneo mengi wakiwa wanaonana kwa karibu.
‘’Tumekuwa mikoani na viongozi wenzangu, tumezunguka mikoani hali ni nzuri kwa mazungumzo tuliyofanya na wanachama wetu, vikao ni vitamu zaidi kuliko vya nje, unapata nafasi ya kuongea na wananchi ana kwa ana kwa muda mrefu, kwa mapenzi na mahaba yote,’’ alisema Lowassa.
Lowassa aliwataka mameya na viongozi wengine wa Chadema jijini humo kukataa kutoa mikataba ya aina yoyote kienyeji na kushughulikia suala la maegesho, ili isifike mahali wananchi wakajuta kuichagua Chadema na kusema afadhali CCM.
Zabuni ya maegesho jijini Dar es Salaam imetolewa kwa kampuni ya Kenya ambayo imeongeza tozo ya kuegesha gari kutoka Sh 300 hadi Sh 500 kwa saa.
Alisema kero ambayo wamekuwa wakikutana nayo katika mikutano yao ni wananchi kutaka uongozi, jambo ambalo alisema kama ingepatikana Katiba mpya zingeongezwa nafasi zaidi za kuteuliwa.
New version ya Safari ya matumaini lazima itafeli tena.JPM 2015-2025.
 
nchi gani ??? tanzania au ile nchi ya mioyoni mwetu (ambayo wwe ndo raisi)....kwa tanzania haiwezekani
 
New version ya Safari ya matumaini lazima itafeli tena.JPM 2015-2025.

Magufuli allikuwa anashughulikia wafanyakazi hewa,wanafunzi hewa nk sasa Lowasa anatoa matumaini hewa! KWELI NIMEAMINI VITA YA KUPAMBANA NA VITU HEWA BADO KUBWA
 
Hats 2015 ilikuwa hivyo hivyo. What next? Na hata kwenye CCM ilikuwa hivyohivyo.
 
Yaelekea Lowassa naye ameamua kuendekeza siasa za mizaha kwa kuwaona Watz. ni villazzza ilimuradi tu aendelee kupata airtime ya umaarufu siku zinavyoenda kama alivyozoea. Kwanza, aseme alishindwaje 2015 na ni kipi hasa kitakachobadilika kuipa ushindi CHADEMA - au chama chochote cha upinzani hapa nchini.
 
Wanasiasa kama Lowasa ni watu muhimu sana kwenye mataifa haya ya Afrika kwa sababu wanaepusha vurugu zinazoweza kusababishwa na wafuasi wao wenye uchu wa kushinda uchaguzi ikifika 2020 atasema tutashinda 2025 ikifika 2025 atasema tutashinda 2030 miaka inasogea na maisha yanaenda wafuasi wake wanakuwa na imani tu ya kushinda uchaguzi unaofuata kwahiyo hakuna vurugu wala matatizo yatakayotokea Mungu akubariki Edo Lowasa uishi maisha marefu ukiendelea kuwa mgombea wa kudumu wa urais wa chadema hadi 2040.
Yeye nani aweze kukusababisha wafuasi wake walete vulugu wakati Nchi ina mifumo yake ya kuzuia vulugu na uvunjaji wa amani.Ushaona kiongozi gani wa Tanzania alisha imiza wafuasi walete fujo na yeye akafanikiwa na dhamiara yake hiyo...ebu nitajie...uenda mnajiaminisha kuwa USALAMA wa TAIFA hili uko mikononi mwa baadhi ya watu fulanifulani viongozi...thubutu yake....
 
Hamfikirii maendeleo ya nchi, mnafikiria kwenda Ikulu tu - Ikulu ni mahali patakatifu na wanaombewa kukaa kule ni viongozi wasiokuwa waroho, wezi, mafisadi, wanyang'anyi nk.

Ombeni kwenye jukwaa msikutane na akina January, Mwigulu, Msakila, George nk CDM hakuna chenu 2020 labda ushindi wa pili au tatu!
 
Bila ya Time huru hakuna liwalo. Mfano mzuri ni Zanzibar yamebaki malumbano tu
 
Hamuwezi kushinda uchaguzi wa raisi kwa katiba ya kidikteta, hata watanzania wote wakipigia kura upinzani.
 
Kwa katiba hii Labla miaka 3000 ijayo
 
Hapo ni lazima ssa viongozi wetu wadai katiba mpya na tume huru otherwise tutaishia kulalamika kuibiwa tena 2020.
Bila Tume huru,katiba huru asahau,hakumbuki kuwa ma Rc,Ma DC,ma DEd wote makada wa ccm
 
Nmeota 2020 wananchi wataenda idodomya kumchukulia mkulu form za kugombea urahisi
 
Back
Top Bottom