Lowassa: Sikuhitajika na Wakubwa!

Lowassa: Sikuhitajika na Wakubwa!

Ozzie

Pole laigwenan kwa ndoto yako na wanaokuunga mkono kuzimwa. si lazima uwe rais kuitumikia jamii. wewe ulishakua kiongozi wa jamii ya watamzania na kazi yako njema imeonelamna. endelea kuiongoza jamii ya watanzanii kwa namna mungu amekujalia wala usikate tamaa.
 
Last edited by a moderator:
Lowassa hakuna chenye mwanzo kikakosa mwisho
 
Tuko nae till the end...Mungu anakusudi na huyu mzee.Saa ya ukombozi imewadia.Misukosuko aliopitia huyu mzee ina hatima njema.Mungu sio dharimu na wala hadhihakiwi.

Mungu ni wa Lowassa peke yake?? Kulikuwa na wagombea wengine 37 pamoja na yeye, wengine sio wa Mungu??
Au mlidanganywa na manabii wenu uchwara Gwajima na TB Joshua kuwa Lowassa atakuwa rais??
Ninyi mlimsikia wapi Mungu akisema Lowassa atakuwa rais.

Acheni kutuzingua na Lowassa wenu.
 
......TATIZO NI CHUKI NA CHAMA KUWEKWA MIFUKONI NA WACHACHE.........ambao wamejimilikisha kuona ccm ni yao!! na si yetu SOTE.
 
Huo ujumbe haujaandikwa na Lowassa. Tumuache mzee apumzike kwani yupo katika kipindi kigumu. Hivyo nawasihi sana msitumie vibaya ukimya alio nao kumfitinisha/thihaki wapendwa wake.
 
Kuna watu humu jf walimshauri vizuri sana hakutaka kuwasikia, na bado wanaendelea kumshauri na ushauri wenyewe ni huo wa kumtaka apumzike, afanye mambo yake tofauti na siasa lkn naona bado mzee wa Monduli kashupaza shingo, mwisho itavunjika......nimegundua washauri wake wanashinikizwa na hela ila hapa JF wanaangalia uhalisia.

Inawezekana huwa hapitii huo ushauri au hayumo humu JF au washauri wake hawamfikishii yale yanayoelezwa na watu humu jf.
 
Kuna watu humu jf walimshauri vizuri sana hakutaka kuwasikia, na bado wanaendelea kumshauri na ushauri wenyewe ni huo wa kumtaka apumzike, afanye mambo yake tofauti na siasa lkn naona bado mzee wa Monduli kashupaza shingo, mwisho itavunjika......nimegundua washauri wake wanashinikizwa na hela ila hapa JF wanaangalia uhalisia.
Huu ndio mustakabali wake bora kwa sasa aachane na siasa; hana nguvu tena aliyokuwa nayo kabla ya mgombea rasmi kutangazwa. Angetaka kubakiza matumaini yake angefuata daraja alilowekewa na Nchimbi na wenzie. Palepale aliposikia kakatwa tu angeitisha press conference mbele ya mashabiki wake na kuchana kadi ya sisiem mbele zao na kutangaza aliye wa kwake amfuate na kuondoka zake mda huohuo kuelekea Monduli. Ule mchakato ungesitishwa ghafla na wazee wote wangeikimbia Dodoma na angekuwa na turufu ya kujadiliana; kwa sasa hana kitu tena, kakosea taimingi na imekula kwake.
 
Makubwa. Mi siku zote najuaga Lowassa ndiye Mkubwa. Rejea..... Hakatwi mtu hapa..... Na asiyenitaka CCM aondoke mwenyewe.
Sasa kutuambia tena kuna "wakubwa" wasiomtaka, anatuchanganya banaa... Ah
 
Mungu ni wa Lowassa peke yake?? Kulikuwa na wagombea wengine 37 pamoja na yeye, wengine sio wa Mungu??
Au mlidanganywa na manabii wenu uchwara Gwajima na TB Joshua kuwa Lowassa atakuwa rais??
Ninyi mlimsikia wapi Mungu akisema Lowassa atakuwa rais.

Acheni kutuzingua na Lowassa wenu.

Hakuna ushahidi wowote kuwa TB Joshua alimwambia Ngoyai kuwa atakuwa rais. Na alishaacha siku nyingi safari za kwenda Lagos
 
Njooni kwetu chadema, CCM walikupenda lakini CHADEMA imekupenda zaidi.
 
Lowassa asilie lile kama vile mama yake ndiye aliyezaa rais tu, na hivyo ilikuwa haki yake. Alshafanya makosa mengi sana katika maisha yake ya kisisasa ambayo yalishamksesha sifa nyingi za kuongoza lakini bado alikuwa anang'ang'ania tu akihangaika na kutoa hongo za namna mbalimbali kusudi tu achaguliwa kuwa rais.

Kosa lake kubwa alijiaminisha kuwa ataukwaa urais na atautumia kuwalipiza kisasi aliowaona "maadui" zake. Huwezi kuwa kiongozi iwapo unajenga makundi ndani ya watu unaotaka kuwaongoza kwa kutenganisha watu wako na maadau ambao watu ni kundi la unaotaka kuongoza. Kwa miaka saba yote aliyolazimika kuachia uwaziri mkuu, yeye ameitumia kujenga uadui zaidi na watu wengi ingawa pia aliitumia kujitengezea kundi kubwa la watu wake. Angekuwa na busara, angeitumia miaka hiyo kuondoa tofauti baina yake na wale anaoona kuwa ni maadui.



attachment.php


Kwa sasa hivi alitakiwa awe amekomaa vya kutosha kujua kuwa hata mwaka 2005 Malecela (tingatinga) aliyekuwa na mvuto mkubwa sana ndani ya CCM wakati huo naye alitolewa kwa njia hii hii iliyotumika kwake, tena afadhali wakati huu waliotolewa walikuwa wengi sana. Mzee yule alikubali matokeo akatulia,. lakini yeye huyu Lowassa anaonekana kupatwa na kiwewe kabisa.
 
mi namheshimu sana huyu mzee lowasa amekejeliwa sana tena sana na bado TBC kuna kipindi maalumu cha igizo linaitwa chondechonde wanamkejeli lakini harbinder seth. mwinikulu, na ma escrow yote yanatukuzwa, watanzania tuna minyoo ya ubongo
 
Waliokuwa wanamsifia lowassa na kujitapa kuwa "hakatwi mtu hapa" mbona siwaoni tena?
Mkuu sasa wanataka kuhamia Chadema halafu wakihamia huko waanze ngonjera zao za ''hakatwi mtu hapa'' sasa wanatafuta njia za kuishi kwa kupitia ''kwa mtia nia aliyekatwa ''mwache Mbowe na baba mkwe wake wajitie kiherehere cha kuwakaribisha wahuni wanaozomea viongozi wao na wapenda rushwa ,huo utakuwa mwanzo wa mwisho wa Chadema.
 
Back
Top Bottom