kamwe lowassa hawezi kuwa kama zuma kwa sababu nyingi tu na chache kati ya hizo ni hiziz:
1. Hana support yoyote toka kwa wafanyakazi wa nchi hii ambao kwa sa ndiy walikuwa instrumental katika kumnyanyua zuma;
2. Zuma alikuwa na eloquence ya hali ya juu na alishuka mpaka kwa watu wa kawaida na vijana ambao ndiy walikuwa chachu ya ushindi wake. By the way huyu wa kwetu hapa amewahi hata kufanya mahojiano na vyombo vya habari vya kimataifa kama bbc, sauti ya ujerumani au hata voa? Kwa lugha gani?;
3. Mbeki alionekana kama mtu ambaye anajali maslahi ya matajiri na watu weupe na kuwaacha watu weusi na wala wa kima cha chini (kwa hapa kwetu sifa hizi za mbeki ndizo za lowassa);
4. Zuma alikuwa na constituency, kwa maana ya kwamba alikuwa ni 'undisputed king' wa wazulu na hao walimpa boost kubwa hasa kwa vile ndilo kabila kubwa kuliko yote. Huyu bwana hapa kwetu hata hao wamasai wenyewe wamem-disown wakidai ni mmeru na hata wangemuunga mkono, hawatoshi kumpa jeuri.
5. Kwa ujumla uungwaji mkono wa huyu bwana umebaki kwa wenye njaa wachache wanaoingia kwenye vikao vya chama na wengine sasa wameanza kumgundua na kuchoshwa na hila zake za hujuma na kiu yake ya kuutaka urais.
Kama yote hayo alisingiziwa ilikuwaje akajiuzulu?Naona unachanganya mada kwa kutoelewa au unafanya makusudi kumbebesha Lowasa tuhuma zisizo mhusu: 1: Wakati Richmond inapokelewa na kupewa mikataba Lowasa hakuwa anahusika kwa aina yoyote ile: hakuwa waziri mkuu wala waziri wa nishati- nieleze anahusikaje na Richmond.2 wakati wa scandal ya bulyanhulu hakuwa muhusika pia. 3. Kumbuka kuwa kamati ya mwakyembe haikumuhoji na ilitoka na maamuzi bila kuzingatia ushauri alioutoa wakati akiwa madarakani. Kwa kifupi tuhuma za watu dhidi ya Lowasa ni za kutunga kwa malengo ya kisiasa.
Hayo uliandika juu mbona mengi hayakutokea kipondi akiwa waziri mkuu yeye, mf. No.1: shule za kata zilianza kujengwa wakati wa mkapa.Wana JF, katika kipindi kifupi ambacho mh, Edward Lowasa aliongoza serikali maendeleo yaliweza kuonekana. Nitaje mambo machache ambayo ni miale ya maendeleo iliyooneshwa na huyu kiongozi shupavu: 1. Kila kata kujenga shule ya sekondari.2. Wanafunzi waliomaliza kidato cha sita kupata kozi ya muda mfupi ili kuongeza idadi ya walimu na kupunguza upungufu.3. Kila kata kuwa na kituo cha afya.4. Kuukataa mkataba usio na maslah wa mamlaka ya maji safi na maji taka DSM.5. Kufuta ada ya kudahiri watoto wanaoingia darasa la kwanza hivyo kuongeza idadi ya wanaoingia darasa la I.Ama kwa hakika tulikuwa bado tunamuhitaji na kama angeendelea kuwepo madarakani huenda sasa kila mkoa ungekuwa angalau na VETA kama siyo chuo kikuu.
Huna habari, mwaka 2015 EL atajiunga na CHADEMA na kuteuliwa kuwa mgombea urais kupitia chama hicho. Na mazungumzo kati yao yameisha kamilika inasubiriwa muda tu
Wkt huohuo ukiri kwamba hakuhusika katika Richmond. Na uache kutumwa na watu kumchafua pasipo na ukweli(maana sababu za kilazimisha kuwa yeye anauhusiano na richmond unazowewe pekeee).....na kungekuwa na Richmond katika kila sekta.
Asant kwa kiniunga mkono japo unafikiri unanipinga, kwa hiyo umekubali kuwa Lowasa alifanya haya: 1: "Lowasa alihimiza kuwa kila kata ijenge shule na seko ili 80% ya watoto wanaomaliza drs la saba waende sekondari. 2: akiwa waziri wa maji alifuta mkataba wa Dawasco. Lakini bado hutaki kuukubali utendaji wake!?.Hayo uliandika juu mbona mengi hayakutokea kipondi akiwa waziri mkuu yeye, mf. No.1: shule za kata zilianza kujengwa wakati wa mkapa. No.2: hiyo ilikuwa kipindi chake lakini ilprove failure maana watoto walikuwa hawaelewi.No.3: Hiyo ya kila kata kuwa na kituo cha afya hapa dsm tu kata kibao hazina hata hiyo zahanati labda ungesema kila tarafa kuwa na kituo cha afya ningekuelewa.No.4: aliifanya akiwa waziri wa maji na maendeleo ya mifugo hakuwa waziri mkuu.No.5: ilifanyika mwaka wa kwanza tu wa uongozi wa Mkapa na sio kipindi cha Lowasa alivyokuwa waziri mkuu.