Lowassa kurejesha fomu kesho

Lowassa kurejesha fomu kesho

PISTO LERO

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2011
Posts
2,819
Reaction score
1,455
Taarifa inatolewa kwa vyombo vya habari, wanachama, wafuasi, wapenzi, mashabiki wa CHADEMA na umma wa Watanzania kwa ujumla kuwa baada ya hatua ya kuchukua fomu ya kuwania uteuzi wa ndani ya chama kugombea nafasi ya urais,

Mheshimiwa Edward Ngoyai Lowassa kesho Agosti 1, 2015 atarejesha fomu yake kwa ajili ya taratibu zingine za ndani ya

Shughuli hiyo itafanyika kuanzia saa 9.00 jioni, ambapo mgombea atakabidhi fomu yake Ofisi ya Katibu Mkuu, Makao Makuu ya Chama, Kinondoni, jijini Dar es Salaam katika hadhara ikayohudhuriwa na viongozi wa chama, wanachama, wafuasi, wapenzi na mashabiki wa CHADEMA kutoka sehemu mbalimbali.

Mheshimiwa Lowassa atarejesha fomu hiyo akiwa mgombea pekee baada ya kuwa ametimiza taratibu za kikatiba hususan kupata wadhamini kutoka mikoa mbalimbali nchi

Hatua hiyo ya kurejesha fomu itafuatiwa na taratibu zingine za kikatiba, ikiwa ni pamoja na vikao vya uteuzi ambavyo vitaketi kwa mujibu wa ratiba ambayo imeshapangwa na chama.
Makene
 
hakuna haja ya wadhamini inatosha hivo hvo. Poa mkubwa ahsante kwa taarifa
 
huyu jamaa tangu akatwe na CCM yaani ndio amejiongezea mashabiki ambao mara ya kwanza hawakuwa upande wake nikiwemo mimi.
Hakika mwaka huu CCM wakae mkao wa kukabidhi Magogoni kwa hiari na Magufuri ajiandae kuwa Mwenyekiti wa CCM tu.
 
lowasa hamna kitu maana nae ni ccm b kwa hiyo piga hawezi kuwaangusha ccm a. ccm wanaakili sana wamempandikiza lowasa huko
 
Back
Top Bottom