Venance Mchael
New Member
- Oct 8, 2016
- 4
- 3
Na bado tutaisoma
Namwonea huruma lowassa bora atulie tu.View attachment 424349
Aliyekuwa mgombea urais kupitia CHADEMA, Edward Lowassa amechambua mwaka mmoja wa uongozi wa Rais John Magufuli tangu aingie madarakani akisema kuna mafanikio machache katika baadhi ya maeneo, lakini maisha ya wananchi yamezidi kuwa magumu.
Lowassa ambaye katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, 2015 aliungwa mkono na vyama vya upinzani vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), alisema hayo jana katika andishi lake kwa vyombo vya habari.
Mwanasiasa huyo aliyewahi kuwa waziri mkuu katika Serikali ya Awamu ya Nne kabla ya kujiuzulu mwaka 2008, amesema katika andishi hilo kwamba, “kile ambacho tulikisema wakati ule kwa nini tunataka mabadiliko, hivi sasa kila mtu anakiona.
“Kwamba pamoja na mafanikio machache katika baadhi ya maeneo, lakini maisha yamezidi kuwa magumu, ajira imeendelea kuwa bomu linalosubiri kulipuka, elimu bure iliyoahidiwa siyo inayotekelezwa, utumishi wa umma umekuwa kaa la moto.”
Chanzo: Mwananchi
kama mimi kichaa na yule ambaye kachimbia michango ya waanga utamwita nani?labda rais Wa watanzania vichaa kama wewe!!
swiss kwa vijembe mficho kama JK! lolwewe piga box tu waache watanzania na mambo yao
swissme
Huyu mzee pammoja na kua na yuhuma hapa na pale lakini hua anaongea kiistarabu sana. Atakosoa bila ya kukashifu au kukebeheTwo words to describe Lowassa, the diplomatic and a politician....
Kaongea kistaarabu Sana.....
Huna sifa za kumuonea huruma Lowassa, yeye ndio anatakiwa kukuonea huruma wewe! Hivi nyinyi mbweha wa kijani huwa mnafikiria kwa kutumia viungo vyenu vya kukalia au kichwa? Huna hata senti moja mfukoni halafu eti "namuonea huruma Lowassa"!Namwonea huruma lowassa bora atulie tu.
Iyo ni tathmini ya mwaka mmoja hujui ya miaka mingine itakua vipi...Ajipe muda, awamu ni miaka 5 na kazi zinaendelea, kwani yeye angetekeleza ahadi zake kwa mwaka mmoja?
Ha ha ha hakuna kitu kigumu kama kumiliki akiliMzee wa mvua za Thailand kaona aingie front mwenyewe baada ya wafuasi wake kuendelea kupotezwa na utendaji safi wa awamu hii!
Hata CCM ni wa ajabu pia, juzi juzi mnabana pua kukataa misaada ya nchi za magharibi kwa madai ya kumudu kujitegemea halafu leo mnaomba msaada kujengewa msikiti na uwanja wa mpira na nchi nyingine ya Afrika.Ila CHADEMA watu wa ajabu sana, Duniani kuna vituko leo hii Luwasa ni CHADEMA damu damu na wao wanashangilia.
Mwenyekiti CCM JF
View attachment 424349
Aliyekuwa mgombea urais kupitia CHADEMA, Edward Lowassa amechambua mwaka mmoja wa uongozi wa Rais John Magufuli tangu aingie madarakani akisema kuna mafanikio machache katika baadhi ya maeneo, lakini maisha ya wananchi yamezidi kuwa magumu.
Lowassa ambaye katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, 2015 aliungwa mkono na vyama vya upinzani vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), alisema hayo jana katika andishi lake kwa vyombo vya habari.
Mwanasiasa huyo aliyewahi kuwa waziri mkuu katika Serikali ya Awamu ya Nne kabla ya kujiuzulu mwaka 2008, amesema katika andishi hilo kwamba, “kile ambacho tulikisema wakati ule kwa nini tunataka mabadiliko, hivi sasa kila mtu anakiona.
“Kwamba pamoja na mafanikio machache katika baadhi ya maeneo, lakini maisha yamezidi kuwa magumu, ajira imeendelea kuwa bomu linalosubiri kulipuka, elimu bure iliyoahidiwa siyo inayotekelezwa, utumishi wa umma umekuwa kaa la moto.”
Chanzo: Mwananchi