Shobi
JF-Expert Member
- May 31, 2015
- 3,401
- 4,371
Natuma salamu za rambirambi kwa familia, ndugu na marafiki, wananchi wa jimbo la Ulanga pamoja na watanzania kiujumla kufuatia kifo cha ndugu yetu mpendwa Mheshimiwa Celina Kombani.
Binafsi nimewahi kufanya kazi na Mheshimiwa Kombani kama naibu waziri kwenye wizara yangu na ninamkumbuka kwa moyo wake wa kujituma na uchakapazi wake.
Mimi na Regina tunaomboleza msiba huu mkubwa kwa taifa huku tukizidi kumuomba Mungu ampe pumziko la milele. Tunaiombea familia, ndugu pamoja na marafiki waweze kupita kipindi hiki kigumu na Mungu awape nguvu na ujasiri kwa kumpoteza mpendwa wenu.
Edward na Mama Regina Lowassa pamoja na familia nzima.
Binafsi nimewahi kufanya kazi na Mheshimiwa Kombani kama naibu waziri kwenye wizara yangu na ninamkumbuka kwa moyo wake wa kujituma na uchakapazi wake.
Mimi na Regina tunaomboleza msiba huu mkubwa kwa taifa huku tukizidi kumuomba Mungu ampe pumziko la milele. Tunaiombea familia, ndugu pamoja na marafiki waweze kupita kipindi hiki kigumu na Mungu awape nguvu na ujasiri kwa kumpoteza mpendwa wenu.
Edward na Mama Regina Lowassa pamoja na familia nzima.