OgwaluMapesa
JF-Expert Member
- May 24, 2008
- 10,942
- 437
Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, amesema hatakubali kuona kiasi kikubwa cha magadi soda kilichogundulika katika Kijiji cha Engeruka Juu, kinageuzwa na baadhi ya watu kuwa balaa kwa wakazi wa eneo hilo badala ya kuwa neema kwao.
Badala yake amewataka wanakijiji hao kujipanga vizuri ili kujiendesha kibiashara kwa manufaa yao na taifa kwa jumla.
Lowassa ambaye pia ni Mbunge wa Monduli (CCM), alifanya ziara ya kikazi ya siku moja kuzungumza na wakazi wa kijiji hicho kuhusu miradi ya magadi soda, umeme, barabara na maji.
Alisema hivi karibuni kumekuwa na ugomvi mara kwa mara katika rasilimali ya ardhi, lakini kwa eneo la Engaruka hakuna tatizo hilo.
Aliwaonya wakazi hao kuacha kushawishiwa na watu wachache kuuza maeneo yao kwa tamaa ya fedha za sasa, lakini hapo baadaye wakajikuta hawana kitu na kubaki kuwa maskini.
Akizungumzia mradi wa magadi soda, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa NDC, Mlingi Mkucha, alisema utafiti waliokuwa wamefanya umebaini kuwapo kwa mita za ujazo trilioni 4 na milioni 700 za magadi soda katika eneo hilo, hali ambayo inaifanya Tanzania kuwa nchi ya tatu kwa kuwa na akiba kubwa ya magadi soda baada ya Marekani na Uturuki.
Chanzo: Nipashe
Badala yake amewataka wanakijiji hao kujipanga vizuri ili kujiendesha kibiashara kwa manufaa yao na taifa kwa jumla.
Lowassa ambaye pia ni Mbunge wa Monduli (CCM), alifanya ziara ya kikazi ya siku moja kuzungumza na wakazi wa kijiji hicho kuhusu miradi ya magadi soda, umeme, barabara na maji.
Alisema hivi karibuni kumekuwa na ugomvi mara kwa mara katika rasilimali ya ardhi, lakini kwa eneo la Engaruka hakuna tatizo hilo.
Aliwaonya wakazi hao kuacha kushawishiwa na watu wachache kuuza maeneo yao kwa tamaa ya fedha za sasa, lakini hapo baadaye wakajikuta hawana kitu na kubaki kuwa maskini.
Akizungumzia mradi wa magadi soda, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa NDC, Mlingi Mkucha, alisema utafiti waliokuwa wamefanya umebaini kuwapo kwa mita za ujazo trilioni 4 na milioni 700 za magadi soda katika eneo hilo, hali ambayo inaifanya Tanzania kuwa nchi ya tatu kwa kuwa na akiba kubwa ya magadi soda baada ya Marekani na Uturuki.
Chanzo: Nipashe