VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,004
Waziri Mkuu Mjiuzulu na Mbunge wa Monduli,Edward Ngoyai Lowassa,amesema kuwa Jiji la Arusha ni gumu sana kisiasa hasa upande wa CCM. Lowassa aliyasema hayo jana hapa Arusha alipokuwa akizindua kampeni yake ya kichama ya kuwasaidia madereva wa pikipiki maarufu kama boda boda. Lowassa,dhahiri kabisa,alishangazwa na mapokezi hafifu ya kichama aliyoyapata huku akiarifiwa kuwa ziara hiyo haikubalikiwa na chama kiwilaya,kimkoa na hata kitaifa.
'Vijana wa Arusha wana bashasha kubwa. Ni wasikivu na waelewa.Lakini hawatabiriki kimaamuzi hasa ujapo wakati wa uchaguzi;wao na CHADEMA na CHADEMA na wao. Hapa pagumu sana.Arusha ni 'stronghold' ya CHADEMA' alisema Lowassa akionesha ukweli wa anachokisema.
'Nitakuwa makini na nivifanyavyo hapa Arusha kichama na kibinafsi' aliongeza Lowassa.
Chanzo: Mimi niliyekuwepo Arusha na sasa najiandaa kurejea Dar.
VUTA-NKUVUTE aka Mzee Tupatupa wa Lumumba Dar (sasa Arusha)
'Vijana wa Arusha wana bashasha kubwa. Ni wasikivu na waelewa.Lakini hawatabiriki kimaamuzi hasa ujapo wakati wa uchaguzi;wao na CHADEMA na CHADEMA na wao. Hapa pagumu sana.Arusha ni 'stronghold' ya CHADEMA' alisema Lowassa akionesha ukweli wa anachokisema.
'Nitakuwa makini na nivifanyavyo hapa Arusha kichama na kibinafsi' aliongeza Lowassa.
Chanzo: Mimi niliyekuwepo Arusha na sasa najiandaa kurejea Dar.
VUTA-NKUVUTE aka Mzee Tupatupa wa Lumumba Dar (sasa Arusha)
Last edited by a moderator: