Tangu wamkata jina mapema huyu Mtu abakia kuwa na nguvu tena nathubutu kusema ndio kwanza nguvu zake zimeongezeka zaidi na ile hali ya kukubalika kwa Wananchi ndio inajidhihirisha zaidi kuliko Mwanasiasa awaye yote ndani ya CCM.
CCM wanajuta!!! kwanini waliamua ovyo kiasi hicho,wanahaha kusikia LOWASSA aweza hamia CHADEMA/UKAWA.Ndani ya CHAMA CHA MAPINDUZI hali sio shwari wamebaki kutupiana lawama.Lakini pamoja na hayo yote,Inaonekana kila kitu kinaharibika upande wa CCM,vichwa vyao vinauma,Walidhania kulikata jina la LOWASSA lisiingie hata kwenye tano bora huko ndio kuyazuia Mafuriko kwa Mkono.Mbaya zaidi hawataki kusikia LAIGWANANI aweza kutua CHADEMA.
Ni hatari zaidi ikitimia kweli ikawa hivyo ndivyo ilivyo EDWARD LOWASSA kuhamia upinzani,ENYI MACCM hamkuliwaza hilo???
Je! Litabakia jiwe juu ya jiwe huko CCM?
Hamkujua kuwa anakubalika na kupendwa sana na wengi ndani na nje ya ccm?
Siasa za kweli hazina adui wala ndugu wa Kudumu,sio ajabu Laigwanan kupokelewa UKAWA,Ukizingatia Intelejensia ya CHADEMA iko juu sana kuliko ya CCM,Siku zote wamewazidi kete kwa mambo ya Msingi ccm hukosa point lakini chadema huonyesha njia ama majawabu kwa UMMA wa WATANZANIA.Maana yake CHADEMA wanajua vizuri sana Lowassa sio FISADI vile,ila kwa kuwa alikuwa kwenye Mfumo mbovu ilipendeza kwa wakati huo kumjumuisha na Magamba yote.
Ni shauku yangu kubwa kusikia EDWARD NGOYAI LOWASSA KAHAMIA RASMI CHADEMAUKAWA.
Najua wabaya wake hamtaki nisema maneno haya.
Ila Lugha hii inasound vizuri sana kwa wapenda mabadiliko.
JARIBU KUFIKIRI KIDOGO
Chadema wamekuwa na mikakati mikali sana na hakika wamejiandaa vema kuiongoza Nchi hii,I SEE THE NEW COUNTRY WAS CAME IN OCTOBER 2015 AFTER ELECTION.
CHADEMA walishandaa siku mingi sana,kila kata watu mia mbili ambao hata ufanya nini kamwe hawawezi kukisaliti chama, hizo ni KURA za uhakika na bado wafurukutwa,wapambe,wakereketwa na wanachama wengine hai jumlisha UKAWA jumlisha LOWASSA kwa mtindo huo CCM haitaweza kusimama kamwe mbele ya UPINZANI.
Hata sasa pamoja na Mh.LOWASSA yuko kimya hicho kimya chake kina mshindo mkuu,Na hio inabainisha huyu mtu ni mbeba tu mpaka kesho.Hapa tulipofika ni patamu sana tena sana kilichobakia ni WANANCHI kushuhudia kuona LOWASSA akifanya Maamuzi magumu ya kuhama CCM na kuhamia CHADEMA.
WANANCHI WANAFURAHIA MABADILIKO KULIKO WAKATI WOWOTE ULE.