Lowassa anaudhoofisha upinzani

Lowassa anaudhoofisha upinzani

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
219,504
Reaction score
911,249
Lowassa alijiunga upinzani baada ya kudhulumiwa Urais ccm. Vinginevyo hakuwa na khoja ya kuwa mpinzani. Hivyo, ni masilahi binafsi siyo sera zimempeleka upinzani.

La ajabu, upinzani uchwara tulionao unamwona ni JEMBE!

Lowassa siyo mpinzani hata chembe ila anatumiwa na ccm kudhoofisha upinzani.

Maswali ya kujiuliza

1) Mbona hasumbuliwi kwa kuwekwa ndani na kufikishwa Mahakamani kama wengine?

2) Mbona hakerwi na mfumo mzima wa chaguzi zetu? Lini ulimsikia akihimiza mageuzi ndani ya sheria za uchaguzi hususani NEC?

3) Mbona hajawahi kuomba msamaha kwa kuwapotosha wapigakura alipowaahidi suala la kulinda kura ni lake aachiwe na baada ya kushindwa akadai aliibiwa?

4) Mbona hadi leo hajatoa majumuisho ya kura alizozipata hususani fomu za vituo na za majimbo kutuhakikishia ya kuwa alishinda kwa 62% kama alivyodai?

5) Mbona hadi leo hajaenda Mahakama kuu kuiomba kibali cha kuhesabu kura zote ili tujue mbichi ni zipi ?

6) Mbona hajalalama marekebisho ya sheria za mgao wa ruzuku zinazolenga kuusambaratisha UKAWA?

7) Mbona hadi leo kaufyata kupigania haki ya kikatiba ya upinzani kuendesha shughuli zao bila vikwazo na vitisho?

NIONAVYO

Lowassa ni CCM mole yuko huko kuwadhoofisha kwa kuwatupia changa la macho kwa kuboresha ruzuku ili wasahau mambo ya kimsingi kama NEC kututendea haki wapigakura.

Lowassa has too much to lose and too much baggage to carry to represent a lynchpin of change we are looking for....
 
sawa, hayo ni maoni yako, sasa tusemeje ndugu? and infact kwa hoja zako humu there is no "lynch pin of change you are looking for"
 
Ila Magufuli kwa kukamata kamata na kunyima uhuru ndio anastawisha upinzani huku akitoa maagizo kuwa spika awashungulikie bungeni nae wakitoka huku nje atawashughulikia!!!

Hivi yule aliyekuwa akiripoti Central kila week kwa kosa la uchunguzi wa uchochezi baada ya kusema masheikh wa UAMSHO toka zanzibar walioshikiliwa Ukonga kwa miaka minne sasa huku kesi tunambiwa uchunguzi bado ni Baba yako ama baba watoto?!!!
 
Hahahaha ameamua awaache tu mkiwa na amani maana angeanza kudai haki kama alivyodai cjui Tanzania tungekuwa wap sasa so pengine kuna kitu amekiona mbele akaamua kutupilia mbali na kutulia
 
Ila Magufuli kwa kukamata kamata na kunyima uhuru ndio anastawisha upinzani huku akitoa maagizo kuwa spika awashungulikie bungeni nae wakitoka huku nje atawashughulikia!!!

Hivi yule aliyekuwa akiripoti Central kila week kwa kosa la uchunguzi wa uchochezi baada ya kusema masheikh wa UAMSHO toka zanzibar walioshikiliwa Ukonga kwa miaka minne sasa huku kesi tunambiwa uchunguzi bado ni Baba yako ama baba watoto?!!!
 
Kumbuka kwa miaka mingi Lowasa alikuwa ni mwenyekiti wa bunge kamati ya ulinzi na usalama.

Fuatilia sifa za mwenyekiti wa kamati hiyo kisha utaelewa undani wa Lowasa.
 
Ila Magufuli kwa kukamata kamata na kunyima uhuru ndio anastawisha upinzani huku akitoa maagizo kuwa spika awashungulikie bungeni nae wakitoka huku nje atawashughulikia!!!

Hivi yule aliyekuwa akiripoti Central kila week kwa kosa la uchunguzi wa uchochezi baada ya kusema masheikh wa UAMSHO toka zanzibar walioshikiliwa Ukonga kwa miaka minne sasa huku kesi tunambiwa uchunguzi bado ni Baba yako ama baba watoto?!!!
Aliekuambia kazi ya magufuli ni kustawisha upinzani ni nani? Subirini ndoto zenu za mchana za kushika dola zitimie ili muweze kuustawisha upinzani.
 
3) Mbona hajawahi kuomba msamaha kwa kuwapotosha wapigakura alipowaahidi suala la kulinda kura ni lake aachiwe na baada ya kushindwa akadai aliibiwa?

Lowassa ni msanii na alikiingiza chama na upinzani chaka kwa kuwalaghai wananchi waondoke vituoni baada ya kupiga kura, huku akijua fika njia pekee ya kuindoa CCM madarakani ilikuwa ni kupiga kura na kuzilinda..

Lowassa & Katibu mkuu Mashinji hawana jipya la kuweza kuusaidia upinzani na chama kwa ujumla..
 
Ni hivi mimi ni mshabiki wa upinzani na hasa cdm, sikuwahi kuumuunga mkono Lowassa na nililalamika kwamba lile ni kosa kubwa haswa baada ya ule upuuzi aliokuwa akiufanya Shibuda. Nilitarajia upinzani na hasa cdm watakuwa walijifunza kuhusu kupokea makapi toka ccm na kuyapa nafasi, cha kushangaza ndio wakafanya kosa kubwa kuliko yote ya kumpokea Lowassa na kumpa nafasi namba moja katika chama ya kugombea urais.

Matokeo yake baada ya Lowassa kuingia cdm, cdm kimegeuka kuwa chama cha kikondoo, hakuna lolote jipya aliloleta Lowassa ndani ya cdm zaidi ya kuwinda nafasi ya kugombea urais tena kwa faida ya CCM. Mambo yaliyoipa cdm nguvu huko nyuma yote yamemezwa na ujio wa Lowassa, kiasi kwamba wanaposema Mbowe na uongozi wa juu walihongwa kutoa nafasi ya kugombea urais kwa Lowassa inakuwa ni ukweli. Leo hii Magufuli na ubovu wake katika uongozi anaonekana ni bora kwani analinganishwa na Lowassa. Lowassa hajawahi kuwa mwanasiasa wa aina ya siasa za cdm, ubora wake wote huwa unaimbwa na wapambe lakini sio yeye.

Nashangaa wapenzi washabiki na wanachama wa cdm kuwa kimya wakati chama kimeendelea kufubaa kwa sababu ya uwepo wa Lowassa. Hili tukubali la kuendelea kuwa na Lowassa ndani y ya cdm ni kuimaliza cdm, ni wakati wa wote wanaoitakia mema cdm kupinga Lowassa kukaa nafasi za mbelembele kwenye mambo ya chama kwani hana mapenzi na chama zaidi ya kuhakikisha cdm inampa nafasi ya kufikia matakwa yake. Huyo Mbowe sio wa kumuacha tena aamue lolote kwani amekiharibu chama kwa faida yake ya muda mfupi.
 
Ni hivi mimi ni mshabiki wa upinzani na hasa cdm, sikuwahi kuumuunga mkono Lowassa na nililalamika kwamba lile ni kosa kubwa haswa baada ya ule upuuzi aliokuwa akiufanya Shibuda. Nilitarajia upinzani na hasa cdm watakuwa walijifunza kuhusu kupokea makapi toka ccm na kuyapa nafasi, cha kushangaza ndio wakafanya kosa kubwa kuliko yote ya kumpokea Lowassa na kumpa nafasi namba moja katika chama ya kugombea urais.

Matokeo yake baada ya Lowassa kuingia cdm, cdm kimegeuka kuwa chama cha kikondoo, hakuna lolote jipya aliloleta Lowassa ndani ya cdm zaidi ya kuwinda nafasi ya kugombea urais tena kwa faida ya CCM. Mambo yaliyoipa cdm nguvu huko nyuma yote yamemezwa na ujio wa Lowassa, kiasi kwamba wanaposema Mbowe na uongozi wa juu walihongwa kutoa nafasi ya kugombea urais kwa Lowassa inakuwa ni ukweli. Leo hii Magufuli na ubovu wake katika uongozi anaonekana ni bora kwani analinganishwa na Lowassa. Lowassa hajawahi kuwa mwanasiasa wa aina ya siasa za cdm, ubora wake wote huwa unaimbwa na wapambe lakini sio yeye.

Nashangaa wapenzi washabiki na wanachama wa cdm kuwa kimya wakati chama kimeendelea kufubaa kwa sababu ya uwepo wa Lowassa. Hili tukubali la kuendelea kuwa na Lowassa ndani y ya cdm ni kuimaliza cdm, ni wakati wa wote wanaoitakia mema cdm kupinga Lowassa kukaa nafasi za mbelembele kwenye mambo ya chama kwani hana mapenzi na chama zaidi ya kuhakikisha cdm inampa nafasi ya kufikia matakwa yake. Huyo Mbowe sio wa kumuacha tena aamue lolote kwani amekiharibu chama kwa faida yake ya muda mfupi.
Mwacheni wazir mkuu mstaafu akamilishe mission yake!
 
Lowassa alijiunga upinzani baada ya kudhulumiwa Urais ccm. Vinginevyo hakuwa na khoja ya kuwa mpinzani. Hivyo, ni masilahi binafsi siyo sera zimempeleka upinzani.

La ajabu, upinzani uchwara tulionao unamwona ni JEMBE!

Lowassa siyo mpinzani hata chembe ila anatumiwa na ccm kudhoofisha upinzani.

Maswali ya kujiuliza

1) Mbona hasumbuliwi kwa kuwekwa ndani na kufikishwa Mahakamani kama wengine?

2) Mbona hakerwi na mfumo mzima wa chaguzi zetu? Lini ulimsikia akihimiza mageuzi ndani ya sheria za uchaguzi hususani NEC?

3) Mbona hajawahi kuomba msamaha kwa kuwapotosha wapigakura alipowaahidi suala la kulinda kura ni lake aachiwe na baada ya kushindwa akadai aliibiwa?

4) Mbona hadi leo hajatoa majumuisho ya kura alizozipata hususani fomu za vituo na za majimbo kutuhakikishia ya kuwa alishinda kwa 62% kama alivyodai?

5) Mbona hadi leo hajaenda Mahakama kuu kuiomba kibali cha kuhesabu kura zote ili tujue mbichi ni zipi ?

6) Mbona hajalalama marekebisho ya sheria za mgao wa ruzuku zinazolenga kuusambaratisha UKAWA?

7) Mbona hadi leo kaufyata kupigania haki ya kikatiba ya upinzani kuendesha shughuli zao bila vikwazo na vitisho?

NIONAVYO

Lowassa ni CCM mole yuko huko kuwadhoofisha kwa kuwatupia changa la macho kwa kuboresha ruzuku ili wasahau mambo ya kimsingi kama NEC kututendea haki wapigakura.

Lowassa has too much to lose and too much baggage to carry to represent a lynchpin of change we are looking for....
I concur! Lowassa alikuwa asset kipindi cha uchaguzi, kwa sasa anaanza kuwa liability!
 
Thats your fair opinion,
Lowassa hajaua upinzani, siasa za sasa si siasa za kianaharakati au siasa za hoja kwa hoja...(Lissu ni classical example wa hili)
Pili indicator ya kujua kama upinzani umekufa au umedorora hadi sasa ni kura pekee...
Tukutane 2019 kwenye serikali za mitaa.

Hata hivyo nikubaliene na wewe kias kuwa upinzani wamegwaya kidogo.. na ukweli ni kwamba hii mikwara si ya kitoto...

Niongeze kusema pia kuwa Chadema inahitaji mabadiliko ya ngazi ya juu ya uongozi... tunataka watu wenye pumzi ndefu na wasioogopa kupoteza kitu...
1.Lissu
2.Lema
3.Msigwa
4. Masha
5.Wenje

Suala la dini hapo ni wao watakavoamua kubalancisha mambo

Hadi sasa huwezi acha mashine kama za kina Nyalandu, Mahanga, Sumaye et all wakabaki hivi hivi bila kazi maalumu...
Lazima washiriki kwenye kanda kadhaa katika kujenga chama kitakachoheshimiwa na top class citizen and business class.

Lowassa alicholeta chadema ni heshima kwa kundi na marika mbali mbali na madaraja ya juu ya wananchi.. hasa wafanyabiashara na viongozi wastaafu, si mtu wa kubeza hata kidogo kwa mpenda mabadiliko yeyote yule...
 
Back
Top Bottom