Lowassa aliona ukosefu wa ajira kwa Vijana kama Bomu; Mbunge Kishimba nae kagusia

Freddie Matuja

JF-Expert Member
Jul 21, 2018
1,467
2,861
Ndugu zangu,
Tanzania inapita kwenye kipindi cha mpito cha mageuzi ya kiuchumi. Na wakati wa kipindi hiki kuna nyimbo nyingi sana zinaimbwa kama namna ya kutatua tatizo la ajira. Edward Lowasa aliona tatizo la ajira kama bomu linalosubiri kulipuka, Jumanne Kishimba nae hana majibu ya nini kifanyike kwa vijana wake 6 waliomaliza chuo kikuu wakati huo aki-challenge thamani ya cheti cha mhitimu wa chuo kikuu maana kama anakosa ajira, kijana hana tools za kumsaidia kuyakabili mazingira yake.

Vyuo vikuu kwa sasa vinakomaa kuja na matangazo mengi kuwa aina ya kozi mpya wanazofundisha zitawafanya vijana wapete kazi, bila ya kuwa na majibu kazi watapata wapi.

Vijana wengi wawe wa vyuo vikuu au vyuo vya kati au walio maliza la 7, form 4 au VETA wote wana something to offer kwa ajili ya kukuza uchumi wa nchi hii. Tatizo lilianza baada ya kuua viwanda na kutegemea imports ya hata toothpick, tollet paper; leo hii baadhi wanaona bodaboda kama mkombozi wakati kiafya inafahamika huwezi kuendesha boda kwa zaidi ya miaka 15 na ukawa mzima kifuani kwa aina ya mavazi wanayovaa vijana wetu.

Kishimba akauliza bungeni, kati ya vijana elfu 40 waliohudhuria usaili wa nafasi 50-70 TRA; kama wangegoma kutoka uwanjani na kukomaa na maafisa waliopo wakilazimisha kuajiriwa, kuna udhibiti gani ungetumika kutuliza hali; wengi pengine hatujui.

Katika historia ya Misri baada ya Yusuf myahudi aliewahi kuwa mkuu wa nchi kufa, akaja Farao (mtawala) ambae hakutaka kuendeleza privilege walizopewa wahayudi na ndugu yao aliekuwa sehemu ya utawala wa Misri. Utawala wa Misri kuogopa wingi wa Wayahudi waliozidi kuzaliana, wakapitisha azimio la kuwafanya watumwa. Lengo lilikuwa kuwa-keep busy na wazalisha kwa maslahi ya uchumi wa Misri. Idadi ilipozidi kuongezeka wakaja na mkakati wa kuwaua watoto wa kiume wa kiyahudi.

Leo idadi ya vijana wenye elimu ya kidato cha nne mpaka shahada ya chuo kikuu ni wengi kuliko walio kazini. Je, kama nchi kuna mkakati wa nini kifanyike walau wawe "enslaved" kama ilivyokuwa Misri ili wazalishe?
Kwa mtazamo wangu, jinsi hawa freshers wanavyozidi kuwa wengi kitaa na kuishia kwenye betting centres na kuwa busy na smartphones, sioni kama ni afya kwa usalama wa uchumi wetu na usalama wa kizazi kinachofatia baada ya hiki cha sasa, kisiasa na kijamii.

Makazini watu wanakuwa organized namna ya kufanya kazi, kuna watu kuwajibishana, kuna watu kutoka katika clerical level mpaka kufikia seniority fulani na kuongeza thamani kwenye jamii kwa mfumo wa kulea jamii ya kazini na kutoa mchango kwenye familia. Hivi kwa trend ilivyo, kama nchi, je tunawafikiria hawa vijana au tunachukulia poa tu? Natamani kitu kifanyike ile tuwe na organized system ya kuwafanya vijana wazalishe na kuwa na pattern ya kuwakuza kiakili na kimalezi.

Naomba kukiri wazi kuwa mfumo wa vikundi vya vijana kuchukua fedha za halmshauri 5% kama mikopo isiyo na riba ni mfumo wenye model mbaya na ndiyo maana hatuoni mfumo wa biashara na shughuli zao za kiuchumi wanazofanya ukitoa matunda. Mfumo kama huo huo wa vikundi, sijui nani aliuanzisha Tanzania unatumiwa na baadhi ya mabenki kama Posta, baadhi ya micro-finance na hata Benki ya kilimo nao wame-adopt model hiyo; suala la kujiuliza tumezalisha waajiri wangapi ambao kupitia vikundi hivi ambao wana staff ya walau wafanyakazi 5-15 ambao wako kwenye mifumo rasmi ya mishahara, pesheni na bima ya afya?

Naomba nikiri kumuunga mkoni JPM kwa asilimia 100. Ila ninashauri in the course of building macro-projects, pia tujenga small and medium projects ambazo ziko kwenye organized system kwa kuanzia na mahitaji ya bidhaa ambazo tuna-import ambazo raw materials zake ziko ndani na kama tuta-agiza basi finished products zifanyikie hapa ili mzunguko wa fedha ubaki ndani.

Kuna siku nilitoa mfano hapa, kuwa Bakhresa ana-import maziwa ya unga na ku-reconstitute ili apate lita laki moja kwa maziwa anayopack. Ukichanganya na maziwa anayongenezea ice cream huenda akiwa anatumia kila siku zaidi ya lita laki 1.5.
Ili kupata lita laki 1.5 tunahitaji walau ng'ombe 6,000 ambapo kila ng'ombe anatoa wastani lita 25 kwa siku; kwa kufanya hivi kama kila farm itakuwa na ng'ombe 600 maana yake ni farm 10; tutoa ajira ngapi za vijana, tutatoa huduma ya madaktari wa mifugo wangapi; tutatoa huduma ya viwanda vya kuuza madawa ya wanyama wangapi; tutatoa vyanzo vingapi vya agro-dealers?

Samaki, kila mwaka huwa tuna-import tani laki 4; walaji wapo. Mpaka zitoke China na Vietnam kweli na forex hizoo zaenda kununua samaki.

Sasa wazee wetu wa uchumi pale BOT, hazina hivi hatuwezi kufikiria namna gani ya kufanya ili tu-cut down imports. Au nyie kazi yenu ni ku-analyse na kutoa reports basi?

Ushauri wangu, it always begins with leadership. Wazungu sio wakweli kwa kutuambia wajengeeni wananchi miundombinu halafu wao watajiletea maendeleo wao weyewe. Sio wakweli hata kidogo.
Wazungu kwa kujua umuhimu wa kilimo na ufugaji kama chanzo cha raw materials za viwanda vyao wanatoa ruzuku kwa wakulima na wafugaji ili viwanda viendelee kuwa operational na ajira za viwandani ziendelee at expense ya kuwa na uhakika wa soko la ndani na kuuza excess nje ya nchi zao. Fikiria nchi kama Netherlands ni ndogo kwa size ya mkoa mmoja Tanzania. Leo hii wanauza milk products mpaka kwetu.

It begins with leadership to organize its subjects to make things happen.

Ilimhitaji Yesu kutoka mbinguni kuja kuwaokoa wanadamu kutoka dhambini. Kwanini wanadamu hawakujiokoa? It begins with leadership
Ilimhitaji Musa akomae na Farao ili kuwatoa Israel Misri, kwanini Waisrael hawakuamua kutoka Misri mmoja mmoja? It begins with leadership
Ilimhitaji Julius Nyerere kuwaondoa wakoloni Tanzania na baaada kuongoza mampambano Kusini wa Afrika; kwanini hakuacha wakomae wao wenyewe... it begins with leadership

JPM anakuwa kama mlaumiwa kwa msingi ambayo ilikiukwa tokea awamu ya pili kuanza. Hata hivyo, JKN nae alihujumiwa sana kwenye model yake ya ujamaa.
Ujamaa (Usoshalist) uliopo Israel, Slovenia, Sweden mbona kule haujafeli? Mwl alikosa watu wenye akili ya kuelewa namna bora ya kukuza ujamaa ambao ungezaa ubepari baadae bila kuua ujamaa pia.

Honestly, tunahitaji organized pattern ya ku-harness nguvu za vijana wetu na akili zao at our advantage. Otherwise wakiwa kwenye nafasi ya they have nothing to loose, 20 years later kundi hili likiwa kubwa sana, yasije yakatokea ya Tunisia, Aljeria, Sudan na Misri.

Kuna Watanzania wenye kuwa sehemu ya suluhisho tupo. Vitu vingine vinahitaji kufikiri kwa pamoja na kuamua kwa pamoja ili kutengeneza mkondo wa maji ili mafuriko ya vijana wanaokuja wa-fall in kwenye huo mkodo wa kuwa kwenye organized economic pattern ya kukuza uchumi wao ambao eventually watachangia uchumi mkubwa wa Tanzania.

Marshall Plan ilikuwa inclusive kwenye sector zote za uchumi wa Ulaya magharibi kwa kuogopa threat ya ulaya kuchukuliwa na Ukomunist wa USSR. Kuchelewa kufanya maamuzi ya haraka yalipelekea Czechoslovakia kuotwaliwa na mabeberu.
Njaa huwa sio rafiki na migomo ya njaa hata kwa wanafunzi ilikuwaga anasababisha uharibifu mkubwa sana. Tusifikie kuwa na wananchi wenye njaa wengi wakajaribiwa kuuza haki ya uzaliwa wa kwanza kama Esau. Esau angekuwa kashiba it could a different story.
Hata Yesu mjaribu alimfuata akiwa na njaa. Ukiona vijana wa Nyerere ambao aliwaamini na kuwasomesha huku na kule na wakafanyiwa vetting wakajaribiwa kwa vipande vya fedha, hali sio njema mjaribu akiwafikia vijana ambao Nyerere wakati tunamzika '99 wao walikuwa wananyonya na baadhi yao walikuwa hawajaanza kuvuta pumzi ya dunia hii.

Shalom.
Wishing you a happy furahiday
 
Unamuunga mkono JPM kwa asilimia 100 Ila.............
Israel wakati timu ya makomandoo wanatoka kwenda Entebbe 1976 kuwaokoa mateka hawakuwa wanakubaliana wote in the mode of operation on how the extraction can be done. Ila walijadiliana huku team chini ya Yoni Netanyahu ikiwa njiani kwenda Uganda.

Kumuunga mkono 100% ndiyo ila kwa kuwa Mungu kanipa fikra na kama mwanafamilia ya Tanzania, ninao wajibu wa kushauri maadam kinachofanyika kinalenga kuwakabili maadui zetu.
 
Israel wakati timu ya makomandoo wanatoka kwenda Entebbe 1976 kuwaokoa mateka hawakuwa wanakubaliana wote in the mode of operation on how the extraction can be done. Ila walijadiliana huku team chini ya Yoni Netanyahu ikiwa njiani kwenda Uganda.

Kumuunga mkono 100% ndiyo ila kwa kuwa Mungu kanipa fikra na kama mwanafamilia ya Tanzania, ninao wajibu wa kushauri maadam kinachofanyika kinalenga kuwakabili maadui zetu.
Yaani kwa madudu anayofanya jpm halafu unadai kuunga mkono ww ni Buku saba Lumumba uko kazn na akili yako umeiweka likizo,unamuungaje mkono mtu kama yule?Tofauti yako na wale uko na inferiority unazunguka sana mbuyu,ila huwez unga mkono ujinga tukakuelewa,we ni Adui wa taifa kwa kuunga mkono mtu na sio utaifa.uzalendo si kuunga mkono raisi,hayo kachukue buku saba kajambe ulale
 
Sasa kama unaona ajira ni bomu unaungaje mkono mtu ambaye kipaumbile chake sio ajira ni kununua ndege zisizo na tija tena bila hata ukaguzi,yaan hawa wazalendo uchwara wa awamu hii wanataka kutuona sisi hatuna akili
 
Elimu,mitaji na mazingira wezeshaji (EMM)
hichi ndicho baazi ya nchi ukisikia hata ajira zina tatulika asilimia fulani,basi mfumo huu ndio unatumika.
 
Sasa kama unaona ajira ni bomu unaungaje mkono mtu ambaye kipaumbile chake sio ajira ni kununua ndege zisizo na tija tena bila hata ukaguzi,yaan hawa wazalendo uchwara wa awamu hii wanataka kutuona sisi hatuna akili
Tatizo la ajira lilianza kuwa na changamoto miaka ya '90 baada ya viwanda vingi kuwa vimekufa na mageuzi ya kiuchumi yalifuatia kuanza kupunguza wafanyakazi na Watanzania kuingia kwenye mfumo wa cost sharing kwenye huduma za afya, maji na elimu. Kabla ya hapo serikali ilikuwa inafanya kila kitu.

Kumlaumu mtu aliekaa madarakani miaka 3 kana kwamba yeye ndiyo kasababisha yote hayo ni upungufu wa kifikra. Njia ya mtu mwenye akili ni kujadiliana na mwenye madaraka kwa hoja njia na mikakati mbadala ya how to balance the two; kujenga uchumi mkubwa wa mindombinu kama anavyofanya sasa na kujenga uchumi mdogo na wa kati kwa kutumia local raw materials kuwa processed na kutoa final product kwa soko la ndani na baadae soko la nje. Kwa namna hiyo tunaweza kutengeneza ajira za viwanda vya ndani na fedha za mauzo ya bidhaa kuzunguka ndani kwa kuhifadhiwa kwenye mabenki na kuwekeza kwenye sekta zingine zenye uhitaji wa bidhaa na huduma.
 
Hii nchi ishajifia mda tu. Nawashauri mlio na kazi huko serikalini ibeni mpaka muwe matajiri. Umasikini sio mzuri aisee

Wizi kwa walio serikalini sio suluhisho na sio tija. Kuna watu walikusudia kutoa zaidi ya milioni 200 at expense ya kumchora twiga na rangi kwenye ndege.

Kumbe hela zipo, suala hapa kwanini tusifikiri kwa pamoja, baada ya kuokoa hizo fedha, kwanini tusikupe wewe au tumpe fulani mkopo wa machinery ambayo inaweza kuchakata pamba walau kuzalisha nyuza za kushona sare za JWTZ, Uhamiaji, Polisi, Magereza, Zimamoto na Uokoaji na JKT.

Vitambaa vinavyobaki vinashona sare za wanafunzi wa shule zetu.

Tukianzia hapo kwa ku-cut down imports hiyo ndiyo akili.

Kukata tamaa na kulalamika will never make a better life.
 
Haya tuanzie hapa,twende taratibu yeye ndani ya hiyo miaka 3 kafanya kipi cha maana kuhusu ajira?

Hivi kuwekeza kwenye ndege au kilimo kipi kinamgusa mtanzania?kilimo ni almost 70% unaitelekeza unanua ndege ambazo zinazalisha hasara?

Hata kama ni miaka mitatu maamuz anayofanya kwa sasa hahitaji kubeba lawama?

Just simple hata mtt wa darasa la kwanza anaelewa this simple come concept
 
Haya tuanzie hapa,twende taratibu yeye ndani ya hiyo miaka 3 kafanya kipi cha maana kuhusu ajira?
Hivi kuwekeza kwenye ndege au kilimo kipi kinamgusa mtanzania?kilimo ni almost 70% unaitelekeza unanua ndege ambazo zinazalisha hasara?hata kama ni miaka mitatu maamuz anayofanya kwa sasa hahitaji kubeba lawama?just simple hata mtt wa darasa la kwanza anaelewa this simple come concept
Kilimo angewekezaje kwa mfano?
U might have a point there
 
Sasa kama unaona ajira ni bomu unaungaje mkono mtu ambaye kipaumbile chake sio ajira ni kununua ndege zisizo na tija tena bila hata ukaguzi,yaan hawa wazalendo uchwara wa awamu hii wanataka kutuona sisi hatuna akili
Kuna ajira za muda mfupi zinatengenezwa in the course ya ujenzi wa SGR na miradi mingine, baada ya miradi kuisha ajira hizo zinakoma.

Mimi nina advocate kwa ajira endelevu zenye kuwawezesha watu kuingia kwenye sekta rasmi ya kupata mishahara ambayo inakuwa taxable, kuingia kwenye mifuko ya pensheni na bima ya afya.

Kuna namna ambavyo wakubwa wanaona kwa mtazamo toafuti na mimi na wewe twaona kwa mtazamo tofauti. Kazi yetu ni kujadiliana kwa hoja na wakubwa ili sote tuone ambacho kila mmoja wetu anaona ili kwa pamoja tushirikiane kudhibiti kukua kundi la vijana wasio na ajira.

Jifikirishe kwa kuangalia picha hii
1099937
 
Wizi kwa walio serikalini sio suluhisho na sio tija. Kuna watu walikusudia kutoa zaidi ya milioni 200 at expense ya kumchora twiga na rangi kwenye ndege.
Kumbe hela zipo, suala hapa kwanini tusifikiri kwa pamoja, baada ya kuokoa hizo fedha, kwanini tusikupe wewe au tumpe fulani mkopo wa machinery ambayo inaweza kuchakata pamba walau kuzalisha nyuza za kushona sare za JWTZ, Uhamiaji, Polisi, Magereza, Zimamoto na Uokoaji na JKT.
Vitambaa vinavyobaki vinashona sare za wanafunzi wa shule zetu.
Tukianzia hapo kwa ku-cut down imports hiyo ndiyo akili.
Kukata tamaa na kulalamika will never make a better life.
Boss unamawazo mazuri sana tatizo boss wako kipaumbele chake sio ajira.
Yeye anataka akiondoka awaachie madaraja, ndege, na vitu vinavyoonekana.

Hujiulizi alitimua watu kibao kwenye ajira ila haajiri?? Hapandishi madaraja ya ajira nk. Tatizo boss wenu hashauriki ana centralize uchumi mpaka makampuni binafsi wanakosa pesa ya kuajiri.
Kodi zimekuwa kubwa makampuni yana retreanch wafanyakazi..ukitaka kujiajiri ufanye ata biashara kodi kila kona.hapandishi madaraja wala mishahara nk. Yaani serikali haiajiri na bado inaitengenexea ugumu sekta binafsi nayo isiajiri sasa madogo wa chuo waende wapi?? . Boss wenu anaona wivu sana watu wakipata ajira au kufanya biashara kupsta pesa anafurahi sana watu wakiwa masikini.
Hao wanyonge anaowatetea ndio wanaumia kwa maamuzi yake yasio na tija. Yeye anadhan anawakomoa wenye pesa kumbe mwisho wa siku hao mssikini anaowatetea ndio wanazid kudidimia.
Wewe unachosema na yeye anachofanya ni vitu viwilli opposite.
Anachofanya yy ni kuhakikisha vijana hawapati kaz na hawawez kujiajiri
 
Kilimo angewekezaje kwa mfano?
U might have a point there
Kuna mfano nishatoa hapo juu sijui kama ulisoma vya kutosha.
Ila nikujuze we need various models ili kukuza uchumi wa kupitia kilimo. Pitia hii model hapa chini

......
Tanzania uzalishaji wa shambani huna mfumo rasmi wa kuratibu nini kinatakiwa kutumika viwandani. Ndiyo maana hawa matajiri baadhi ya bidhaa za kilimo wanazouza kama mafuta, maziwa, biscuits wana-import na kufanya kufungashia upya hapa. Kuna Chocolates za Mo anauza kafungashia India, kwa namna hii, kwenye mfumo wa kiuchumi tafsiri rahisi, fedha nyingi zaenda India kulipia malighafi, umeme, wafanyakazi, TBS ya huko, TFDA ya huko, logistics...just to mention a few.

Maziwa ya Bakhresa ananunua toka India na kuyachanganya na maji (reconstitute) then ana-pack. Kwa siku Bakhresa ana-pack Lita laki 100 za maziwa ya pack, ukichanganya na maziwa na ice cream, kuna kiwango kikubwa cha fedha za maziwa ambazo kama angenunua kwa wakulima wa Tanzania, mzunguko huo wa fedha ungewafaidisha akina Masanja, Masawe, Mwanjala, Ogola na Kokusoma.

Kwa uhitaji tu wa maziwa kwa kiwanda cha Bakhresa kuna ajira za Watanzania zinapotea, kuna consultancy ya madaktari wa mifugo zinapotea, kuna viwanda vya madawa ya wanyama zinapotea; kuna agro-vets ambazo zingeuza madawa ya wanyama zinapotea.
Ndiyo maana ukipiga picha ya hasara Tanzania inayopata kwa imports inatuathiri si kidogo. Wachumi wa BOT, hazina na Wizara ya Kilimo hili ni moja ya eneo ilitakiwa watengeneze mkakati wa kisera ku-facilitate mikopo ya uazalisha wa raw materials kama hizo kama moja ya mkakati wa ku-cut down imports za kile ambacho tunaweza kuzalisha na then kinalika hapahapa.

Inawezekana hata ndugu yetu Mayalla akapata kazi ya kutengeneza documentary za mnyororo wa thamani ya toka maziwa yanazalishwa ndani mpaka Bakhresa anachakata na yanaingia sokoni.
 
Tulitakiwa tuwe definition yetu ya unemployment. Hii ingesaidia sana badala ya kuasili kutoka kwa mabeberu wakati sisi ni vimbuzi jike
 
Boss unamawazo mazuri sana tatizo boss wako kipaumbele chake sio ajira.
Yeye anataka akiondoka awaachie madaraja, ndege, na vitu vinavyoonekana.

Hujiulizi alitimua watu kibao kwenye ajira ila haajiri?? Hapandishi madaraja ya ajira nk. Tatizo boss wenu hashauriki ana centralize uchumi mpaka makampuni binafsi wanakosa pesa ya kuajiri.
Kodi zimekuwa kubwa makampuni yana retreanch wafanyakazi..ukitaka kujiajiri ufanye ata biashara kodi kila kona.hapandishi madaraja wala mishahara nk. Yaani serikali haiajiri na bado inaitengenexea ugumu sekta binafsi nayo isiajiri sasa madogo wa chuo waende wapi?? . Boss wenu anaona wivu sana watu wakipata ajira au kufanya biashara kupsta pesa anafurahi sana watu wakiwa masikini.
Hao wanyonge anaowatetea ndio wanaumia kwa maamuzi yake yasio na tija. Yeye anadhan anawakomoa wenye pesa kumbe mwisho wa siku hao mssikini anaowatetea ndio wanazid kudidimia.
Wewe unachosema na yeye anachofanya ni vitu viwilli opposite.
Anachofanya yy ni kuhakikisha vijana hawapati kaz na hawawez kujiajiri
Boss wangu, keeping quite will never make things better.
But thinking loudly by giving relevant way how we can get out of here na kwa Mkulu kuendelea kuwa na tax base kubwa atatuelewa.
Tatizo ni either watu wanamwogopa sana na mpaka wanashindwa hata kumpelekea proposal za maana.
Kuna Mtanzania ana-proposal ya kuzalisha vifaa tiba ambavyo by 97% tuna-import.
Alimwagiza waziri wa fedha apokee business plans za viwanda vya kuzalisha madawa na vifaa tiba.

Ila kama huyu ninaemfahamu, say angepata walau gov. guarantee kukopa TIB au NHIF kununuliwa machinery na raw materials. Soko lipo maana mnunuzi ni MSD na other private sectors. Hapa tunatengeneza ajira, tuna-cut down imports na uwekezaji kulipa deni.
Say NHIF anaweza kuwa shareholder in the course of running business na kupokea dividend. Then deni liki
Mambo mengine sio rocket sayansi, na maamuzi ya kufikiri kwa pamoja.
It begins with right attitude, leadership and art of being persuasive with facts
 
Back
Top Bottom