Ndugu zangu wanaukawa, mimi ni kijana msomi wa viwango vya juu na kura yangu mnayo dhahiri.
Lakini si kwa sababu nimewasikia sana kwenye taarifa za habari kwa kuwa hampati nafasi. Sijui kama umuhimu wa habari zenu unapewa kipaumbele na vyombo vingi vya habari.
Pia sio kwa sababu nimeona matangazo yenu kando ya barabara au mitaa mbalimbali kwa kuwa zipo chache sana. Nadhani tunatakiwa kujitangaza zaidi ya mshindani wetu. Haswa ktk maeneo yenye mikusanyiko mikubwa ya watu na njia ya televisheni.
Zaidi, si kwa sababu nimeona habari zenu maalum ktk mitandao ya kijamii. Hapa mmelega siku za karibuni tofauti na mlipoanza kampeni. Sijajua kama ni mkakata ili tusizoee kuwasikia ili kutuwekea hamu mwishoni kuelekea siku ya uchaguzi (creating scarcity of information readying for surprise show up).
Nitawapa kura kwa kuwa napenda mabadiliko ili kuondoa ccm madarakani. Hilo moja langu binafsi lumewapa kura yangu tayari. Tupo wengi kiasi.
Ila msipojinadi na kuleta upinzani kwa ccm mtajikuta mnashindwa uchaguzi kwa kukosa kujulikana na pia kushindwa kushawishi wengi ambao ni mtu kati ( undecided). Usomi na uelewa wangu wa umuhimu wa mabadiliko umenifanya thabiti na sitatetereka kamwe hadi kieleweke. Wenzetu ambao hawana maamuzi yao bali uamuzi wa kushawishiwa kwa ngoma, muziki, taarabu na ngonjera bila kusahau pushapu watapigia ccm kura.
Nashauri mtoke mtuhabarishe kwa wingi ili tuwapigie kura zaidi mpate ushindi wa kishindo hapo 25.10.2015. Tunahitaji updates za mikutano popote Lowassa alipo au mbunge au vipindi maalum kupitia tv.
Mbowe pia aache kuelezea jinsi ccm wanavyojipanga kuvuruga uchaguzi kwa kuwa inawakatisha tamaa wale ambao hawajaamua 100%. kuwapa kura ingawa hawaipendi ccm. Mambo hayo myajadili ndani kwa ndani mkizungumza na tume. Mnatakiwa mtupe moyo wa kusonga mbele daima hadi mwisho huku mkituhakikishia kuwa hakuna kuibiwa kura. Na ninyi viongozi mkipambana na mbinu chafu kimya kimya kwa kutumia mifumo yenu ya ndani ya chama.
Tunaomba mikutano irushwe live kwenye miji mikubwa ili tuone kama ccm wafanyavyo. Sitofurahi nikisikia ccm wakipata ushindi wowote mwaka huu ukiwemo urais!!
Chonde chonde msitupooze bali mtutie joto hadi siku ya uchaguzi.
Hizi tafiti feki za Twaweza na wengineo fafanueni kwa kuwa wengi wanakatishwa tamaa ya kupiga kura na ukiona ccm wanaendeleza mbinu hii ujue inawaletea faida. Pia mtolee maelezo ya kutosha suala la mdahalo msionekane mnakwepa jambo fulani.
Nimewaasa kwa kuwa kura za uhakika zinamomonyolewa na mbinu chafu za ccm. Huo ndio ukweli. Kurugenzi ya habari UKAWA amkeni unga robo saa mbaya wakuu.
Nawasilisha wakuu.