Lowassa aiweka nchi rehani

Lowassa aiweka nchi rehani

TataMadiba

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2014
Posts
9,868
Reaction score
5,753
Zikiwa zimebaki siku 30 kabla ya uchaguzi mkuu wa rais, wabunge na Madiwni unaotarajiwa kufanyika oktoba 25 mwaka huu, Mgombea anayegombea kupitia umoja wa Katiba ya Wananchi, Edward Lowassa anadaiwa kuanza kutoa vitisho kwa baadhi ya wafanyabiashara ambao wamekuwa wakigoma kushiriki kuchangia fedha kwa ajili ya kuwezesha kampeni zake kwa kuwambia kuwa akichaguliwa kuwa rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania atawashugulikia.
Aidha amekuwa akiwaahidi wafanyabishara wanaomchangia ili kuweza kufanikisha kmpeni zake kuwapa rasilimali ya nchi ikiwamo vitalu vya gesi na Bandari.
Madai ya Lowassa kuwatisha wafanyabiashara wanaogoma kuchangia kampeni z UKAWA yanathibitishwa na Kauli ya Mwenyekiti wa CHADEMA wakati wa harambee iliyofanyika juzi katika Ukumbi wa Mlimani city kuwa kuna wafanyabiashara wanagoma kuchangia kwa kuhofia kushughuliwa na vyombo vya dola. Hata hivyo taarifa za ndani zinadai, sababu aliyoitoa Mbowe siyo ya kweli ila ukweli ni kwamba wafanyabiashara hao wamejiridhisha kuwa LOWASSA hawezi kushinda na kuchangia kampeni hizo ni sawa na kuchezea bahati nasibu.
chanzo: SAUTI HURU.
20150925_192930.jpg
 
kipaumbele elimu, cha pili elimu cha tatu elimu , mchague Lowassa
 
Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, MamaSamia Suluhu Hassan akimsalimia Katibu wa CCM mkoa wa MorgoroRojas Rumuli wakati wa mapokezi yake, alipowasili mkoani Morogoro kufanya mikutano ya kameni katika mkoa huo leo
Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akimsalimia mgombea Ubunge Jimbo la Gairo, Sadik Murad wakati alipowasili mkoani Morogoro, kufanya mikutano ya kampeni mkoani humo.
Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akiwapungua mkono wananchi waliofika kumlaki alipowasili mkoani Morogoro leo. Kulia ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dodoma, Adam Kimbisa na wapili ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Morogoro, Inocen Karogeresi
Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM Mama Samia Suluhu Hassan akiwasili kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Gairo A, kuhutubia mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika jimbo la Gairo mkoani Morogoro.
Baadhi ya wananchi wakiwa na mabango kwenye mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika jimbo la Gairo leo.
Katibu wa CCM, mkoa wa Morogoro, Rojas Romuli akihutubia wananchi katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika viwanja vya shule ya msingi Gairo A katika jimbo la Gairo mkoani Morogoro
Mgombea Ubunge jimbo la Gairo Sadik Murad akihutubia wananchi atika mkutano wa kampeni wa Mama Samia uliofanyika leo katika jimbo hio mkoani Morogoro
Umati wa wananchi ukiwa umefurika kwenye Viwanja vya Shule ya Msingi Gairo A, wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika katika jimbo la Gairo mkoani Morogpro
Mwananchi akionyesha bango la kumfagilia Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM, Dk. John Magufuli wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika jimbo la Gairo mkoani Morogoro
 
jamani jamani,lowasa anapigwa kotekote asee,huku samia,huku magufuli,kule mwigulu,,,,,dah....!!
 
Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, MamaSamia Suluhu Hassan akimsalimia Katibu wa CCM mkoa wa MorgoroRojas Rumuli wakati wa mapokezi yake, alipowasili mkoani Morogoro kufanya mikutano ya kameni katika mkoa huo leo
Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akimsalimia mgombea Ubunge Jimbo la Gairo, Sadik Murad wakati alipowasili mkoani Morogoro, kufanya mikutano ya kampeni mkoani humo.
Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akiwapungua mkono wananchi waliofika kumlaki alipowasili mkoani Morogoro leo. Kulia ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dodoma, Adam Kimbisa na wapili ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Morogoro, Inocen Karogeresi
Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM Mama Samia Suluhu Hassan akiwasili kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Gairo A, kuhutubia mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika jimbo la Gairo mkoani Morogoro.
Baadhi ya wananchi wakiwa na mabango kwenye mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika jimbo la Gairo leo.
Katibu wa CCM, mkoa wa Morogoro, Rojas Romuli akihutubia wananchi katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika viwanja vya shule ya msingi Gairo A katika jimbo la Gairo mkoani Morogoro
Mgombea Ubunge jimbo la Gairo Sadik Murad akihutubia wananchi atika mkutano wa kampeni wa Mama Samia uliofanyika leo katika jimbo hio mkoani Morogoro
Umati wa wananchi ukiwa umefurika kwenye Viwanja vya Shule ya Msingi Gairo A, wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika katika jimbo la Gairo mkoani Morogpro
Mwananchi akionyesha bango la kumfagilia Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM, Dk. John Magufuli wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika jimbo la Gairo mkoani Morogoro
kwa nini mkuu magu asingemgawia wasanii wengine jamaa mbinasi sana. anashindwa kumpa mgombea mwenza hata bongo muvi wawili. huu mkutano unahadhi ya udiwani.
 
Hiki kizazi ni cha maangamizi. Kuna bango moja limeandikwa ''IKURU.....'' yaani alitaka kuandika IKULU....
 
Eti mbunge wa Gairo anaitwa Sadick Murad. Mafisisiem bwana hata hayajitambui wabunge wao
 
Back
Top Bottom