Lowassa afunika Iringa

Lowassa afunika Iringa

@ Ben Saanane, Hakulazimishwa kujiuzulu. Taarifa ilitamka 'ajiangalie halafu achukue uamuzi'. Hakuna sehemu yoyote aliyolazimishwa kujiuzulu. Tatizo mlisha tembea sana na hoja ya ufisadi, sasa ni monotonous kuzidi kuishadidia. Hapo Lowasa ndipo anaawacha kuelekea touch line. 2015 mtarudi tena na hoja ya ufisadi, imeshawachosha watu masikioni.

Watu gani waliochoshwa? Au wewe ndiyo mmoja wao?
 
Anaandaliwa na CDM kuchukua nafasi ya SLAA, wanaona anafiti kutokana na kuwa mkristo kuliko kumpa ZITTO nafasi hiyo.

Halafu mkiambiwa nyie ndio waanzishi wa udini Tanzania mnakataa. Kama hayo anayoyafanya Zitto ni maelekezo ya dini yake basi nadhani mtakua mnautukana Uislam bila kujua, mimi namcha Mungu, ninavyo fahamu hakuna dhambi mbaya anayo ichukia Mungu kama Dhambi ya Unafiki. Please usiutukanishe huo uislamu kwa kumlinganisha Zitto na dini yake wala watu wa Kigoma na tabia yake.
 
thatha wewe uko upande gani hapa kwasababu huko CCM mmepasukapasuka, huyu Fisadi Gamba anayepita makanisani kuomba apigiwe debe na wachungaji ni chama lako au
 
Waziri Mkuu mstaafu na mbunge wa Monduli amedhihirisha nguvu kubwa na utajiri wa watu aliyonao, baada ya kupata mapokezi makubwa Mkoani Iringa.Lowassa amewasili Iringa asubuhi hii akiongozana na wabunge karibu wote wa mkoa wa Iringa,kwa ajali ya Harambee ya ujenzi wa kanisa na Kituo Cha radio Cha overcomers.viongozi wote wa Chama tawala Mkoani Iringa na Serikali nzima imempokea Mh Lowassa.



Kwanza kabisa, rekebisho ... sio mstaafu! ni aliyeachishwa kazi.

Pili, angalia bluu, huo utajiri wa watu ndio hao viongozi wa maccm na serikali nzima ya maccm mkoani!
Kwa hiyo hapo jipya liko wapi??
 
Hayo Mapokezi atakuwa amejiandalia yeye Mwenyewe, ni sawa na wewe un akuwa na Part home, Unaandaa kila kitu mwenyewe na baadae sasa unaoga unavaa freshi na unakaa kusubiria uhudumiwe msosi na vinywaji ulivyo andaa mwenyewe
hiyo ndiyo kweli, huyu EL siku zote huwa anaandaa mapokezi yake mwenyewe, anakazana sana ili 2015 wae mgombea kwa tiketi ya CCM. na kwa sababu sheria ya uchaguzi inaweza isiwe tayari, atapita kwa kuchakachua. Mungu aepushie mbali.
 
akhsante sana mkuu,hapo upo sawa sawia,tatizo letu sisi tunavyoangalia mtu ni tofauti na Mungu anavyoangalia.mtu akiwa ametenda kosa juzi,jana na leo ametenda mazuri,je ni haki kumhukumu kwa kosa la juzi ambalo inawezekana kabisa alishatubu?tuache kuhukumu tusije tukahukumiwa
 
jamaa ni mpambanaji sana, na cha kufurahisha hana hata aibu, kwa tuhuma zinazomuandama nadhani hilo neno muadilifu angeomba wasilitumie,najaribu kufikiria ingekuwa kigogo mmoja wa cdm ndio anashinda makanisani kuendesha harambee cjui ccm wangesema nini,cdm chama cha kidini au huyo kigogo ndio mdini?
Kuna msemo unasema atafutae hachoki so tusibeze hizi pilika za lowasa zinaweza kuwa na mshindo mzuri badae tukabaki tukisema jamaa fisadi na wakati huo yupo ikulu.
 
Hehehe niseme ukweli Lowasa namwogopa. Nguvu anayotumia kuupata huu uraisi ni beyond normal. Haiwezekani ikawa tu eti ni kutuletea maendeleo sie waTZ kwa roho gani nzuri aliyonayo huyu jamaa.
Yani he wants that seat by hook and crook!
 
Ben acha noma, huyu MASTER ni mtendaji, akipata nchi kwa kazi atayopiga Watanzania miioyo itasuuzika.

Nami natafuta fursa kubwa ya kumzuia yeye na chama chake kuingia ikulu mwaka 2015.Vijana ndio tutakaoamua.Utendaji kazi bila uadilifu ni UHUNI.
 
akhsante sana mkuu,hapo upo sawa sawia,tatizo letu sisi tunavyoangalia mtu ni tofauti na Mungu anavyoangalia.mtu akiwa ametenda kosa juzi,jana na leo ametenda mazuri,je ni haki kumhukumu kwa kosa la juzi ambalo inawezekana kabisa alishatubu?tuache kuhukumu tusije tukahukumiwa
Hakika, Mambo ya toba ni mambo ya kiroho, mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke hawezi kuyaingilia. Watanzania hawatampigia mtu yeyote, kura kwa kuamini bali kwa kuona matendo yake ya ukweli na daima ukweli huwa unajitenga na uongo hatimaye!
 
Anaandaliwa na CDM kuchukua nafasi ya SLAA, wanaona anafiti kutokana na kuwa mkristo kuliko kumpa ZITTO nafasi hiyo.

Walewaleee...ukiamka huwa unawaza udini tu..!! kwa hiyo hata waliooa waislam watoe talaka kwa wake zao kwa kuwa ni wa islam, acha chuki best.
 
nilisikia toka kwake kama sijasahau 2010 kuwa wingi wa watu kukufuata au kukusikiliza si kuwa wanakubaliana na wewe; sijui hii tafsiri inaendelea kuwa kweli hata hapa! hata hivyo watu wa iringa wana msimamo wao ambao hauwezi kuutabili kirahisi
 
huu ni uzi wa kwanza kushuhudia lowasa anapewa makavu... upepo umebadilika.......
 
Kuna kitu nashindwa kuelewa. Wabunge wapo iringa kuandamana nae. Na huku bunge linaendelea. Kwahyo wananchi wa baadhi ya majimbo ya iringa hawana wawakilishi kwa sasa bungeni. Ila wapo na huyo fisadi... Hayo yanayojadiliwa bungeni hayawahusu hao wananchi wa iringa? Naombeni tujadili hili.
 
bora askofu boaz nae apate fungu lake hapo!ila amekosea timing,coz cdm nao watakua huko,angesubiri wapite!bt nway lets wait n see!
...hyo harambee itakuwa lini?
 
Kuna kitu nashindwa kuelewa. Wabunge wapo iringa kuandamana nae. Na huku bunge linaendelea. Kwahyo wananchi wa baadhi ya majimbo ya iringa hawana wawakilishi kwa sasa bungeni. Ila wapo na huyo fisadi... Hayo yanayojadiliwa bungeni hayawahusu hao wananchi wa iringa? Naombeni tujadili hili.

Hili nalo neno!anzisha uzi wake!
 
Back
Top Bottom