Wakudadavuwa
JF-Expert Member
- Feb 17, 2016
- 17,505
- 16,005
Hili lazima tulizungumze, Edward Lowassa ni mjumbe wa kamati kuu tena asiye na hata mwaka mmoja katika wadhifa huo lakini katika mikutano ya CHADEMA inashangaza kwani;
- Huingia wa mwisho na kulakiwa na mwenyekiti, ndugu Mbowe na, Makamu wenyeviti bara na Zanzibar, Katibu Mkuu na Manaibu.
- Hupanga mambo ya kujadliliwa katika mikutano
- Ana kura ya veto, kura yake ni ya turufu ni kubwa kuliko wajumbe wa mkutano wowote wa CHADEMA.
- Anakaa Meza kuu wakati wajumbe wa 'level' yake wanakaa viti vya kawaida.
- Posho yake ya kikao ni kubwa kuliko ya Mwenyekiti.
- Je thamani ya wajumbe wakongwe CHADEMA kama Prof. Baregu, Mabere Marando ni ndogo kulinganisha na Lowassa?
- Tundu yuko wapi wakati katiba ya CHADEMA inavunjwa?