Lowassa aache uchonganishi, hakuna njaa nchini

Lowassa aache uchonganishi, hakuna njaa nchini

Na wale wa magu waliomwambia magu kuwa wananjaa akawajibu vile nao wachonganishi
 
Kuhusu makaburi nenda bwai. Kuhusu mimbari mbona wakatoliki wana ruhusu? Na kurudisha mali nyumba zilizogwiwa washikaji zimerudishwa? Siyo kwamba watu hawajui Ila wamenyamaza tu
 
Kitendo cha Mwanasiasa mkongwe kusimama mazabauni/jukwani na kuitangazia dunia kwamba chama chake (cha upinzani) kitagawa chakula kwa wenye njaa, ni kitendo sahihi kwa mujibu wa majukumu ya chama cha upinzani? Jadili kwa hoja na utulivu.
 
Sawa Mungu, umesikika hukumu ulizotoa. Kama Lowassa aliweza kufanya yote hayo peke yake bila ccm wengine kujua, bila Mawaziri wenzake na Rais wa wakati huo kujua basi natangaza kuanzia leo huyu jamaa ni 'Role Model wangu'.

Hiyo ni akili kubwa mno, ni U-genius uliopitiliza, na Mahakama ya mafisadi hajapelekwa! Na mashamba yake hayajaporwa! Hii ni kitu ya kuigwa.

Ni bora mwizi anayesaidia watu kwa matendo kuliko kama maandiko yasemavyo, kuliko 'mtakatifu' mchoyo na mwenye kulitaja bure jina la Mungu.
 
Kama taifa lingekua linajiweza kwa 120% mngegawa chakula kwa vile hakuna mnatafuta njia ya kukimbia majukumu tunajua nchi ipo chari... mmekula pesa za bukoba kwani mlitangaza kuwa tusaidie serikali iweke miundo mbinu yake bukoba sasa hili la njaa pia sidhan kama nilakukimbia nyie gawaeni icho kilichopo.... kama mmeshindwa achen jamaa atafute agawe sie tunaitaji kushiba tu sio kelele ata kama atakuja kukigawa lyatonga mrema sie tutakula tu.... pia kwa vile buku saba zina wasumbua ata akianza kugawa pia mtamsifia
 
Mleta mada hauna hoja kabisa.

EL ametumia madhabahu kusema kwamba wapo tayari (CDM) kusaidia maeneo yaliyo na uhaba wa chakula, kuna ubaya gani??

Mbona yeye kila akienda mahali kusali anapanda madhabauni na kuongea tena vitu vingine ambavyo havina maana kabisa??

Serikali imeamua kulikimbia tatizo la njaa kwa kulazimisha kwamba hakuna njaa.

Waacheni wenye moyo wa kusaidia watu wenye njaa wawasaidie.

Mburuluzzzz hamna hoja.. Fainali 2020.
 
Hali yenyewe tu inajionesha kwamba njaa ipo sasa wewe unayeponga njaa hakuna ni mapenzi yako tu ya kichama na unaamini kila kitu unachoambiwa na chama.
 
Waulize maaskofu na mashekhe nani kawambia kuna njaa. Na wamezungumzia mbele ya madhabau
 
Umetumwa kumsaidia mtani wa makabila? Kwa hiyo mashekh na mapadri na wenyewe ni wanasiasa au walutherani? Kweli aliyetuloga alifunga kila kitu
 
Nani mwenye mamlaka ya kutangaza hali yoyote ya hatari katika nchi? Mfano wa wazi kabisa ni pale tulivyovamiwa na Nduli Idd Amin Dadaa,Hayati Baba wa Taifa Mwl J.K.Nyerere akiwa amiri jeshi mkuu wa majeshi ya Tanzania aliutangazia umma tena ktk mkutano maalumu na vyombo vya habari juu ya uvamizi wa nchi yao kutoka kwa Idd Amin Dadaa.
Mfano wa pili na hata baada ya kutokea kifo cha baba yetu au baba wa Taifa Mwl J.K.Nyerere ni Rais wa wakati huo ndugu Benjamin William Mkapa akautangazia umma wa Watanzania kupitia vyombo vya habari juu ya msiba huo.
Nachotaka kusema kila nchi inautaratibu wake wa kutangaza majanga ya kitaifa naweza kusema labda majanga makuu yanayotokea au yanayotishia kutokea ktk nchi,kwahiyo Watanzania tuwe makini kwa hilo kwani wahenga walisema 'Miluzi mingi ilimpoteza Mbwa muelekeo' kwahiyo Watanzania kama kunatishio lolote la njaa Rais wetu ni mtu wa watu na nimpenda watu na Rais wetu yupo ndani ya jamii hii hii ya Watanzania, kama kunatishio lolote ktk nchi atautangazia umma juu ya tishio hilo kwa sababu yeye ndiye kiongozi mkuu wa Taifa hili teule.
Yaani kukupenda wewe kama kada mwenzetu isiwe kua anatupenda sote.Mambo mengine tuachane na siasa uongo..njaa hipo tu
 
Watanzania mwogopeni Mungu kwani Lowassa ndio kaomba chakula? Wananchi ndio wanalalamika acheni roho mbaya
 
Yaani kukupenda wewe kama kada mwenzetu isiwe kua anatupenda sote.Mambo mengine tuachane na siasa uongo..njaa hipo tu
Kwahiyo suruhisho la tatizo hili unalosema la njaa nini,kutoa chakula kwa wananchi tu si ndiyo,kama ni hivyo basi nchi hii kunakitu kinachoitwa ilimradi nishibe tu lakini ya kesho itajulikana hiyo hiyo kesho si ndiyo.
Kumbuka tumekuwa tunasumbuliwa na njaa kila mwaka kwa sababu ya nchi ya kukosa mipango ya muda mrefu,tulikuwa na viongozi wanaowaza tatizo litokee tu iliwao wa neemeke na hilo tatizo lakini sasa tunakiongozi anayejiuliza kwanini tunakosa watalii kwa sababu ya kutokuwepo vyombo vya usafiri vya kuwatoa huko waliko na kuwaleta hapa kwetu moja kwa moja,tunakiongozi anasema kwanini nchi inapata mapato kidogo yatokanayo na kodi kwa sababu watu wanakwepa kulipa kodi au kodi zinapatikana lakini zinaingia kwenye mifuko ya watu wachache na hatimae Rais wetu amejitahidi kutatua hilo tatizo.
Mkipata kiongozi wa nchi anayejiulizauliza juu ya mateso wanayopata wananchi wake,huyo ndiye kiongozi.
 
1. Unasikitika sana Lowassa kupewa madhabahu ilihali ni mdhambi sana: Hapa umekosea sana-kama unazungumzia dhambi ambazo Yesu alitufia msalabani ili zisafishike, huna uwezo wa kujua kama Lowassa ana dhambi au la, maana uhusiano baina yake na Mungu wake huujui hata chembe kwa kuwa hujui ni lini Lowassa aliomba msamaha wa dhambi alipojiona ana hatia mbele za Mungu. Kwa hiyo huna mamlaka yoyote ya kuzungumzia hali ya kiroho kuhusu Lowassa!

2. Unasema uongo kwamba Lowassa ametangaza janga la njaa na hivyo amekiuka sheria uliyoitaja hapo na anastahili kushughulikiwa. Lowassa, kama ambavyo viongozi wengine wakiwemo wa dini na wananchi wa kawaida, wanaamini kuwa kuna uhaba mkubwa wa chakula katika baadhi ya maeneo. Kwa hiyo hajavunja sheria yoyote kuitambua hali iliyopo, wala haiwezi kuwa criminal offence kusaidia watu waliona uhitaji wa chakula bila kujali kama kuna njaa au la.

3. Unadai hakuna mwananchi atakayepokea chakula kutoka kwa Lowassa kwa kuwa mikono yake imejaa damu! Kwanini unajipa kazi ya kuzungumzia watu ambao kwanza hawakufahamu, bali wanamfahamu na wana imani kubwa na "mwenye mikono iliyojaa damu"! Huoni kama unapoteza muda wako?

4. Unawataka Chadema waache kutumia unachokiita msamiati wa njaa kuwa ajenda ya kisiasa. Nadhani kuna umuhimu wa kushirikisha viungo vyako vyote kabla ya kukurupuka. Hivi akili yako inakuelekeza kuamini kuwa watanzania ni wajinga mno kiasi cha kusombwa na propaganda za njaa wakati hawana njaa?
 
Kwahiyo suruhisho la tatizo hili unalosema la njaa nini,kutoa chakula kwa wananchi tu si ndiyo,kama ni hivyo basi nchi hii kunakitu kinachoitwa ilimradi nishibe tu lakini ya kesho itajulikana hiyo hiyo kesho si ndiyo.
Kumbuka tumekuwa tunasumbuliwa na njaa kila mwaka kwa sababu ya nchi ya kukosa mipango ya muda mrefu,tulikuwa na viongozi wanaowaza tatizo litokee tu iliwao wa neemeke na hilo tatizo lakini sasa tunakiongozi anayejiuliza kwanini tunakosa watalii kwa sababu ya kutokuwepo vyombo vya usafiri vya kuwatoa huko waliko na kuwaleta hapa kwetu moja kwa moja,tunakiongozi anasema kwanini nchi inapata mapato kidogo yatokanayo na kodi kwa sababu watu wanakwepa kulipa kodi au kodi zinapatikana lakini zinaingia kwenye mifuko ya watu wachache na hatimae Rais wetu amejitahidi kutatua hilo tatizo.
Mkipata kiongozi wa nchi anayejiulizauliza juu ya mateso wanayopata wananchi wake,huyo ndiye kiongozi.
Kwahiyo ukipata tatizo unaanza kwanza kulitatua au unaanza kwanza kuangalia chanzo alafu ndio unalitibu....aaah mfano kuna kipindupindu hapo Chato na watu wanakula je utaanza kuwatibu na kuwaokoa au utaanza na kutafuta chanzo za huo ugomjwa. ..Nilisema tumsifie kada mwenzetu
 
HONGERA SANA BRO AUGUSTINO UMECHAMBUA VIZURI SANA RIPOTI YAKO NA RIPOTI MBALIMBALI ZA NCHI KWELI CHADEMA WANACHONGANISHA SANA JAMII YA WATANZANIA
 
Nadhani watanzania tuache ushabiki katika mambo yanayohusu maisha ya watu.
 
Nani mwenye mamlaka ya kutangaza hali yoyote ya hatari katika nchi? Mfano wa wazi kabisa ni pale tulivyovamiwa na Nduli Idd Amin Dadaa,Hayati Baba wa Taifa Mwl J.K.Nyerere akiwa amiri jeshi mkuu wa majeshi ya Tanzania aliutangazia umma tena ktk mkutano maalumu na vyombo vya habari juu ya uvamizi wa nchi yao kutoka kwa Idd Amin Dadaa.
Mfano wa pili na hata baada ya kutokea kifo cha baba yetu au baba wa Taifa Mwl J.K.Nyerere ni Rais wa wakati huo ndugu Benjamin William Mkapa akautangazia umma wa Watanzania kupitia vyombo vya habari juu ya msiba huo.
Nachotaka kusema kila nchi inautaratibu wake wa kutangaza majanga ya kitaifa naweza kusema labda majanga makuu yanayotokea au yanayotishia kutokea ktk nchi,kwahiyo Watanzania tuwe makini kwa hilo kwani wahenga walisema 'Miluzi mingi ilimpoteza Mbwa muelekeo' kwahiyo Watanzania kama kunatishio lolote la njaa Rais wetu ni mtu wa watu na nimpenda watu na Rais wetu yupo ndani ya jamii hii hii ya Watanzania, kama kunatishio lolote ktk nchi atautangazia umma juu ya tishio hilo kwa sababu yeye ndiye kiongozi mkuu wa Taifa hili teule.
Ni kweli kabisa Kiongozi, MWENYE JUKUMU LA KUTANGAZA JANGA AU TATIZO LOLOTE LA KITAIFA NI MKUU WA NCHI HUSIKA,, HAO WANAO TANGAZA TANZANIA INA NJAA WAMETOA WAPI HAYO MAMLAKA???? TUHESHIMU MIFUMO YA KATIBA TUHESHIMU MIFUMO YA NCHI
 
Back
Top Bottom