Pole sana ndugu yangu Kengemumaji, your source of information is not reliable. Hakika nilikuwa nafikiri kuanzisha uzi mpya kuhusu uongo wa ITV na kampeni za Arumeru Mashariki. Lakini sitafanya hivyo na badala yake nitachangia hapa ktk uzi wako hasa kwa mikutano ya leo ya kampeni za CCM ilifanyika Kikatiti na Patandi ambayo nilibahatika kuhudhuria na kusikiliza sera.
Ukweli ni kwamba watu waliojitokeza katika mkutano wa Kikatiti ulioanza mapema na hata ule wa Patandi uliomalizika saa kumi na moja jioni walikuwa ni wachache. Wengi wao walikuwa ni wakina mama na watoto pamoja na vijana wa green guard na wanausalama ie polisi wa FFU, makachero, usalama wa ccm ooops sorry Usalama wa Taifa ambao walikuwa wengi sana kuliko kawaida.
ITV wameonesha picha za siku ya ufunguzi na sio za leo maana mimi nilikwepo katika mikutano ya Kikatiti na Patandi. Sijui ITV wanafanya hivyo kwa malipo gani au wanajikomba kwa CCM tu. Jibu wanalo wenyewe.
Bahati mbaya sana hawajaonesha tukio la kundi la watu katika makutano ya barabara ya Arusha - Moshi ukiwa unatoka katika uwanja uliofanyika mkutano wa kampeni kuzomea msafara huo kwa kuimba mafisadi mafisadi mafisadi....
Msafara wa magari ya kifahari ya Land Cruiser VX V8 yaliyowabeba Mh Mkapa, Mh. Lowassa, Mh. Nnape, Mh. Wasira, Mh Mukama, Mh Sophia Simba na wengine wengi wakitoka mkutanoni hapo Patandi kuelekea Usa River. Hata utitiri wa wanausalama uliokwepo washindwe cha kufanya na badala yake kuwashauri madereva waongeze spidi.
Pole kwa kudanganyika na hiyo source yako ITV habari. Sio vyote ving'aavyo ni dhahabu!