Camilo Cienfuegos
JF-Expert Member
- Apr 23, 2015
- 19,230
- 68,253
Pesa Inafanya Dunia Inazunguka.
Huyu Mzee huyu, i hope Kikwete, Kinana na wenzake wamejipanga vizuri incase anakatwa jina.Hatakwenda kirahisi,itakuwa shughuli kidogo.
Sasa hapa EL anaonewa au hao wengine hawatendewi haki kwa kutosemwa? Kama vipi anza wewe kuwasema, it is a free country.I have a feeling kuwa Lowasa anaonewa, Hii inadhihirika hata humu jamvini, kashfa za ufisadi zilizofanywa na viongozi mbalimbali wa ccm waliotia nia ziko nyingi sana, kwa nini watu wanazungumzia sana richmond na kusahau hata escrow ya juzi? Mie nafikiri kuwa ufisadi ni ufisadi tu na yeyote aliyehusishwa na ufisadi wowote hafai kuwa rais. Hata yule aliyechakachua katiba yetu hatufai.
Hivi yeye lowasa ni nani mpaka aseme hakuna wa kumkata jina,?kwanini anaona yeye ndio pekee anaefaa kuwa rais na si mtu mwingine yeyote? Je anamtishia nani kutangaza maneno haya kwenye vyombo vya habari? Ngoja tusubiri tuone kama ccm wataogopa hivi vitisho vya huyu fisadi. Haiwezekani mtu mmoja tena fisadi atishie nchi nzima kiasi hiki.