Nyamgluu
JF-Expert Member
- Mar 10, 2006
- 3,160
- 1,727
Mkuu, unamaanisha kwamba jamaa ni fisadi lakini anawajali wananchi kuliko kina Pinda anayejiita mtoto wa mkulima lakini hana jipya? Kama kweli fisadi Lowasa leo hii kaonekana malaika, pamoja na fedha chafu anazomwaga kwa wananchi na ambazo hazijulikana kazipataje, hiki ni kiashiria tosha kwamba kweli CCM wameishiwa viongozi....kuna ombwe kubwa sana la viongozi ndani ya CCM!!!!
Mkuu mbona umeeelezea vizuri kuliko hata mimi!! Yani ndio nilichotaka kusema. Marekebisho madogo tu, naona umezidisha chumvi kusema tunamwona malaika. Hakuna malaika, tunajua ni fisadi lakini pia ni kichwa he is an intelligent man. Kuna viongozi CCM hata danguro huwezi kuwapa waendeshe lakini lowasa unampa kampuni yako huku ukijua pamoja kuwa utaibiwa lakini faida utaiona na kampuni haitakufa sababu ni mtu mwenye PRIDE na ni mwenye chongo kati ya vipofu!