Lowasa aukana urais

Lowasa aukana urais

Always, ukweli ni mchungu, lakini inabidi usemwe.
Lowassa ni fisadi, ni kweli, lakini watanzania wengi wanamkubali, huo nao ni ukweli hata kama hatuutaki.
Katika pita pita zangu kila sehemu ninayofika hata kama ni safari za mikoani huwa najaribu kuchokoza mada za siasa ili kupata mawazo yao. Wengi wanajua kuwa jamaa ana kashfa, ila wanasema ni mchapakazi. Wengi wanasema kama Lowassaa atapitishwa kuwa mgombea bila shaka watampa kura yao. Naomba msinishambulie mimi mgeni jukwaani bandugu:lock1:


kama mwizi mbona hawampeleki mahakamani bana, huwezi mwita mtu mwizi tu from no where...na kwa sabb wameshindwa kumpeleka mahakamani hiyo inathibitisha kuwa lowasa sio mwizi..na ndio mana watu tuna imani naye..

ukiangalia kwa mapana yake kunzia serikali hadi wapinzani wote wezi tu!!!!!! kwani hujasikia huyo mbowe anakopesha chama chake hela na baadae anajilipa mamilioni zaidi? anaununua vifaa bya chama mwenyewe na chenji anawekandani..anafanya hayo kwa kushirikiana na watu wake wachache ndani ya cdm..hapo hajapewa wizara au uraisi itakuwaje?
kwa kifupi watanzania wengi hawajui tu kwamba siasa ni ajira na kwamba wanasiasa hawako kwa ajili ya wananchi bali kwa maslahi yao..mpka uelewe haya ndio utaelewa kuwa hakuna mwanasiasa msafi kizazi hiki
 
.... lazima asimame mtu mwenye mvuto na ushawishi kwa watu wa lika zote,E.L ni moja kati ya watu hao,ama magufuli,lakini kama tutataka rais mwanamke basi Mama rose anaweza pata nafasi hiyo.

Nyekundu:

Rais wa mvuto ana gharama kubwa sana ...waulize bei ya rais huyo watanzania walioshiriki uchaguzi mkuu kuanzia miaka ya 2000. Kwa kifupi sifa hii haifai kutiliwa maanani kupata rais wa Tanzania.

Bluu:

Ushawishi waweza kuwa muhimu kama utatumika vyema kwa viongozi husika. Lakini ushawishi ukitumika vibaya yaweza kuwa yale ya akina Lamwai, Mrema wa CCM, NCCR-mageuzi na TLP ya sasa, Kafulila, Kaburu wa enzi hizo,..na sasa Zuberi. Pia ushawishi ukitumika vizuri yaweza kuwa yale ya akina Baba wa Taifa.

zambarau:

Kuchagua rais kwa kigezo cha jinsi (me au ke), huu ni ubaguzi mwingine wa kijinsia...ambao unalenga kuwagawa Watanzania kwa malengo yaleyale ya propaganda za kishezi zinazogawa watanzania kwa ukabila, udini, rangi, ukanda na mengine kama hayo. Pia hii itakuwa inaendeleza udhalilishaji wa jinsi ya "ke" kuwa haijiwezi bila kupendelewa na kwa namna moja ama nyingine , pia mnazidi kujenga badala ya kubomoa mfumo dume.

Rais atokane na sifa za kiongozi bora. Jinsi ya mtu kamwe haitakuja kuwa sifa ya kiongozi bora kwa Watanzania wanaohitaji kusonga mbele kimaendeleo kwa kujitegemea bara bara.

Engineer (ni kidhani eng. uliyoambatanisha kwenye ID yako inawakirisha sifa hiyo) rudi design room uandae mkakati mpya wa kupata Rais anayefaa kuiongoza Tanzania, huu wa sasa uko chini ya kiwango kwa asilimia mia moja.
 
Nyekundu:

Rais wa mvuto ana gharama kubwa sana ...waulize bei ya rais huyo watanzania walioshiriki uchaguzi mkuu kuanzia miaka ya 2000. Kwa kifupi sifa hii haifai kutiliwa maanani kupata rais wa Tanzania.

Bluu:

Ushawishi waweza kuwa muhimu kama utatumika vyema kwa viongozi husika. Lakini ushawishi ukitumika vibaya yaweza kuwa yale ya akina Lamwai, Mrema wa CCM, NCCR-mageuzi na TLP ya sasa, Kafulila, Kaburu wa enzi hizo,..na sasa Zuberi. Pia ushawishi ukitumika vizuri yaweza kuwa yale ya akina Baba wa Taifa.

zambarau:

Kuchagua rais kwa kigezo cha jinsi (me au ke), huu ni ubaguzi mwingine wa kijinsia...ambao unalenga kuwagawa Watanzania kwa malengo yaleyale ya propaganda za kishezi zinazogawa watanzania kwa ukabila, udini, rangi, ukanda na mengine kama hayo. Pia hii itakuwa inaendeleza udhalilishaji wa jinsi ya "ke" kuwa haijiwezi bila kupendelewa na kwa namna moja ama nyingine , pia mnazidi kujenga badala ya kubomoa mfumo dume.

Rais atokane na sifa za kiongozi bora. Jinsi ya mtu kamwe haitakuja kuwa sifa ya kiongozi bora kwa Watanzania wanaohitaji kusonga mbele kimaendeleo kwa kujitegemea bara bara.

Engineer (ni kidhani eng. uliyoambatanisha kwenye ID yako inawakirisha sifa hiyo) rudi design room uandae mkakati mpya wa kupata Rais anayefaa kuiongoza Tanzania, huu wa sasa uko chini ya kiwango kwa asilimia mia moja.

naomba uelewe kuwa,vyama vya siasa duniani kote vinamalengo yanayofanana,nayo ni kushika dola,kama ni sawa,basi usitegemee kuona jiwe likisimamishwa ktk chaguzi yeyote ile duniani.na kama huamini hili basi ktk chama ulipo labda malengo ni kupokea ruzuku tu na si kushika dola.
kila chama kinajitahidi kumsimamisha mtu atakewezesha chama kushika dola.hata kama hapo ulipo ni mpiga kazi na huna mvuto kwa wapiga kura,usitegemee kupata mafasi ya kupeperusha bendera ya chama chako,kwani utawapotezea malengo yao,labda tu iwe ni chama cha kusindikiza wengine na kusubiria ruzuku kama ndio chanzo zha ajira na maisha kwa viongozi huzika
 
ni kwamba,wewe unaweza usimpe,lakini waendesha boda boda na marafiki zake,jamaa ndugu na majirani watafanya hivyo,unaweza usiamini kitakachotokea,lakini ndio siasa ilivyo kwani vyama vyote duniani malengo yake ni kushika dola na si kupaka wanja na kikawaida huwezi kusimamisha jiwe kama unahitaji kushika dola,ni lazima umsimamishe mtu mwenye uwezo na mvuto kwa jamii,ndani ya ccm E.L anao uwezo huo,akifuatiwa na Dr. magufuli,Dr.makyembe,lakini kama tutahitaji rais mwanamke basi mama Dr.migiro anaweza kusimamishwa

No wonder why, our cities are poorly planned and buildings made ready to collapse.
 
Ngoyai is your next President.

Kaeni mtulie hata wana boda boda wanafahamu
 
Umiliki wa chombo cha usafiri kwa vijana kunawasaidaje vijana kumuwezesha kuwa na maendeleo endelevu (sustainable development) ukizingatia changamoto za kumiliki chombo hicho?

umiliki wa chombo hicho kwa vijana utamsaidia Lowasa kutengeneza ngazi ya kuelekea kwenye urais, ijapokuwa sasa hivi anajishaua kwamba hautaki urais.
 
....mtu hatari ni yule anayejifanya hataki kumbe anataka,inamaana yupo radhi kufanya lolote kisirisiri...
 
Always, ukweli ni mchungu, lakini inabidi usemwe.
Lowassa ni fisadi, ni kweli, lakini watanzania wengi wanamkubali, huo nao ni ukweli hata kama hatuutaki.
Katika pita pita zangu kila sehemu ninayofika hata kama ni safari za mikoani huwa najaribu kuchokoza mada za siasa ili kupata mawazo yao. Wengi wanajua kuwa jamaa ana kashfa, ila wanasema ni mchapakazi. Wengi wanasema kama Lowassaa atapitishwa kuwa mgombea bila shaka watampa kura yao. Naomba msinishambulie mimi mgeni jukwaani bandugu:lock1:
Ni kweli wanamkubali ila na sie wananchi watz ni noma aisee tunaongozwa na watu wasiozidi 20 ambao wakisema Lowasa ni mbaya kila mtu atasema mbaya kama ilivyotokea miaka iliyopita na sasa hivi tena wananchi wengi wanaonekana kusema Lowasa mzuri, usishangae tena miezi michache kabla ya kuchukua fomu hali ikabadilika tena na kuanza kusema mbaya tena wale wale waliokuwa wanamsifia wakabadilika
 
Kama ni kumchagua devil mwenye kufaa kutoka CCM! basi Lowassa ni afadhali mara 1000000000000000000 times
 
Ktk viongozi ambao Chama Cha MIZIGO kimebahatika kuwapata ni pamoja na Huyu EL!HOFU NI AFYA YAKE HAWEZI KUKAA MADARAKANI KWA ANGALAU KWA 5YRS,

sasa utamfananisha lowassa na huyo babu yenu mnywa gongo mwenye kifafa?
 
Back
Top Bottom