Love melted before my eyes

Love melted before my eyes

Hii ni story ya throw backs!

Yaani matukio mbali mbali yaliowatokea waTanzania wanaoishi Tz, Canada, China na UK
Kulingana na maisha waliyoishi~wanavyoishi

Kwasababu ni ndefu sana na wabongo mnapenda kulia lia nikirusha waya mrefu, basi nafupisha!

Badala ya kuanza na mwaka 2008 naruka mpaka mwaka 2014 hadi 2017

Enjoy

Beige:

Baada ya kupigwa na maisha, mambo hayaendi, mambo machungu, mambo magumu, mambo yamesimama,nikikwambia ni sheeedah

Kwa malalamiko yake yeye mwenyewe anajiongelea rohoni

Nimemaliza chuo UK, nimerudi nimetafuta kazi weee lakini wapi! Utadhani nina gundu! Mzee wangu anajiandaa kustaafu, tangu mwaka 2010 mpaka 2014 sijaitwa hata sehemu 1 kwa interview
Nikaamua kwenda kujisomea masters, nikamaliza nikarudi tena Tz, pamenunaa, kweli bongo sio pamchezo mchezo.

Nikajua mzee wangu kuajiriwa kwake kwa miaka mingi nitapata connection hata kwa marafiki zake lakini waaapi! Kila mtu amenuna! Hakuna cha msaada kwa mjomba wala shangazi wala best friends

Basi najikaliaga tu ndani naangalia tv nikaamua kufanya angalau vibiashara, weee! Kama nimetikisa kuzimu! Biashara haiendi
nimeuza nyanya, nimesambaza dagaa maofisin kwenye mabenki na majumbani na nyumba za ibada, nguo za kike na kiume za mitumba nimeuza, mtoto wa UK nimechooookaaa yani nikaona Mungu kaenda likizo kulala! Maana sio kwa kupauka huku! Utadhani nimeshushwa Mbinguni kuja duniani kuhubiri injili! Jesoooooos Christ Mungu jaman nihurumie Abeg.

Nilikuwa na ki bwana changu ki boyfriend nilikipata UK, yeye akawa ameshapata kazi, akawa ananipetipeti elfu 20, elfu10, laki 2 inategemea na mwezi ulivyowaka kwake. Lkn me sikuridhika na ile hali, japo naishi na wazazi lakini bado asee, wazazi hawawezi kuku- support hela kiila siku, Hakuna kitu kinasumbua kama kukaa nyumbani miaka 4 hauna kazi, hauingizi pesa, hauingizi shilingi, me mtoto wa kike, ninamahitaji yangu,nikijiangalia ni mtu wa maendeleo, napeeeenda maendeleo, nina akili ya maisha, nimefanya biashara zote zimekataaa, sasa nimebakia nawaza sijui nimelogwaaa au?!

Kwakweli kama kuombewa nimeombewa sana tu, hakuna mtu anaetoa sadaka kama mimi, sijui 1st fruit (malimbuko), sijui zaka (thithe) hata siibi, sadaka za kila j2 nipo, michango ya kanisani na ahidi ikifika siku ya tukio kulipa sina hata sumni, basi Mungu ananiona ananisamehe, nikaacha mchezo wa kuahidi kanisani. Maana sina chanzo cha kuniingizia pesa mjini!

Yani ukiniangalia mimi.Beige wa UK sio Beige wa Dar

Kukawa na reunion ya watoto tuliosoma UK, tunajijua sie, tulivyo na swaga za kufa mtu!

Nikashindwa kwenda ila natamani
Wakarusha whatsapp sherehe ilivyobamba, wakaandika tumekumiss Beige, bila wewe shughuli haikunoga kiviiile, uuuwi nikamshukuru Mungu maana ningeenda na tenge langu pale ingekuwa noumer! Niliuzaga nguo zangu zooote za UK wakati nauza nguo za mitumba, nikabakiwa na nguo za kibongo, sikuweza hata ku attend reunion.

Mzee akastaafu bwana hapo ndo niliijua kuzimu inafananaje. Maisha ya shida, hapa nilipo nina CV 10 za aina tofauti tofauti, nimesha apply kazi elfu 8 lakini sijaitwa interview hata 1, dah Mungu jaman Mbona unanionea?!
Maisha yangu ni kuchat whatsapp na kuforwad sms za kuchekesha

Biashara zote ziligoma, nimeuza mpaka vitenge wapi, kwanza watu wanakopaaaa, jamani wabongo wanakooopaaa! Kulipa sasa ni sheedah! nimeanzisha blog wapi, yani utadhani kuna shetani ametumwa akae tu na mimi benet aniharibie

To make a long story short, rlshp yangu na yule boyfriend ikawa a-mess, tulianza from scratch! Lakini alipokaa juu kwenye high horse, akaniona me kama mavi, nikamfumania fumu, kiruuu, na mdada m1, ambae nilikuwa na suspect, yeleuuuwi nilichanganyikiwa, rlshp ya miaka 8, mwanaume anakutupa nje kisa hauna kazi, hela, nililala home kama kichaa, naliaaaa.
Sio kama sikuwa na wanaume waliokuwa wananipenda, wanataka kunioa lkn nilikuwa zuzu enuf kuwakataa, nilikuwa very faithfull na rlshp yangu, nikaliaaaaaaa, liaaaaaa, jamaani nililiaaaaa, mamangu mzazi halali alijua ntajiuaaaaaa, nikawa kama nimechanganyikiwaaaa, asee Mungu tu na Mama yangu ndio wanajua, kupotezewa miaka 8 ya mahusiano ni mbayaaaaa, nikakaa mwaka mzima nalia, natukana, nimechanganyikiwaaa, naliaaaaa, dada zangu wanapiga simu wako UK, CANADA wamesikia nimetendwaaa, wananiambia we told u soooo, fanya mpango ukuje ukae hukuuu, mama anawaambia hapaanaaa, huyu ndo namtegemeeaaaa, ndo kila kitu hapa ndani, mwacheni akae na mimi

ITAENDELEA SAA 10 JIONI

This story must be true Ic,Imenikumbusha story ya Dem Wangu

Nilikua na dem katoka UK kamaliza degree yake ya kwanza alikua ana swag sana yani nilikua nikitaka kumtoa out ananiambia sasa hapa mbona ovyo , wakati ndio kamaliza chuo tu hana hata pesa,ndio kwasababu nilimpenda nikawa na go with it

akawa ananiambia mimi sitaki kazi ya mshahara less than 1M enzi hizo 2011,Aka apply kazi akawa akiitwa kwenye interview anataja mshahara kubwa ikawa wanampiga chini coz ilikua nje ya Budget

Akasema ngoja kwanza apige ACCA yani CPA ya UK ili akiunganisha na degree yake ya UK aajiliwe kama Chief Accountant mshahara uwe mrefu zaidi nikawa nawaza vipi awe chief accountant bila uzoefu nikamshauri aanzie msharara mdogo ndio uzoefu utampa mshahara mkubwa hakunisikia,Alipo jaribu kuappy VISA ili arudi UK aka chukue hiyo ACCA ubalozi wa UK kipindi hicho uko Kenya sijui kama wamesha rudi dar kwa sasa, wakampiga chini so VISA akakosa na kazi akawa hana

Kipindi hicho mimi ni kawa nishaanza kumpotezea taratibu coz nilimuona sio wife material hakuwa na mawazo ya uhalisia wa maisha ya Tanzania.

Nikapata kazi mkoa,Tukawa tuna wasiliana kama marafiki tu, akanipigia simu siku hiyo analia maisha ni magumu sana anatafuta kazi yoyote coz home kwao kushakua kwa moto anazinguliwa na kaka zake kisa anaonekana haoneshi juhudi za kusaka kazi

Saizi kazi EXIM Bank analipwa Mshahara Sh 270,000 baada ya makato amechoka mbaya ,Nilipo onana nae akaniambia saizi amenyooka alikua anajidanganya sana sana alipo fika from UK kwani alikataa mshahara wa laki 8 na mpaka saizi ungekua umesha ongezeka.

Umri wake umekwenda ana 30 yrs ananiambia anataka mchumba wa kumuoa ila hajapata anahisi hata olewa kabisa

In my heart nikawaza angekua mke wangu ila ndio tayari nishaoa na nina watoto sasa.

She is so lonely

Nilicho jifunza kutoka kwa huyu dem wangu wakitambo ni kwamba wasichana wengi wanaotoka kusoma nchi za nje huwa wana expections kubwa sana

Nawaomba wabadilike
 
This story must be true Ic,Imenikumbusha story ya Dem Wangu

Nilikua na dem katoka UK kamaliza degree yake ya kwanza alikua ana swag sana yani nilikua nikitaka kumtoa out ananiambia sasa hapa mbona ovyo , wakati ndio kamaliza chuo tu hana hata pesa,ndio kwasababu nilimpenda nikawa na go with it

akawa ananiambia mimi sitaki kazi ya mshahara less than 1M enzi hizo 2011,Aka apply kazi akawa akiitwa kwenye interview anataja mshahara kubwa ikawa wanampiga chini coz ilikua nje ya Budget

Akasema ngoja kwanza apige ACCA yani CPA ya UK ili akiunganisha na degree yake ya UK aajiliwe kama Chief Accountant mshahara uwe mrefu zaidi nikawa nawaza vipi awe chief accountant bila uzoefu nikamshauri aanzie msharara mdogo ndio uzoefu utampa mshahara mkubwa hakunisikia,Alipo jaribu kuappy VISA ili arudi UK aka chukue hiyo ACCA ubalozi wa UK kipindi hicho uko Kenya sijui kama wamesha rudi dar kwa sasa, wakampiga chini so VISA akakosa na kazi akawa hana

Kipindi hicho mimi ni kawa nishaanza kumpotezea taratibu coz nilimuona sio wife material hakuwa na mawazo ya uhalisia wa maisha ya Tanzania.

Nikapata kazi mkoa,Tukawa tuna wasiliana kama marafiki tu, akanipigia simu siku hiyo analia maisha ni magumu sana anatafuta kazi yoyote coz home kwao kushakua kwa moto anazinguliwa na kaka zake kisa anaonekana haoneshi juhudi za kusaka kazi

Saizi kazi EXIM Bank analipwa Mshahara Sh 270,000 baada ya makato amechoka mbaya ,Nilipo onana nae akaniambia saizi amenyooka alikua anajidanganya sana sana alipo fika from UK kwani alikataa mshahara wa laki 8 na mpaka saizi ungekua umesha ongezeka.

Umri wake umekwenda ana 30 yrs ananiambia anataka mchumba wa kumuoa ila hajapata anahisi hata olewa kabisa

In my heart nikawaza angekua mke wangu ila ndio tayari nishaoa na nina watoto sasa.

She is so lonely

Nilicho jifunza kutoka kwa huyu dem wangu wakitambo ni kwamba wasichana wengi wanaotoka kusoma nchi za nje huwa wana expections kubwa sana

Nawaomba wabadilike

Dah pole sana rafiki! Itabidi me na wewe tuonane asee ... ningependa kumfahamu ex wako maana nahisi amepita alikopita Beige
hatasielewii hii story

Kiruu! Huelewi nini sasa! Pole sana
 
Duh! Pamoja na kuwa haijaisha hii story yako, lakini nimekuonea huruma sana. Pole sana.
 
DISSASTER'S SHOW:

Ah me bwana me sina maneno mengi, me hard core kama kawaida, yani habari za madem wala sinaga
Unajua bwana me nimezaliwa kwa Mbagalaa kama Diamond, maisha magumu rafkizangu we acha tu, hapa nilipo naona kama nipo ulaya!

Wenzake wanacheka, enhe na jina la dissaster ukapewa na nani?!

Dissaster:
Ah hili la jina nitawaambia, basi bwana maisha yangu na wazazi wangu mbagala, kwanza me mamangu alinizaa peke yangu baadae akawa hawezi tena kuzaa, aliolewa akiwa mkubwa kwa babangu amempita mzee wangu miaka 7 mbele

Wenzake : tobaaa, suga mommy!

Dissaster akaendelea ndio kunipata mie kwa kisu kuchomolewa sipumui, wakachapa chapa na wewe wakajua nimekufa, wakampa mama anishike kwa mara ya mwisho akawa analia ananikumbatia anasali nikapiga chafya achuuuu!

Wenzake wanachekaa, we bwana me niliwaambia huyu ana vituko kuliko mbwiga wa clouds fm! Akajisemea Gabon, enhe endelea stering!

Dissaster: basi wakaniita muujiza lakini kufika home nikakua mpaka naanza nursery ilo jina la miujiza silipendi, me jina la cheti muujiza shaban, jina la mtaani dissaster ukija kwetu uulize muujiza haunipati
Basi utani utani shuleni na nini, eh kuja kushtuka naonewa nasemwaaa nikawa sikubali naenda mazoezi uwanja wa yanga, napiga tizi na wala unga wa mtaani ila me stumii basi tu nabeba mabablish!
Nikafika la 7 nimepaaanda juu kama Johnny Bravo wa cartoon network!
Che! Wanawake wananishambulia me ndo don shuleni, kesi yoyote leta na solve kwa hela, ugomvi wowote na solve kwa biti,ntakupiga, ntakudundaa, napiga vitoto vikaniheshimu, akina dada ndo sana tuu chapa pumbuz kwa condom, nilikuwa sina akili kilaza wa kufa mtuu, ni sheedah!
Basi la7 nikafeli nikaenda shule ya private jitegemee, dah huko ndo kabisaa, ni balaa yani kama wametoa moto wameweka makaa kwenye motoo nachapa ngumi kama mjeshi, asbh me ndo naongoza gwaride na mazoezi nikawa kiranja mkuu akili sina F ndio eneo langu, tukavuka form 2 form 3 form 4 matokeo nina div 3 sikuamini, me dissaster imekuwajeee?! Sieleeeewiii! Nikapata shule Makongo, kule ndo kabisaa mnatembea toka mwenge mpaka makongoo kwa mguu, acha tu form 6 nikapata div 3 tena ndipo nikaanza kujikubali, nikaangukia CBE hapo karibu na mnazi mmoja piga first 1 nikapita, 2nd yr, nikapita, 3rd yr nikakamatwa na Sapu 2, tukapiga kitabu weee wenzetu wakanunua pepa waarabu, mjeda nimetuna tuna pepa ikaletwa kibabe tukasoma majibu asbh mtihani wenyeweee, tukapitaaa nika graduuu, nikaja kupata ajira na advance diploma yangu ya CBE hapo NMB
TUKAANZA kama field miezi 6, wakatuongeza miezi 6 mwakaaa tunasotea hamba mshahara ni nauli tuuu, tukaja ingizwa kwa payroll mshahara wa kwanza laki 3 ukukatwa kodi inabakia laki 240. Dah nikachokaa lkn poa tu sa unafanyaje, nikaitamani sana CRDB lakini kila nikiapply siitwi basi nikatulia zangu NMB na bimkubwa nyumbani akafurahi mwana nimepata ajira hata kama nalipwa elfu 10 fresh tu


Nikapiga kazi wee miaka 3 mshahara nikapandishwa nilihamishwa department, ukafika mpaka mil1.2 net salary, bimkubwa akafurahi nikaupeleka mshahara wa kwanza wote kwa mama na baba, wakauombea pale wakagawana pasu kwa pasu me nikaondoka mikono mitupu nikawa na survive na vi hela vyangu vya awali kabla mshahara haujapanda

Asukwambie mtu sikuelewa kwanini yalikuwa yananitokea hayo, baada ya kupeleka mshahara kwa wazee jamaa nikaanza kubadilishwa idara, nenda marketing, nikakaa marketing miaka 2, hela nje nje kudadeki yani me mshahara naweza nikawa sijaugusa miezi 3 naishi kwa zile deal za marketing, unaenda huku mtu anakutoa elfu 20, 50, laki 1, kha sa me nishazoea yale maisha ya kujibana na laki 2 kwa wiki naweza kusanya hela za nje kama hata laki 4 mpaka 5 inategemea yani kima cha chini laki 1 kiiila wiki nje ya mshahara

Nikaanza kupata connections za watu channels nini napata watu wananiambia habari za biashara fungua hiki fungua kile nikaona nifungua bar yangu kule mbagala
Unajua si kwetu sio waislam saaana lakini waislam, nikamkaribisha mzee pale akafurahi, yeye anasimamia counter mauzo bimkubwa kashika jiko!
Bar ikakolea bwana mauzo yakapandaa, kwa siku tunauza mil 4 mpaka 5, kwa investment ya mil 2, ilivyofika miaka 2 tukanunua lile eneo, mzee ali fight mpaka mwisho, bar ikawa yetu hatulipi tena rent, maisha yakaanza kubadilika, Mbagala kule tena tukahama tukahamia nyumba za kariakoo za NHC, rent kwa mwezi laki 2 ndogo sana kwetu, nyumba ya mbagala tukai renovate tukaipangisha, me bado nipo NMB sitaki kupaachia pale, wala hamna mtu anaejua kuwa nina baa ila nawaambia tu kuna bar napendaga kukaa maeneo ya home so washikaji wanakuja tunakunywaa wee maana hawawajui wazazi, hii dunia ukitaka kufanikiwa fanya mambo yako kimya kimya sio unabwabwaja mwanaume kama umeulizwa tutaanza kukuhisi we shoga au sigara kali!
Miaka 5 nimekaa NMB hakuna anaejua kuwa nina bar! Nikaongeza tena saloin barbershop pale kinondoni studio, rent laki 2 nikaingia lipa kodi ya nusu mwaka nikaweka vijana wawili, tunalipana kwa percent! Bwana wale vijana walipiga mzigo, palikuwa panapakije magari,

Pembeni pana boutique la nguo za kiume, mie mjeda nina saloon hajui mtu

Ofisini tukapewa seminar ya kuwekeza kwenye hisaa, nikawekeza mwana his TBL, SIGARA, TWIGA CEMENT, SWISSPORT, NMB, CRDB, hakuna anaejua zaidi ya wazazi basi

Nikamnunulia bimkubwa ka vitz na mzee akachukua Noah, wapo buzy wana run bar kama yao kumbe yetu, mambo yakatiki nikarudi shuleni, nikaenda kusoma degree mlimani, ndio kukutana na Gabon, analia liiia mwenyewe kaachwa na Suzana nikamwambia we njoo saa 8 usiku fala wee uone unavyoibiwa

Toni akasema kumbe huyu boya ndo alikutonya?! Wakacheeeeka, Gabon akawajibu me niliwaambia huyu dissasster ni sheedah! Mengine sikutaja kusema nikaacha nikijua kijana atamalizia!

Dissaster akaendelea kufunguka nikasoma zangu BCOM shule ikaisha nikapanda daraja kazini toka marketing kwenda finance, hela ikaongezeka lakini kiukweeeeli toka moyoooni mshahara hata sijui ji bei gan upo benk sijauchungulia huu mwaka wa 3, hela inayoingia bar na kule saloon sina hata muda wa kuangalia mshahara, nikajiongeza nikanunua Verossa yangu kali nyeusii nikaweka tainted vioo, maisha yanaenda nikahama kariakoo nina hadhi zangu nikarent mikocheni nikawaacha wazazi kkoo.
Tukawa tunawasiliana na Gabon weekend tunatoka tunakunywaaaaa Isumba Lounge pale upanga maisha yanakwenda, hakuna hata m1 anataka kuongelea kuhusu pussies yani kama mie nina pending pussies kibaoo! Na delete tu na delete tu sio kwamba sina hamu kama anavyosema Gabon haya mambo ukiendekeza utakuwa mlemavu wa akili, kweli uzinzi kitu kibaya sana Mungu tu alijua akatuonya tukae mbali ile kitu inakukula sio kitoto,

Sasa hivi ndio nina plan ya kuoa yani hapa natafuta mwana mkaaaaali kuna demu m1 nilimwona vodacom anaitwa nani tena yule Gabon, anaitwaaa Hot Momma, kale kadem kamenyooka sio kitoto, yule ndo naangalia angalia kama naweza pata maisha pale ila zaidi ya pale sidhani

Toni akamwuliza ukiskia kaolewa je

Dissaster: kaolewa ten?! Ebwana ee wee usinifanye nikalia sahivi! Mmh makubwaa au unamfahamu?!

Toni: niliskia watu wanamwongelea Barclays anashogake si yule yupo hivi na vile
Dissaster: enhee huyo huyooo
Toni: kaka labda uwe unamwibia mumewe lakini najua ameolewa sana tu, tena juzi kati jamaa alimfukuzia mpaka kwao kamfanyia fujo nini, me niliskia harusi ilikuwa kali mjini wadada wa pale bank walienda wakawa wanarusha selfies na nini kwenye ma instagram nini, ni sheedah!

Dissaster akanyong'onyea ghafla, wanamwuliza kaka vepee?! Kwani mwanamke yupo pekeyake?! Tafuta bwana mwengine kwani Tsh ngapi?!

Dissasster: akawa mpolee ghafla kama kuku kamwagiwa maji, basi niacheni tu niondoke hata hamu ya chakula sinayo, dah! Akachukua simu yake kaingia kwenye gari huyoooo moto bati, wenzake wanashangaa

Gabon akasema haya mambo ndio nisioyataka, misalaba ya kizembe kama hivi sipendi sa analia nini?! Kha
Akina Toni na Mr Wonder wanacheka, kuangalia saa sa 4 usiku wakaaga haoo wakaondoka




ITAENDELEA SAA 4 USIKU

Hahahah nimempenda disaster..
 
@ Money Penny kwanza napenda kukupongeza kwa kipaji chako cha uandishi, natumaini hii imetokana na "hobbies" zako za kupenda kuangalia movies etc. Hivyo nakushauri uangalie jinsi unavyoweza kubadili hobbies kuifanya biashara.

Kama ulivyo eleza kuwa umechukua miaka mingi kutafuta kazi kumbe kazi ulikuwa nayo bali kwa bahati mbaya ulikuwa huitambui, hata hivyo bado hujachachelewa, endeleza kipaji chako cha uandishi iwapo mwanzo inaweza kuwa ngumu lakini nina uhakika mwisho wa siku utafaniliwa. Hii inaweza kwenda sambamba na jinsi unavyo weza kutumia e marketing katika katika kupanua wigo zaidi hivyo waweza wasilia na tech section wakushauri au tuwasiliane inbox.

Wazo na ushauri tu.
 
Endelea kuchagua wanaume ka unachagua movie,siku ukija kustuka.....waya haah haah

Weweee! Nakuona nakuona single boy
Unalalamiiiikaaa niaaaaajeeee!!
@ Money Penny kwanza napenda kukupongeza kwa kipaji chako cha uandishi, natumaini hii imetokana na "hobbies" zako za kupenda kuangalia movies etc. Hivyo nakushauri uangalie jinsi unavyoweza kubadili hobbies kuifanya biashara.

Kama ulivyo eleza kuwa umechukua miaka mingi kutafuta kazi kumbe kazi ulikuwa nayo bali kwa bahati mbaya ulikuwa huitambui, hata hivyo bado hujachachelewa, endeleza kipaji chako cha uandishi iwapo mwanzo inaweza kuwa ngumu lakini nina uhakika mwisho wa siku utafaniliwa. Hii inaweza kwenda sambamba na jinsi unavyo weza kutumia e marketing katika katika kupanua wigo zaidi hivyo waweza wasilia na tech section wakushauri au tuwasiliane inbox.

Wazo na ushauri tu.

Hahaha. Asante kaka, jaman mimi sio Beige mbona mnanichanganyaa?! Njoo inbox kaka nikupe no yangu tuongee seriously! Ila umenifagilia mbaya mpaka naona aibu. God Bless you
 
Back
Top Bottom