Love melted before my eyes

FUK~MI:

XITANG!
Kama napaona! Kha kile kijiji sikipendi, naskia pameendelea eti, to hell! Sipataki hata kupaona na wale wanakijiji naskia wengi waneshakufa, ila watoto wao bado wapo, bora mama yangu aliondokaga huko maana sio kwa ushenzi waliotufanyia

Mama yangu alikuwa anauza bar, analala bar, nyumba yake ndio bar, walevi wakilewa anawafukuza, mama yangu alikuwa mrembo sana, sana hakuna kijiji kizima hakuna, wale mabwashee walijaribu sana kumtaka anawakataa

Alipendanaga na mtoto wa mwenyekiti wa kijiji, zamani mtoto wa mwenyekiti wa kijiji ilikuwa deal sio kitoto, mama yangu kwao walikuwa maskini wa kufa, ila alikuwa mrembo hakuna mfano, wakapendanaaaa na huyo mtoto wa tajiri, mama wa mtoto wa tajiri hakupenda akawatenganisha kea kumpeleka kusoma nje, mama yangu alivyoambiwa wakapanga waonane chini ya mchungwa, ndio kupigana mabreka mtoto wa mkuu wa kijiji akasepa! Baada ya mwezi mama anamsaidia mama yake kuuza genge akaanza kutapika, tapika na wewe hospital moja, kufika ana mimba ya mwezi mmoja, mama alipigwaaaa pigwaaa kuanzia hospital mpaka home akaona isiwe shida, babu yangu akamtetea akakaa pale mpaka akajifungua ndio nikazaliwa mie Yoorèn!

Hilo jina hata usitake kujua maanake, ina maana ni mkojo! Yani me nikaitwa mkojo na mamangu kweli ina sound jaman au dharau hizi?!
Nilipofikisha miaka 10 mama akaondoka kwa wazazi wake, akawa anaishi kwake anauza bar, mie nikaanza shule shuti kutaniwa jamaa, yooorèn yooorèn, shule ikawa chungu mpaka namaliza chekechea, doh! Nimechokaa!
Nikaanza darasa la 1, mambo ni hivyo hivyo mpaka darasa la 5, akarufi yule bwana aliempa mamangu mimba, nikapelekwa kuwa mie ndo ile product ya love waliofanyaga kwenye mchungwa! Mama mkwe wa mama yangu akawaka, hataki kuniona, ila baba yangu alinifurahia kweli, akawa anakuja bar ananiona kwa siri ananiachia hela, ananibembeleza ananiambia me ni msichana mreeembo sana wala nisikasirike hamna mrembo hapo kijijini zaidi yangu, nikifika shule wakinitania nawaambia me ni msichana mreeembo sana kuliko wote duniani wanashangaa, nikawa mtemi ghafla, nina confidence, datasa la.7 likaisha, nikawa k
mkubwaaa, nimeshakuwa mdadaa mreeembooo, shape ya kichinaaa! Mzuuuriii, baba yangu akanipeleka private schools bila bibi kujua, nikapiga shule, nakuwa wakwanza kila siku, nikamaliza form 6, nikapata scholarship kwenda UK, University of Birmingham, nikamuacha mama ingawa roho yangu ilikataa sana, nikaenda kwa ubishi kuwa baba atamwangalia mama, nikapiga 1st yr, 2nd, 3rd, mitihani ikaisha, nikaja kuitwa na head of school, kwenda kuambiwa mama yangu amekufa! Nililiaaaaaaa sikuelewa kwanini, nikaambiwa nirudi kuzika mama, kurudi nilikuwa na mtu wa mochwari na baba yangu, hamna cha mwana kijiji wala wale wanaokunywaga kwa maza pale bar, tukazika kichina china baada ya siku 3 akaja mtu ameshikilia sanduku, kumbe ni lawyer, akasema kuwa kuna mirathi iliachwa pale na mama, ambayo ni nyumba na pesa kidogo, kuangalia pesa kumbe ni dola 10,000 skuelewa mama alizitoa wapi ni pombe tu au?! Tukaangaliana na baba hatukuelewa nikamwuliza baba we ndo umefanya haya akasema hapana! Basi nikafanya yangu nikasaini zangu makaratasi nikaelekezwa shekeli zilipo tukasepa na baba mpaka eneo la tukio nikasaini nikaambiwa unataka zibaki benki au uchukue nikasema zibaki bank tukarudi home
Baada ya siku 3 ya tanga nikamwuliza baba kitu gani kimemwua maza, alipoanza kunielezea gari nje ikaingia, bibi mzaa baba akaja, baba akanibusu kwenye paji la uso akiahidi kuwa atarudi kunielezea, akaondoka, nikafunga milango yoote nikakimbia mpaka kwa bibi na babu
Kufika bibi hayupo babu anaumwa mbayaa, piga yowe na wewe hamna hata mtu anakuja! Majirani wanamiangalia kama picha ya Yesu ukutani, nikajikokota mpaka hospital babu akapata nafuu akanipa mkanda mzima wa kifo cha bibi mzaa mama na kifo cha mama
Nililia mpaka.madokta wakanilaza, kuamka naambiwa babu amekufa tayar, uuuwi nikaliAaaaaa mpaka nikalazwa tena kuamka nikaambiwa nikamzike babu, nikaenda kumzika kichina china, nikarudi nyumbani kwa mama
Nampigia simu baba hapatikani, nikaamua kufunga safari kwa bibi mzaa baba nakuta watu wamejaaaa, eh naambiwa baba amefariki jana usiku! Uuuuwi nilihisi dunia imeniandama, how?! Nikalia hamna hata alienishikilia wala.kunisikiliza! Wananipita kama mavi, kweli jina langu la Yoorèn walikosea sa a kuniita! Nikalia wee pale nikanyamaza na kurudi home mwenyewd ivi unajua hakuna mtu aliyejigusa kunisemesha?! Kunishika, kunibembeleza kila mwanakijiji ananipita pembeni, nikarudi home kwa mama nikalala, ndani siku 5, nikaanza kusaka nyumba, saka saka na wewe, saka saka nikakutana na nguo za mama, boxi la chuma (safe box) na biatu na album za picha zetu, nikawa naangalia nacheka, nalia, nacheka, dah siamini kwanini Mungu kawaondpa jamaa, uuuwi jamaaa kufiwa kubaya, nimefiwa mara 4 kwa mpigoooo, inaumaaa

Baadae naskia hodiii! Kufungua mkuu wa kijiji kaja kupiga mnada nyumba ya maza na babu na bibi, so natakiwa kupisha njia, chukua kila ulichonacho ondoka, wakaipiga nyumba mnada n
a kila kitu alichokuwa nacho mama walipe madeni ambayo mama alikuwa nayo, nikaondoka na nguo za mama na boxi la chuma na album zangu za picha ya mama, nikakimbia kile kijiji nikaingia Shangai, nikarent hotel, nikalala wiki nzima, baada ya wiki nikapigiwa simu, toka Birmingham kuwa matokeo yametoka nimefaulu sana na kuna watu wanataka kuniajiri, nikaenda bank nikachukua zile hela, nikarudi UK, kufika ikasaini kuanza kazi na Delloitte company UK kama tax analyst! Hapo ndipo nilianza maisha yangu mimi Yoorèn nikiamini mama na babu na baba wapo na mimi kwa kila hatua!

ITAENDELEA SAA 1 USIKU

Saaa moja kml uje tena dada yetu maana kanavutia kweli haka kastory
 
FUK~MI:

XITANG!
Kama napaona! Kha kile kijiji sikipendi, naskia pameendelea eti, to hell! Sipataki hata kupaona na wale wanakijiji naskia wengi waneshakufa, ila watoto wao bado wapo, bora mama yangu aliondokaga huko maana sio kwa ushenzi waliotufanyia

Mama yangu alikuwa anauza bar, analala bar, nyumba yake ndio bar, walevi wakilewa anawafukuza, mama yangu alikuwa mrembo sana, sana hakuna kijiji kizima hakuna, wale mabwashee walijaribu sana kumtaka anawakataa

Alipendanaga na mtoto wa mwenyekiti wa kijiji, zamani mtoto wa mwenyekiti wa kijiji ilikuwa deal sio kitoto, mama yangu kwao walikuwa maskini wa kufa, ila alikuwa mrembo hakuna mfano, wakapendanaaaa na huyo mtoto wa tajiri, mama wa mtoto wa tajiri hakupenda akawatenganisha kea kumpeleka kusoma nje, mama yangu alivyoambiwa wakapanga waonane chini ya mchungwa, ndio kupigana mabreka mtoto wa mkuu wa kijiji akasepa! Baada ya mwezi mama anamsaidia mama yake kuuza genge akaanza kutapika, tapika na wewe hospital moja, kufika ana mimba ya mwezi mmoja, mama alipigwaaaa pigwaaa kuanzia hospital mpaka home akaona isiwe shida, babu yangu akamtetea akakaa pale mpaka akajifungua ndio nikazaliwa mie Yoorèn!

Hilo jina hata usitake kujua maanake, ina maana ni mkojo! Yani me nikaitwa mkojo na mamangu kweli ina sound jaman au dharau hizi?!
Nilipofikisha miaka 10 mama akaondoka kwa wazazi wake, akawa anaishi kwake anauza bar, mie nikaanza shule shuti kutaniwa jamaa, yooorèn yooorèn, shule ikawa chungu mpaka namaliza chekechea, doh! Nimechokaa!
Nikaanza darasa la 1, mambo ni hivyo hivyo mpaka darasa la 5, akarufi yule bwana aliempa mamangu mimba, nikapelekwa kuwa mie ndo ile product ya love waliofanyaga kwenye mchungwa! Mama mkwe wa mama yangu akawaka, hataki kuniona, ila baba yangu alinifurahia kweli, akawa anakuja bar ananiona kwa siri ananiachia hela, ananibembeleza ananiambia me ni msichana mreeembo sana wala nisikasirike hamna mrembo hapo kijijini zaidi yangu, nikifika shule wakinitania nawaambia me ni msichana mreeembo sana kuliko wote duniani wanashangaa, nikawa mtemi ghafla, nina confidence, datasa la.7 likaisha, nikawa k
mkubwaaa, nimeshakuwa mdadaa mreeembooo, shape ya kichinaaa! Mzuuuriii, baba yangu akanipeleka private schools bila bibi kujua, nikapiga shule, nakuwa wakwanza kila siku, nikamaliza form 6, nikapata scholarship kwenda UK, University of Birmingham, nikamuacha mama ingawa roho yangu ilikataa sana, nikaenda kwa ubishi kuwa baba atamwangalia mama, nikapiga 1st yr, 2nd, 3rd, mitihani ikaisha, nikaja kuitwa na head of school, kwenda kuambiwa mama yangu amekufa! Nililiaaaaaaa sikuelewa kwanini, nikaambiwa nirudi kuzika mama, kurudi nilikuwa na mtu wa mochwari na baba yangu, hamna cha mwana kijiji wala wale wanaokunywaga kwa maza pale bar, tukazika kichina china baada ya siku 3 akaja mtu ameshikilia sanduku, kumbe ni lawyer, akasema kuwa kuna mirathi iliachwa pale na mama, ambayo ni nyumba na pesa kidogo, kuangalia pesa kumbe ni dola 10,000 skuelewa mama alizitoa wapi ni pombe tu au?! Tukaangaliana na baba hatukuelewa nikamwuliza baba we ndo umefanya haya akasema hapana! Basi nikafanya yangu nikasaini zangu makaratasi nikaelekezwa shekeli zilipo tukasepa na baba mpaka eneo la tukio nikasaini nikaambiwa unataka zibaki benki au uchukue nikasema zibaki bank tukarudi home
Baada ya siku 3 ya tanga nikamwuliza baba kitu gani kimemwua maza, alipoanza kunielezea gari nje ikaingia, bibi mzaa baba akaja, baba akanibusu kwenye paji la uso akiahidi kuwa atarudi kunielezea, akaondoka, nikafunga milango yoote nikakimbia mpaka kwa bibi na babu
Kufika bibi hayupo babu anaumwa mbayaa, piga yowe na wewe hamna hata mtu anakuja! Majirani wanamiangalia kama picha ya Yesu ukutani, nikajikokota mpaka hospital babu akapata nafuu akanipa mkanda mzima wa kifo cha bibi mzaa mama na kifo cha mama
Nililia mpaka.madokta wakanilaza, kuamka naambiwa babu amekufa tayar, uuuwi nikaliAaaaaa mpaka nikalazwa tena kuamka nikaambiwa nikamzike babu, nikaenda kumzika kichina china, nikarudi nyumbani kwa mama
Nampigia simu baba hapatikani, nikaamua kufunga safari kwa bibi mzaa baba nakuta watu wamejaaaa, eh naambiwa baba amefariki jana usiku! Uuuuwi nilihisi dunia imeniandama, how?! Nikalia hamna hata alienishikilia wala.kunisikiliza! Wananipita kama mavi, kweli jina langu la Yoorèn walikosea sa a kuniita! Nikalia wee pale nikanyamaza na kurudi home mwenyewd ivi unajua hakuna mtu aliyejigusa kunisemesha?! Kunishika, kunibembeleza kila mwanakijiji ananipita pembeni, nikarudi home kwa mama nikalala, ndani siku 5, nikaanza kusaka nyumba, saka saka na wewe, saka saka nikakutana na nguo za mama, boxi la chuma (safe box) na viatu na album za picha zetu, nikawa naangalia nacheka, nalia, nacheka, dah siamini kwanini Mungu kawaondoa jamaa, uuuwi jamaaa kufiwa kubaya, nimefiwa mara 4 kwa mpigoooo, inaumaaa

Baadae naskia hodiii! Kufungua mkuu wa kijiji kaja kupiga mnada nyumba ya maza na babu na bibi, so natakiwa kupisha njia, chukua kila ulichonacho ondoka, wakaipiga nyumba mnada na kila kitu alichokuwa nacho mama walipe madeni ambayo mama alikuwa nayo, nikaondoka na nguo za mama na boxi la chuma na album zangu za picha ya mama, nikakimbia kile kijiji nikaingia Shangai, nikarent hotel, nikalala wiki nzima, baada ya wiki nikapigiwa simu, toka Birmingham kuwa matokeo yametoka nimefaulu sana na kuna watu wanataka kuniajiri, nikaenda bank nikachukua zile hela, nikarudi UK, kufika nikasaini kuanza kazi na Delloitte company UK kama tax analyst! Hapo ndipo nilianza maisha yangu mimi Yoorèn nikiamini mama na babu na baba wapo na mimi kwa kila hatua!
Ilikuwa ni christmass 2013 kwenda 2014



ITAENDELEA SAA 1 USIKU


Hi na ile mbona tofauti lkn zote nzuri
 
1st CLASS BEYAAACH:

Kwakweli poleni Beige na Fu~Mi. Poleni sana,
Am no angel either ( me sio malaika pia) lakini maisha yangu sio ya kudanganya!
Me nimezaliwa na kijiko cha silver mdomoni, mama yangu alikuwa balozi nchini Canada, Baba alikuwa Mfanya biashara mzuri tu, kwetu tumezaliwa 3, me ndo msichana pekee wengine wote wanaume. Kwetu me wa mwisho kaka zangu wamenitangulia so nilikuwa protected always na kaka zangu, nilipeeeendwa yani me na baba yangu tumeivaaa. Kuanzia Nursery mpaka Chuo nimesoma Canada, nilizaliwa Bongo nilipofika mwaka Mama akahamishiwa Canada, life yangu ni kama ya akina Prince William, Charles, sijui shida, what is shida?! Eh?! Me sijisifii

Ninekuja kusoma Nursery expensive schools, nakaa expensive streets, houses, hotels, 1st class flights, 1st class saloons, parties, music, books yani harry potter haijatoka mtaani me nasoma manual script! Nyie mnakuja kucheki harry potter me naongelea movie zingine!

Nikamaliza shule nikaingia chuo,nikapiga business nikamaliza BBA, nika fall inlove na fashion, nikaomba nipelekwe kwenye fashion industry, nakutana na akina Naomi campbell, Tyra Banks, eh! Nyie mpaka mje kuwaskia me nime~hang nao sanaaa tuu! Nikaanzisha clothing line yangu nikiwa canada, mzee aka weka pesa yake pale, nikafaulu nguo zikatemaaa, nikapata karibia dola laki 5, kaka zangu wakaniona me wa ukweli,
Kakangu wa kwanza daktai Canada, ni Neuro~surgeon, ana mke na watoto 3, kakangu wa pili ni Financial Analyst, alianza kufanya kazi HSBC BANK baadae akapata IMF baadae akahamia World Bank. Ameoa ana watoto mapacha 2 wote wakike na kiume mmoja

Yani kwetu shida hamnaga! Au niseme kulikuwa hamnagaaa, mzee wangu na ma connection yake ya business yupo mbaaalii, tunaonana jioni kwa dinner table tuu, me sikubahatika kuolewa nilijiona mdogo sanaa, nikawa natafuta hela nanunua ma hisa Canada na Marekani na UK, kiukweli me ni raia wa Tz lakini nimekulia Canada tz siijui saaaana maana nimeondoka na mwaka
Nikaamua kwenda kusoma Master ya MBA, univeristy of Toronto, nikamaliza nikaendeleza bness yangu ya fashion lakini nikawiwa sana kuja Africa kujifunza fashion hizi za vitengee sijui nini, mwaka wa 2013 mwishoni kwenda 2014.
Nikateremka kwa mrembo wa France, bibie Nanawax, tukaongea biashara ya kutengeneza vitenge, nikamwuzia idea akaikubali, akawa model mwenyewe me nika pinch in some money (invinsible investor) akafanya vizuri sana, nikawa nawatuma wazungu wanakuja ku cut design and stuff! Mpaka sasa NANAWAX sidhani kama ana mpinzani, kwakweli namshukuru Mungu me maisha ya shida shida hata siyajui nawasikia nyie na inanifanya nizidi kumshukuru sana Mungu kwa jinsi alivyonipendelea

Wenzake wakaangaliana tu kweli Mungu aache kututania!

Akaendelea na ubuyu, maisha yakaja kunipiga au sijui nilikosea wapi, me sikuwahi kuwa na boyfriend wala nini, buzy na maisha tuu so mpaka umri wa miaka 26 nikawa bado bikra

Wenzake wakasema tobaaa! Enhe!?

Sasa siku moja nipo zangubkwenye ndege (1st class) naja zangu na maza Tz, aliitwa huku bwana, tukaingia Tz tukafikia hotelini The Kilimanjaro Hotel, tumekaa mpaka alipopata nyumba Oysterbay! Tukahamia Oysterbay, tukakaa me na biashata zangu kwenye ipad! Siku moja maza yupo ofsini nikasema niende kutembea Mbudya! Kama nilikosea sijui nilipatia, nikalipanda boti pale sea cliff, kufika mbudya watoto wa kibongo kibao na much know zao ushuzi mtupu me nawaangalia nawadharaaaau nimejikalia na kichupi na sidiria na bake kwa jua! Nimeoiga sun googles zangu kama kawaida yangu, na kajuice kadogo kamekaa hapo pembeni mara namwona mnyamwezi amesimama mbele yangu, nikamwangalia kwenye miwani akahisi nimelala! Kumbe namwona akaja akanisalimia sikumjibu
Hi;
Me: kimya
Mnyamwezi: naitwa Wonder!
Me: kimya
Akaenda akachukua kiti cha plastic akaja akajiongelesha weeee
Me: kimyaaa!
Akaongea wee me hata sikumsikiliza nawaza biashara zangu wenzake wakaja wakamchukua akaondoka, nikarudi zangu home baadae
J2 naenda church hapo st.peters nimekaa kwenye ibada naskiliza preachings mara namwona kasimama kwa pembeni ananiangalia, nikajikausha, saa ta kutoka akaja kunisalimia
Oh samahani nakufananisha!
Me: nikafungua gari nikaingia
Na yeye akaingia
Nikamkata jicho, kwa maana shuka you disgusting maniac!
Akaniuliza ivi wewe ni bubu?! Sikumjibu
Akaniambia, dada me nakupenda naomba unielewe, nataka hata dk 20 na wewe
Nikawasha gari vuuuum mpaka sea cliff, nikapaki pale spurs nikaingia kula akanifuata, nikaagiza na yeye akaagiza. Nikala nikakaribia kumaliza akaniambia dada me nakupenda, nataka kuwa mpenzi wako, sikumjibu!
Akaendelea kuongea weeeeee, nikalipia chakula nikainuka kwenda toilet kurudi namkuta, nikanyanyua kila kilicho changu nikaondoka akanifuata, nafungua mlango yupo nyuma yangu, nikaingia ndani ya gari akanishika kwa nguvu akanichum, chum chum chum na wewe me nimeukaza mdomo kama mamba, yeye anajaribu kuutoa ulimi auingize kwangu me nimebana mdomo
Akachoka akaacha business card yake kwenye gari yangu akaondoka me nikawasha gari huyoo wetu njia nzima najifuta mamate yake,

Ikabidi nipaki tu pembeni ninawe usi na mdomo nikafika nyumbani nikaogaaa bonge la bath, najisugua mwili mzima huku nalaani, shenzi kabisa hawa majambazi ana bahati sijamwitia polisi, nikaenda kwenye gari nkaichukua ile bness card akaitupa kwenye dustbin nikaendelea zangu na biashara zangu za online na blogs!

Baada ya wiki 1 akaja nyumbani mdogowake na maza, tukamkaribisha katoka huko kijijini, akapewa chumba akalala lakini ma mdogo huyu hakosi kung'ang'ania kukaa chumbani kwangu, sijui alikuwa na nini na mimi, roho yangu ilimkataa kabisaa, nikawa simpendi siku nyingine nikitoka sirudi, nalala hotelini hata wiki namwambia nimesafiri, nikirudi namkuta kahamia chumbani kwangu yani kero mtindo m1, jamani sitakaa nimsahau yule mama mdogo nikakuta amevurugua chumba changu, kapuliza perfume zooote, kachukua nguo yani so classless
Nikamsemea kwa dadake(mama yangu) akasema basi nitaongea nae and shit, akaenda ongea nae kesho akaaga anarudi kijijini, me nikaendelea na maisha yangu siku nimekaa napanga nguo naona nguo moja siioni, ni top yangu nilikuwa naipenda sana naivaaga usiku siku ya alhamisi, mh siioni, uliza maids hamna kitu, uliza kwa mama hamba nikajua tu moja kwa moja kuwa mamdogo kachukua nikaenda kumweleza mama (dadake)
Dadake kusikia akanikalisha chini kunieleza, kuwa yule mdogowake anapenda kwenda kwa mganga sanaaa, na hajui wala haelewi kwanini alumkaribisha
Mmiaka ya nyuma, alishawahi kumkaribisha akamkuta amelala na mumewe (baba yake) akapataga mimba, nikakasirika sana hata kabla wewe haujazaliwa (mama ananihadithia sasa)
Mtoto akazaliwa me nikadai talaka kwa mume nimenuna kweli kweli, baadae nikamweleza bibi yako alikuwa bado yupo hai akaweka kikao tukasuluhishana nikasamehe ndio kupata kazi kuwa balozi, tuka reconcile na babako hapaa pita pita za hapa na pale nikapata mimba yako

Sasa mama yako mdogo yule mtoto Mungu alivyo wa huruma siku unazaliwa ndio siku mwanae aligongwa na gari akafa, sikuweza kuhudhuria msiba kabisaa, kwasababu ya uzazi na wewe ulipofika mwaka 1, nikapata promotion kazini nikaondoka kwenda Canada. Sasa kama amechukua nguo yako basi kuna kitu, tukafunga safari mpaka kwa Pastor wa kilokole, yakapigwa maombi weeeee tukarudi home
Baafa ya siku 3 tunapigiwa simu kuwa mama mdogo anaumwa sana mahututi kalala kitandani hajiwezi
Mama na mie tukafunga safari mpaka mbeya
Tunatia mguu kwa bibi watu wanalia, Mama mdogo amekufa sasa hivi yani kama mnapishana nae mlangoni, mama akalia pale me hata sijui misiba ndo nini, tukakaa msiba ukaisha wakazika tukasubiri tanga likavunjwa mama akasema tukae mpaka 40 nimechukua likizo, tukamaliza 40 mbeya ni sawa na kumaliza 40 kuzimu, pabayaaa, basi natambulishwa pale kwa watu wajomba na nini, siku haziendi! No connection na Tz yenu no internet basi nikaona nacheleeewa kweli kweli! Siku 1 bibi akaniita akaniambia jinsi gani mama mdogo alivyoumwa nika connect na yale maombi niliofanyiwa ndio siku aliumwa nikajua mamdogo kuna kitu wakati naongea na bibi kuangalia pembeni naona ile nguo yangu kudadeki, nikamwuliza bibi hii top vepee akaniambia nilipewa zawadi na mamako mdogo, nikauchuna chunu! Siku ya kuondoka nikamwambia bibi hii nguo itupe tu usiivae, hakujua kwanini akamwita kijana wa ng'ombe akamwambia akaitupe. Kijana na tamaa zake akaenda kumpe girlfriend wake, beibe kuivaa akafa siku hio hio hawakuelewa! Wakajua labda kifo cha ghafla, nikajua ile nguo iliwekewa kitu kibaya sana, nikaondoka Mbeya nikiwa salama rohoni, bibi hakuivaa tena ile top na mimi sikuichukua, lakini njia nzima nikawa namuwaza Mr Wonder sikujua kwanini!



ITAENDELEA SAA 3 USIKU

Usizingue basi...yaani usikose
 



HOT MOMMA:

Dah poleni sana warembo, me kama mnavyojua nimeolewa nikiwa nimepigikaa weee na kupigika namaanisha nimekitembeza weeeee mpaka kuja kuangukia kwa huyu jibaba, nilichachooooka na kuzurura kama mbwa koko wa kike!

Mimi bwana kwetu dar, yani nikisema kwetu daaaaaar namaanisha, me mtoto wa temekeee, kwa TMK, mnalala saa 8 usiku mnaamka saa 3 asbh chai saa 5 asbh lunch saa 10 jioni dinner saa 3 usiku!
Yani maisha flani ashlomo mageni, maisha ya kingese usitamani kuyaishi, ituachie sisi tu, mambo ya mdundiko mtaa wa 3, mambo ya msuto kwa jirani, mambo ya vigodorooo, mambo ya akina taarab, hadija kopa, yani kule ndo kule, TMK, eh! Nyie niacheni, akaanza kulia wakambembeleza pale marafkizake! Akawa sawa akaendelea kufunguka

Shule nursery nimesoma nyumbani kwa mwl mkoja ivi alikuwa anafundisha olympio, enzi izo olympio hot cake, ung'eng'e kibao, tunaenda shuleni akirudi yeye jioni saa 11 kusoma nursery, basi nikamaliza nursery naishi na mama na baba, kwetu tumezaliwa madada 3, dadangu wa kwanza anaishi mwanza kwa mumewe aliolewa akiwa mdoogo wa miaka 20, wa pili anakaa Arusha anasoma chuo cha diploma, na mie ndo mziwanda mwenyewe kama mnavyoniona, nimekoleeeea rangi ya mtume, mweupe pee! Wananiitaga accidental child walijua wazazi wameshamaliza kuzaa mie nikaja ndo maana wao wameshaolewa na mwingine yupo chuo mwaka wa 3 mie ndo nursery!

Sina hili wala lile siku naamka mama akaumwa, ghafla baba akakimbiza hapo mwananyamala hospital, mama akatundikiwa drip wakaona hapa parefu transfer muhimbili
Akina dada wakaja baada ya siku 1, kumsabahi bu mkubwa, tumekaa pale bu mkubwa katangulia mbele ya haki
Msiba msibani sie watoto wa kiislam hailali kama wakristu! Tukazika baada ya siku 1, hapo makaburi ya kinondoni, tukarudi home TMK, kusikilizia gawiwo la nguo sijui, nikapewa nguo ya mama na picha zake tulipiga wote na mama na baba, dada zangu wakachukua nguo zingine za mama na viatu na mapochi ah me mdogo najua nini ndio kwanza nikaambiwa na dada mkubwa nakuwekea nakuwekea
Tukabakia na baba pale, dada mkubwa akaona isiwe shida, ngoja nimchukue doko tukaishi nae mwanza baba hawezi kaa na mtoto wa kike nikapelekwa mwanza bwana!
Kufika nikaanza kusoma shule za ukweli, naishi kule kwa matajiri Kepree, napelekwa shule za ukweli nikaambiwa nirudie nursery, nikarudia maana nilikuwa naakili sana nilianza shule nina miaka 2, ndani ya miaka 2 nursey yetu ya TMK nikawa nimeshaua! Nikarudia nursery mwaka m1 nikiwa na miaka 6 nikaanza primary 1 english medium
Mume wa dadangu alinipenda kama mwanae, nikawa naenda shuleni na wanae wengine wadogo, wakanichukulia kama mwanao lakini me najua kuwa mie sio mtoto ni shemeji wa mume wa dadangu!
Tumeenda wee nikafaulu darasa la 4, nikaingia la 7 nikafaulu sana nikapata scholarship kwenda kusoma arusha, dadangu wa mwanza akakataa akasema nije kwanza dar kumsalimia baba, nikaja dar nimekuwa mkuubwa baba anashangaa, nikaishi pale TMK sipapendi papo ovyo naongea english wale madogo tuliokuwa tunasomaga nao nursery ya jioni nawaona wamekuua wenyewe wanaringa wanaimba nyimbo za uswazi! Ah me nikawa nakaa ndani kama mwali, likizo ikaisha baba akasema nisome dar! Dada akakataa akasema natakiwa kukaa karibu nae kwasababu ndo kwaanza nakua, nikarudi tena mwanza kuendelea na form 1 pale pale, piga form2 fumua wastan A, piga form 4 nina div 1, piga form 5 nikasema nije kusoma Dar kwasababu nimeshakuwa mtu mzima!
Nikaja dondoka hapo Mzizima High school, mtoto wa TMK lakini nawakimbizaje watoto wa mzizima?! PCB mtoto form 6 nimetoka na div 1.4 mzee hakuamini maana sio kwa purukushani zile za madaladala ya kwenda temeke, unayapandika kariakoo kulee shule ya uhuru kule kwa mbele, ni sheedah pale fire hapatoshi sikuelewa nilipataje ile 1 nilihisi kama mama yangu alikuwa nyuma yangu ananisimamia.
Mzee akafurahi na akina dada wakafurahi, nikaulizwa unataka kwenda kusoma wapi nikasema Mlimani, nikadondoka mlimani BCOM
Nikawatandika mwaka wa kwanza wapili watatu nikafaulu na 1st class, sikuwa na muda wa ku date kabisaa nilitamani nimalize shule nimtoe baba yangu temeke, nikaja kupata kazi Buzz (kwa sasa mnaiita Tigo) mshahara wa kwanza laki 5, kiru!
Nikapata nyumba kijitonyama nikamtoa baba oale akawa anaishi kijitonyama, kule TMK tukapangisha nyumba mzee anachukua kodi anajipoza.
Nikajitahidi kazini nikapandishwa mshahara mpaka mil 1 net salary. Nikanunua kiwanja ndani ya mwaka 1, nikaanza kujenga tegetaa ndani ndani hapo nimenunua kiwanja kwa mkopo wa mil 7. Nikasimamisha ukuta mzee wangu akawa anasimakia ujenzi nikawa sina presha, kazi zinaenda sina hili wala lile nawaza nyumba iishe baba ahamie kule tuishi wote!
Baada ya miaka 3 nyumba ya vyumba 3 ikaisha, tukahama kijitonyama tukahamia tegeta, kwetu hata kama kuna foleni lakini kwetu, baba akapata amani na furaha kila siku ubarikiwe ubarikiwe nikawa nabarikiwa kweli, visafari vya hapa na pale mikoani huku nalipwa per DM. Nakuja kumgawia baba pasu kwa pasu, nikanunua gari rav 4, baba akawa analiendesha mie nakuja ofsini na bajaj.

Baada ya mwaka nikanunua nami gari yangu Extrail, nikampa baba mimi nikaendesha Rav 4 ya zamani basi tu apate amani. Mzee wangu kila siku Mungu akubariki Mungu akubariki
Buzz wakaondoka wakaja watu wengine nikahamia Vodacom. Nikapiga mzigo pale na akina Mwamvita Makamba wee, nikawekwa kwenye mambo ya marketing, nilete clients, nikaiba wateja wote wa buzz nikawaleta vodacom.. nikapandishwa cheo kwenda SA ikawa kama kwenda chooni, mzee wangu nae yupo vzuri lakini akawa mpweke sana basi skuingine nikisafirishwa namsafirisha na yeye aje tu ilimradi asibakie mpweke akawa anafurahi nikampeleka english kozi akawa anajua Yes No kidogo kidogo maisha yakaenda

Sikumoja akaniita mwanae. Anauliza kama nimepata mchumba. Nikamwambia hata sina, kwanza wa nini me naweza kujihangaikia mwenyewe. Mzee akaguna ikabidi aniweke sawa. Akanipiga na swali 1 la uchungu sana inamaana me sitaona wajukuu kutoka kwako?! Nikaumia roho sana nikamwambia baba niombee tu, wanaume waongo sana, ila naamini utawaona wajukuu very soon miaka 2 mbali basi namtia moyo tu akafurahi akaniombea tukalala.

Wiki ikapita ofisini akaja mzungu bwana toka Italy, kuniona akashoboka ananitaka, nikamkubalia kwa juu juu kumbe ana maanisha! Akanikaribisha Moven Pick kiofisi me nikaenda, kufika hamna cha ofisi wala nini ananitaka, nikamshushua nikamwambia we si umeoa jamaa?! Akaniambia wala sijaoa! Mh! me sijui hili wala lile nikasema labda maombi ya mzee home yametiki. Nikamkubalia usiku huo wala sikurudi home! Tukalala hapo hapo ndio bikra yangu kuchomolewa kudadeki nikiwa na miaka 26! Kuamka asbh mzungu kasepa, nikaoga na kujikusanya kucheki simu missed calls 20 na sms 10 toka kwa baba, nikampigia simu nililala kwa rafkiangu akaguna, kukata simu naangalia midamu kama nipo leba! Kweli mzungu kafanya yake, nikajikusanya nikaingia ofsini, saa 3 asbh aibuu, nikasema nilimpeleka mzee hospital wakaamini nimevaa nguo za jana, mzungu simwoni, bdae namwulizia naambiwa alishaondoka kwenda kwao nikalaani, hakuna mfano, nimeporwa bikra uuuwi nilichanganyikiwa nikaomba na likizo ghafla ya siku 5, nikarudi hotelini nikalia weeeee mpaka uchungu ulivyoisha hapo saa 10 jioni, nikifkiria na foleni la tegeta bora nipige tu simu nilale pale. Nikamcheki mshure akanielewa nikalala Movenpick.
Usiku nashuka restaurant nakula mara naona mkaka anakuja ananisemesha
Hii seat ina mtu nikamjibu hapana
Akajisogeza akakaa, akawa anajiongelesha me kimya nina morn bikra yangu! Mh yeye anaongea na mtu anbae haeleweki, kuja kushtuka ananiwekea business card katikati ya maziwa yangu anaondoka.
Me nikamwangalia sikummaliza nikasonya mxiiiiuuuuu, nikamwita waiter kumlipa akaniambia ushalipiwa na yule kaka aliekaa hapa nikashangaa nikapanda juu nikalala na ile bness card sikuitoa pale kifuani

ITAENDELEA SAA 4 NANUSU USIKU

Mweeeee....tamthilia
 
Kwakweli kama kuombewa nimeombewa sana tu, hakuna mtu anaetoa sadaka kama mimi, sijui 1st fruit (malimbuko), sijui zaka (thithe) hata siibi, sadaka za kila j2 nipo, michango ya kanisani na ahidi ikifika siku ya tukio kulipa sina hata sumni, basi Mungu ananiona ananisamehe, nikaacha mchezo wa kuahidi kanisani. Maana sina chanzo cha kuniingizia pesa mjini!

Mtu mwenye Master's ya ukweli awezi kufanya hii kitu; yaani, kudanganya.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom