dont trust any 1
JF-Expert Member
- Jun 30, 2015
- 251
- 203
Saaa moja kml uje tena dada yetu maana kanavutia kweli haka kastoryFUK~MI:
XITANG!
Kama napaona! Kha kile kijiji sikipendi, naskia pameendelea eti, to hell! Sipataki hata kupaona na wale wanakijiji naskia wengi waneshakufa, ila watoto wao bado wapo, bora mama yangu aliondokaga huko maana sio kwa ushenzi waliotufanyia
Mama yangu alikuwa anauza bar, analala bar, nyumba yake ndio bar, walevi wakilewa anawafukuza, mama yangu alikuwa mrembo sana, sana hakuna kijiji kizima hakuna, wale mabwashee walijaribu sana kumtaka anawakataa
Alipendanaga na mtoto wa mwenyekiti wa kijiji, zamani mtoto wa mwenyekiti wa kijiji ilikuwa deal sio kitoto, mama yangu kwao walikuwa maskini wa kufa, ila alikuwa mrembo hakuna mfano, wakapendanaaaa na huyo mtoto wa tajiri, mama wa mtoto wa tajiri hakupenda akawatenganisha kea kumpeleka kusoma nje, mama yangu alivyoambiwa wakapanga waonane chini ya mchungwa, ndio kupigana mabreka mtoto wa mkuu wa kijiji akasepa! Baada ya mwezi mama anamsaidia mama yake kuuza genge akaanza kutapika, tapika na wewe hospital moja, kufika ana mimba ya mwezi mmoja, mama alipigwaaaa pigwaaa kuanzia hospital mpaka home akaona isiwe shida, babu yangu akamtetea akakaa pale mpaka akajifungua ndio nikazaliwa mie Yoorèn!
Hilo jina hata usitake kujua maanake, ina maana ni mkojo! Yani me nikaitwa mkojo na mamangu kweli ina sound jaman au dharau hizi?!
Nilipofikisha miaka 10 mama akaondoka kwa wazazi wake, akawa anaishi kwake anauza bar, mie nikaanza shule shuti kutaniwa jamaa, yooorèn yooorèn, shule ikawa chungu mpaka namaliza chekechea, doh! Nimechokaa!
Nikaanza darasa la 1, mambo ni hivyo hivyo mpaka darasa la 5, akarufi yule bwana aliempa mamangu mimba, nikapelekwa kuwa mie ndo ile product ya love waliofanyaga kwenye mchungwa! Mama mkwe wa mama yangu akawaka, hataki kuniona, ila baba yangu alinifurahia kweli, akawa anakuja bar ananiona kwa siri ananiachia hela, ananibembeleza ananiambia me ni msichana mreeembo sana wala nisikasirike hamna mrembo hapo kijijini zaidi yangu, nikifika shule wakinitania nawaambia me ni msichana mreeembo sana kuliko wote duniani wanashangaa, nikawa mtemi ghafla, nina confidence, datasa la.7 likaisha, nikawa k
mkubwaaa, nimeshakuwa mdadaa mreeembooo, shape ya kichinaaa! Mzuuuriii, baba yangu akanipeleka private schools bila bibi kujua, nikapiga shule, nakuwa wakwanza kila siku, nikamaliza form 6, nikapata scholarship kwenda UK, University of Birmingham, nikamuacha mama ingawa roho yangu ilikataa sana, nikaenda kwa ubishi kuwa baba atamwangalia mama, nikapiga 1st yr, 2nd, 3rd, mitihani ikaisha, nikaja kuitwa na head of school, kwenda kuambiwa mama yangu amekufa! Nililiaaaaaaa sikuelewa kwanini, nikaambiwa nirudi kuzika mama, kurudi nilikuwa na mtu wa mochwari na baba yangu, hamna cha mwana kijiji wala wale wanaokunywaga kwa maza pale bar, tukazika kichina china baada ya siku 3 akaja mtu ameshikilia sanduku, kumbe ni lawyer, akasema kuwa kuna mirathi iliachwa pale na mama, ambayo ni nyumba na pesa kidogo, kuangalia pesa kumbe ni dola 10,000 skuelewa mama alizitoa wapi ni pombe tu au?! Tukaangaliana na baba hatukuelewa nikamwuliza baba we ndo umefanya haya akasema hapana! Basi nikafanya yangu nikasaini zangu makaratasi nikaelekezwa shekeli zilipo tukasepa na baba mpaka eneo la tukio nikasaini nikaambiwa unataka zibaki benki au uchukue nikasema zibaki bank tukarudi home
Baada ya siku 3 ya tanga nikamwuliza baba kitu gani kimemwua maza, alipoanza kunielezea gari nje ikaingia, bibi mzaa baba akaja, baba akanibusu kwenye paji la uso akiahidi kuwa atarudi kunielezea, akaondoka, nikafunga milango yoote nikakimbia mpaka kwa bibi na babu
Kufika bibi hayupo babu anaumwa mbayaa, piga yowe na wewe hamna hata mtu anakuja! Majirani wanamiangalia kama picha ya Yesu ukutani, nikajikokota mpaka hospital babu akapata nafuu akanipa mkanda mzima wa kifo cha bibi mzaa mama na kifo cha mama
Nililia mpaka.madokta wakanilaza, kuamka naambiwa babu amekufa tayar, uuuwi nikaliAaaaaa mpaka nikalazwa tena kuamka nikaambiwa nikamzike babu, nikaenda kumzika kichina china, nikarudi nyumbani kwa mama
Nampigia simu baba hapatikani, nikaamua kufunga safari kwa bibi mzaa baba nakuta watu wamejaaaa, eh naambiwa baba amefariki jana usiku! Uuuuwi nilihisi dunia imeniandama, how?! Nikalia hamna hata alienishikilia wala.kunisikiliza! Wananipita kama mavi, kweli jina langu la Yoorèn walikosea sa a kuniita! Nikalia wee pale nikanyamaza na kurudi home mwenyewd ivi unajua hakuna mtu aliyejigusa kunisemesha?! Kunishika, kunibembeleza kila mwanakijiji ananipita pembeni, nikarudi home kwa mama nikalala, ndani siku 5, nikaanza kusaka nyumba, saka saka na wewe, saka saka nikakutana na nguo za mama, boxi la chuma (safe box) na biatu na album za picha zetu, nikawa naangalia nacheka, nalia, nacheka, dah siamini kwanini Mungu kawaondpa jamaa, uuuwi jamaaa kufiwa kubaya, nimefiwa mara 4 kwa mpigoooo, inaumaaa
Baadae naskia hodiii! Kufungua mkuu wa kijiji kaja kupiga mnada nyumba ya maza na babu na bibi, so natakiwa kupisha njia, chukua kila ulichonacho ondoka, wakaipiga nyumba mnada na kila kitu alichokuwa nacho mama walipe madeni ambayo mama alikuwa nayo, nikaondoka na nguo za mama na boxi la chuma na album zangu za picha ya mama, nikakimbia kile kijiji nikaingia Shangai, nikarent hotel, nikalala wiki nzima, baada ya wiki nikapigiwa simu, toka Birmingham kuwa matokeo yametoka nimefaulu sana na kuna watu wanataka kuniajiri, nikaenda bank nikachukua zile hela, nikarudi UK, kufika ikasaini kuanza kazi na Delloitte company UK kama tax analyst! Hapo ndipo nilianza maisha yangu mimi Yoorèn nikiamini mama na babu na baba wapo na mimi kwa kila hatua!
ITAENDELEA SAA 1 USIKU