Live updates: Tanzania vs zimbabwe

Live updates: Tanzania vs zimbabwe

Hv tz tukimfunga Zimbabwe tunapita magroup au kuna match nyingine .


Kuna Sudan ana wasubiri na Msumbiji! Mshindi wa mechi ya zimbabwe na tz anakutana na mshindi kati ya sudan na msumbiji ambayo msumbiji kashinda 5 leo!
 
Tumechemka sana hili lazima tuseme na tunalalamika ivi kwa kuwa tunaipenda nchi yetu na timu yetu ila timu yetu ipate mechi angalau moja na nchi ambayo kiwango chake kinalingana na zimbabwe kushinda leo goli moja bado timu n nyepesi sana angalia msumbiji kashinda ngapi jaman tuondoke hapa tulipo mawazo yahame sasa tusibakie hapahapa tuu hii n timu yetu sote.

Mwalimu ana mda nfupi sana apate mechi angalau hata mbili za maana kabla hatujaenda zimbabwe
 
Miaka nenda rudi visingizio vile vile, tunaikalia politiki tu, huwezi kupanda bangi ukavuna mchicha.

Miaka ile wakati wa mtifuano wa FAT ileee, Jenerali Ulimwengu akiwa mwenyekiti wa BMT, alitoa wazo tujitoe kwenye haya mashindano angalau kwa miaka mitatu, tutengeneze timu za watoto za taifa na vilabu vikiwamo vilabu vikubwa navyo vijipange kuwa na timu za watoto na vijana, baadaye tushiriki mashindano ya vilabu na timu ya taifa, lakini wahafidhina wa yanga na simba walikataa katu katu. Ni kama muongo mmoja umepita sasa lakini mambo ni yale yale, akili ile ile, kuku wa kienyeji unataka leo asipekue pekue akitaka kula mtama?!

Tutakalia politiki tu, bila kuwekeza, uwekwezaji uchwara tutaendelea kuwa kichwa cha mwendawazimu tu, kila mwenye 'akili' anakuja kujipigia kipara.

Leo hata waliokuwa vibonde wetu Burundi tunapigana vikumbo kupapatikia wachezaji wao? Na wanatupiga dozi kisawa sawa kama wendawazimu!

Siasa za soka kwenye magazeti, usimba na uyanga wala hazitatupeleka kokote kule.

Tutaendelea kuwa 'wahindi' wa soka kwenye ukanda huu na Afrika kwa ujumla.
 
Mkuu mpunga mm nataman kuwa na mdahalo wa kitaifa kuhusu mpira wetu hasa timu yetu ya taifa star napanga kuja kukusannya pm za wana jf hapa ili kuishinikiza tff iandae hili tumeshapotea ila tunaweza kujipanga tuende mbele maana hadithi n ile ile tuu hakuna jipya
 
Mkuu mpunga mm nataman kuwa na mdahalo wa kitaifa kuhusu mpira wetu hasa timu yetu ya taifa star napanga kuja kukusannya pm za wana jf hapa ili kuishinikiza tff iandae hili tumeshapotea ila tunaweza kujipanga tuende mbele maana hadithi n ile ile tuu hakuna jipya

Naunga mkono hoja yake. Uzuri wake Raisi wa TFF ni member hapa.
 
Mkuu Malinzi, with due respect, tumekuwa "positive" tangu 1961! What do we have to show for all this time? Hata mimi niko pessimistic kidogo!

Again, with due respect, unaonaje mkiliangalia upya suala la sisi kung'ang'ania Uanachama wa "Shirikisho la Wachovu" (CECAFA), kuna sababu gani inayotuzuia sisi kujiunga na COSAFA ambako kuna ushindani zaidi? Hebu fikiria tukutane kila mwaka na A. Kusini, Zimbabwe, Malawi, Zambia, Botswana, angola, Malawi, Swaziland, n.k? Ninaamini tukihamia huko, baada ya vichapo kadhaa, tutapiga hatua kuliko kila mwaka kukutana na Timu kama Somalia, Eritrea, Burundi, n.k.

Kama ni vigumu sisi kujitoa CECAFA, basi angalau tuombe kualikwa mara moja moja. Kiwango cha Timu za COSAFA kiko juu kuliko cha CECAFA. Tunahitaji ushindani huo. Ninaamini wenzetu wa Nchi Jirani wangekuwa hapa kwetu ki-Jiografia wangekuwa tayari washatosa CECAFA kama walivyofanya Zambia, tena kwa manufaa makubwa baada ya Miaka kadhaa.

Ni mawazo yangu tu Mkuu! Asante!

Naheshimu na kukubaliana na mawazo yako kwa kiasi fulani japo naona kujitoa CECAFA ni kwa sasa ni uamuzi usio wa lazima. Kanuni ya mpira ni maandalizi ya mchezaji, timu na miundombinu. Bado sisi hatuna maandalizi ya kutosha ya muda mrefu, ndio maana hata hapahapa CECAFA bado sisi sio big brother. Timu yetu haitishi. Ingekuwa tunatisha CECAFA, labda ningekubaliana na wewe tujitoe sasa na kutafuta ushindani zaidi.

Angalia Ngoromgor heroes, ni timu nzuri sana licha ya kufungwa na Nigeria iliyotwaa ubingwa wa dunia mwaka jana. Timu hii inapaswa kuendelezwa kwa kucheza mechi nyingi dhidi ya timu kubwa kama Nigeria, Ghana, Misri n.k. Hebu tuigeuze timu hii iwe ndio timu ya taifa miaka 3-4 ijayo baada ya kupitia mafunzo ya kina na mechi nyingi za majaribio.

B ila kuwa na maandalizi ya namna hii tutaendelea kulaumiana milele
 
Back
Top Bottom