MCHONGANISHI
JF-Expert Member
- May 28, 2011
- 372
- 364
Leo kuna mkutano wa hadhara wa CHADEMA mkoa wa Shinyanga katika viwanja vya mahakama nguzo 8 Majengo. Mgeni rasmi ni mwenyekiti wa CHADEMA Taifa mh. Freeman Mbowe.
Sasa tunasubiri mkutano uanze huku tukiburudishwa na gwaride la Red Brigade.
----------------------------
View attachment 103240
---------------------
Sasa tunasubiri mkutano uanze huku tukiburudishwa na gwaride la Red Brigade.
Wakuu.
Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Kamanda Freeman Mbowe, akiongozana na viongozi kutoka makao makuu pamoja na wabunge wa Kanda ya Ziwa Mashariki, punde wanaelekea kwenda kuhutubia mkutano mkubwa wa hadhara mjini Shinyanga, eneo la Nguzo nane, Mahakama ya Mwanzo, ni baada ya kikao cha ndani kilichomalizika muda mfupi uliopita.
Ni sehemu ya mikakati ya kuimarisha kanda hiyo ambayo ni kati ya ngome kubwa za CHADEMA.
UPDATES:
»• Meshack Opulukwa: kama kuna mikoa inaombea na ina hamu kubwa uchaguzi mkuu ufike haraka wafanye mabadiliko makubwa kuiondoa CCM ni Shinyanga na Simiyu. Wananchi wameshachoka na kushindwa kwa CCM!
• Chombo chochote kikitumika sana kinaingia uchakavu. CCM imeshaingia uchakavu, haiwezi tena kutumika kuleta ukombozi wa maendeleo. Kwa kauli ya Pinda maana yake ni kwamba mihimili 3 haina maana kwa serikali ya CCM. Anasema chama cha magamba, chama cha wezi kimeamua kuwateketeza na kuwatelekeza wakulima wa pamba. Haiwezi tena kuwatetea. Kazi hiyo inafanza na CHADEMA, waiunge mkono.
» • Heche: mkutano mkubwa kama huu, CCM wanatumia miezi 2 kuuandaa kwa kusomba watu kutoka maeneo mbalimbali. Anazungumzia simcard tax. Anasema sasa maskini kabisa wa Tanzania atatozwa sawasawa na tajiri mkubwa kabisa wa Tanzania.
• Kwa mwaka atalipa sh. 12,000, kiasi kikubwa kuliko wakati wa kodi ya kichwa iliyoanza kufutwa Hai na Karatu, kwa sababu ya uongozi wa CHADEMA maeneo hayo kisha ikafuata nchi nzima.
• Majuzi baada ya wabunge wenu wa CHADEMA, kwenda Arusha kuomboleza na kuzika, watu wa CCM kwanza hawakujali, wakaendelea na shughuli, tofauti kbs na kawaida ya bunge, kisha wakapitisha hiyo kodi! Ndiyo maana kila siku nawaambia watanzania wenzangu, tushukuru kuwepo kwa CHADEMA na viongozi wake makini, la sivyo Watanzania wote tutauzwa!
»• Sasa kapanda Mwenyekiti. Anazungumzia kwanza, anawapatia hongera wale wote walioko kwenye mfungo wa ramadhan wakitekeleza moja ya nguzo muhimu za imani yao. Anaelezea tukio la Arusha na matukio yote yaliyotokea uchaguzi wa kata 26
Updates combination chini ya Tumaini Makene itawajuza.
----------------------------
View attachment 103240
---------------------
![]()
![]()
![]()
![]()
![]()
Kwa hisani ya mpiga picha Pukudu na Tumaini Makene Shinyanga huko.