Listi yangu ya Kuepusha Tanzania na Balaa,vikwazo,Je List Yako wewe nani?

DSN

JF-Expert Member
Feb 2, 2011
2,837
1,674


Nimetafakari sana na kuona tunahitaji kikosi kazi kitakacho mshauri Rais jinsi ya kulivusha Taifa,katika kipindi hiki kinachohitaji busara kubwa sana.kwani Siku za nyuma Watanzania walipopita kwenye kipindi kama hiki Baba wa Taifa kwa uwezo binafsi [Personal or individual skills] kama ni Mchezo wa mpira wa mguu ni kiwango cha mchezaji mmoja kuwa na uwezo mahiri wa kucheza zaidi ya wenzie katika timu, mfano wake ni kama Pelle,Maradona na zama za kina JJ Okocha, na Ronaldo de Lima,kwa kiwango cha sasa tunasema Messi.

Lakini kuna ubishi unaendelea kuwa Ronardo De Lima ni mzuri zaidi ya Messi kwa zama ma enzi zake.Kwa hilo mimi nakubaliana nao wote wanaokubali Ronaldo ni mzima kwenye mchezo wa soka kwenye zama zake, kuliko Messi wa sasa kwa kulingana na mazingira na nyakati zetu za sasa,kulinganisha na mazingira ya Ronaldo ya zama hizo.Uwezo wa Ronaldo kucheza na mabeki wenye misuri mizito duniani wakati huo nabado akaweza kupenya na kutikisa nyavu basi ni mcheza bora zaidi ya kiwango cha Messi cha sasa.Vivyo hivyo katika siasa za nyumbani Tanzania Mwalimu kwa zama zake,ukilinganisha na watawala wetu wa sasa kiwango cha Mwalimu kwa Taifa hili ni sawa na Pelle japo wapo wakina Messi wa leo katika siasa za sasa.Na Messi amezaliwa akakua na kujua kuwa hata acheze vipi bado hatomfikia Pelle mfalme wa Soka.

Kwenye siasa zetu hapa nyumbani tunaitaji wakina Ronaldo kuhimili mikiki ya misuko suko kulingana na zama na nyakati tulizo nazo kwa sasa.Na kulivusha Taifa kama Mwalimu alivyoweza kupitia hatihati hizo nabado akalivusha Taifa toka kwenye majaribu hayo.Hivyo nakubali Mwalimu kwa zama hizo na alikua na kiwango cha juu wakati huo cha kuwavusha Watanzania katika kuelewa siasa na maswala mazima ya maendeleo yao kama Taifa,ukilinganisha na zama hizi tulizo nazo [Pelle v/s Messy].


Maamuzi ya kitaifa na kimataifa mara nyingi yanahitaji mwamuzi, awe na busara na uthubutu wa kuweza kufanya dhidi ya hilo atakalo kufanya au kuamua hatima yake.

Nimejifunza vitu fulani vizuri sana kuusiana na Rais wa 35 [Rais wa Marekani mwaka 1961-1963], Mr John Fitzgerald Kennedy [JFK].Nimepata kuona sinema [Movie] ya Kennedy na ndugu yake Robert Francis ''Bobby'' kennedy [RFK]. Kupitia sinema hiyo nilijifunza na kuona ni jinsi gani kiongozi akisukumwa kufanya maamuzi magumu na mazito kwa Taifa kwa kasi na umakini mkubwa sana, na bado akafanya kazi hiyo kwa uamakini huo.

Kupitia kikosi kazi,[Taski Force] chake wakati huo wa vita baridi [Cold War] Viongozi wengi wa kijeshi na Serikali walikuwa wakitaka Marekani ingie vitani, kutokana na chokochoko za vita baridi kati ya USSR na Marekani ikiwemo na Cuba.Lakini kupitia JFK na Bobby ,wamarekani hawakuingia vitani na ukawa ndio mwisho wa vita baridi na hivyo,kuwa mtu muhimu sana kwa bidii binafsi aliepusha dunia kuingia kwenye vita ya TATU YA DUNIA.Hiyo yote pamoja na mapungufu yake kama binadamu katika kupenda wakina mama Warembo kama alivyodondoka kwa mcheza sinema maarufu na mrembo wa wakati huo Marilyn Monroe.Lakini bado alibaki kuwa kiongozi wa kupigiwa mfano kwa maamuzi binafsi ya kielevu na uthubutu [Intellecutal and Braveness decisions].

Aikuishi hapo Rais wa 42 [Mwaka 1993-2001] Taifa hilo Kubwa Duniani Mr William Jefferson ''Bill" Clinton nae kama waliomtangulia akafuata nyayo kwa kuwa na maamuzi yaleyale ya busara na welevu mkubwa kiasi kuhufanya uchumi wa Taifa hilo kuwa mkubwa sana Dunia na kuongeza umaarufu wa Taifa ilo kufahamika sana Duniani kote kama Super Nation,nae pamoja na hayo bado akabaki kuwa binadamu asiekamilka na kupata doa dogo la kupenda wanawake warembo kama vile Monica Samille Lewinsky.

Kwa sasa wataalamu wanaendelea kufanya utafiti kuona kuna uhusiano gani ,kwa watu aina hiyo wenye uwezo mkubwa wa kutoa majibu yanayotatiza jamii kitaifa na kidunia, wanakuwa na ugonjwa wa kupenda wakina mama warembo [JFK v/s Monroe na Bill v/s Monica] .Bado wanaendelea kwa kuwa utafiti ni kitu endelevu uenda siku moja watatwambia majibu sahihi ya utafiti wao juu ya watu hawa wenye uelevu na uthubutu [Intellectual and Braveness] inakuwaje wanakuwa na kaugonjwa haka kakupenda wakina dada warembo.

Nikilejea kwenye hoja halisi kama ningepewa nafasi nani amsaidie Rais wetu kwa ushauri wa kupata mambo ya msingi yawe Dila [Vision] kutuvusha,ningependa kumuomba Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Jakaya Mrisho Kikwete,kuunda kikosi kazi [Task Force] ya kutuvusha kutoka kwenye misukosuko ya kitaifa,kikosi kazi hicho kitachompa ushauri wa nini kifanyike ili tuvuke.Kuna mambo mengi ya msingi yamelizongo Taifa na yanahitaji majibu na maamuzi makali na yenye uthubutu,kama alivyosema swahiba wake Edward Lowasa.


Kama ningepata fursa hiyo timu yangu ya kumshauri Rais wetu katika mambo ya msingi ambayo Taifa linataka majibu,Panel kama kikosi kazi cha ushauri bila kujali chama,itikadi ya kisiasa,dini ili kulitoa Taifa katika kipindi hiki kigumu,kilichogubikwa na wingu la sintofahamu nyingi.Na maamuzi yatakayopatikana hapo yamuongoze Rais katika kutoa mwafaka wa majibu jamii inayoyategeme ili kulivuka daraja hilo.

KIKOSI KAZI [TASK FORCE]
1: Waheshimiwa Marais wote wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania
A: Mhe: Ali Hassan Mwinyi
B: Benjamini William Mkapa

2: Marais wote wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar
3: Mjane wa Baba wa Taifa

4: Mawaziri Wakuu Wafuatao
A: Salim Mohamed Salim
B: Judge: Joseph Sinde Warioba|
C: David Cleopa Msuya
D: John Marecela

5: Wakuu wa Jeshi na Wanadhimu Wakuu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania [JWTZ],waliopo Madarakani na Wastaafu.

6: Wakurugenzi wa Usalama wa Taifa [DG] wastaafu na walioko madarakani.

7: Viongozi wa Kisiasa
A: DK Wilbrod Slaa
B: Maalim Seif Sharif Hamad
C: Pro Ibrahim Lipumba
D: DK Wilson Mukama
E: Mchungaji Mtikila
F: Freeman Mbowe

8: Viongozi wa Kidini
A: Kaldinali Polycarp Pengo na katibu wake Tanzania Episcopal Conference [TEC]
B: Sheikhy Issa Shaban Simba na Katibu wake wa BAKWATA
C: Mkuu wa Jumuiya ya Wakristo na Katibu wa Jumuiya hiyo Christian Council of Tanzania [CCT] na Katibu wa Jumuiya hii.
D: Mkuu wa Kanisa la Kiinjiri la Kilutheri la Tanzania Askofu DK Alex Malasusa
E: Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana la Tanzania Mchungaji Mokiwa
F: Askofu wa Kanisa la Wasabato Mchungaji Joshua Kahula.
G: Mkuu wa Kanisa la Assemblies of God Dk Barnabas
H:Wazee wa Jadi [Nikimaanisha wazee wa kimila toka pande zote za Tanzania ]
I: Viongozi wa madhhebu ya Hindu na bohara.

9: Wanataaluma kada muhimu.
A: Prof Issa Shivji [Sheria na Katiba UDSM]]
B: Xavier Lwetama [UDSM]
C: Renatus Mkinga [Dar es
D: Pro Baregu [Mwanza]
E: Wakuu wa Vyuo vya UMMA,kama [UDSM,DODOMA,IFM,CBE,MZUMBE n,k]
F: Tindu Lissu [Sheria na Mambo ya Mikataba]
G: ZitoKabwe [Elimu na Changamoto kwa vijana wa sasa]
H: Viongozi Mwenyekiti na katibu wa Jumuiya ya Serikali za ya wanafunzi wa vyuo Elimu ya juu na chuo kikuu.

10: Viongozi wa Serikali ni kama ifuatavyo
A:John Pombe Magufuri [Waziri]
B: Samweli Sitta [Waziri]
C: DK Harrison George Mwakyembe [Naibu Waziri]
E: Anna Tibaijuka. [Waziri].

11: Taasisi
A: Mkurugenzi wa Takukuru Mr Edward Hosea
B: Mkurugenzi wa Mtandao wa Jinsia Nchini [TNGP ] Usu Mallya
C: Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake [TAMWA]
D: Katibu mfuko wa Mwalimu Nyerere foundation.[Joseph Butiku]
E: Mkurugenzi wa HAKI ELIMU Tanzania.

12: Wazee waliotukuka katika utumishi wa umma ndani ya Serikali na nje ya Serikali
A: Peter Kisumo
B: Sir George Kahama
C: Judge Mark Bomani
D: Edwin Mtei
E: Reginald Mengi


 
Nakubaliana na mawazo yako kwa kiasi kikubwa. Wengi ya watu uliowataja ni muhimu kwa kila mtanzania anayejali zaidi ya tumbo na mafanikio binafsi. Hujamtaja Lowasa. Sijui ni maksudi au bahati mbaya lakini nahisi angestahili kuingia pia. Watu kama Prof. Paramagamba Kabudi wangefaa sana.
Hofu yangu ni kwamba ukiunda task force kubwa sana sometimes inaishia kuwa kama kundi la wabunge wa CCM. Utashangaa mwisho wa siku una watu wa kushabikia mambo pasipo kutafakari.
 
Nakubaliana na mawazo yako kwa kiasi kikubwa. Wengi ya watu uliowataja ni muhimu kwa kila mtanzania anayejali zaidi ya tumbo na mafanikio binafsi. Hujamtaja Lowasa. Sijui ni maksudi au bahati mbaya lakini nahisi angestahili kuingia pia. Watu kama Prof. Paramagamba Kabudi wangefaa sana.
Hofu yangu ni kwamba ukiunda task force kubwa sana sometimes inaishia kuwa kama kundi la wabunge wa CCM. Utashangaa mwisho wa siku una watu wa kushabikia mambo pasipo kutafakari.

Kweli kundi kubwa linaweza kuwa kikwazo lakini pia ukizingatia vigezo nilivyotumika si rahisi kwa kundi hili kutumika.Wamarekani wameweza kuwa strong nation kwa kuwa wanavitu kama hivi na wanatumia msuguano wa hoja mahususi kuibuka na jibu sahihi [conflict of interest ] kutoka kwenye kada tofauti.

Timu hiyo ukiangalia kuna watu waliotumikia Taifa kwa moyo wa dhati,na wana moyo mkubwa wa kujua UTU ni nini.Hivyo basi moral nayo imetumika kupata candidate wasiotiliwa shaka
 
Mimi nimependa hiyo story ya Kina JFK na mdogo wake Boby Kennedy, nimeipenda coz mie pia ni mmoja ya watu ambao nimekuwa nikifatilia na kustudy siasa za marekani.. Siasa za bongo na maamuzi ya viongozi wetu huwa ni usanii sana!
 
DSN nafikiri umepotea kidogo.
KATIBA MPYA NDIO SULUHU YA MATATIZO YA NCHI HII.

Ndio katiba ndio suluhu,lakini utafikaje pasipo kuwa na timu makini ya kuamua ni nia zipi zitatufikisha hapo.Kwa sasa kuna mambo kibao tunaitaji majibu yake ili tusonge mbele.
1: Katiba Mpya
2: Wajibu wa viongozi kulitumika Taifa na sio wachumia tumbo
3: Ufisadi [EPA,Richmond n,k]
4: Migomo isiyoisha kumbuka wadogo nao wanakopi wakiona ndio njia sahihi ya kudai haki [Yaitaji usikivu wa Serikali]
6: Maisha Magumu baadaya kuwa na Maisha bora
7: Ukosefu wa Ajira
8: Ukosefu wa uvumilivu wa kisiasa [Watendaji wa Serikali kuamini mtu asipoiunga CCM mkono huyo aitakii mema Tanzania]
9: Uchoyo,wivu,uongo, majungu na unafiki imekua ni utamaduni wa Watanzania
10: Ulafi uliotawaliwa na uchu wa mali [Rushwa]
11: Matatizo ya Umeme umeludisha nyuma maendeleo ya Taifa na kudumaza ustawi wa wanajamii.
12: Kushuka kwa elimu,na elimu ndio msingi wa nguvu kazi kupata maarifa
13: Wizi uliokithiri wa Mali ya UMMA na dhidi ya wanajamii.
14: Ukosefu wa Maadili ya Taifa
15: Uthibiti wa wanajamii kwa kusimamia imani zisizo kubalika kwenye jamii, hivyo kuongezeka kwa imani chafu za kishirikina na kuongeza hofu kwa wanajamii hivyoo kupelekea udumazo wa jamii kimaendeleo. [Hii ni kazi inayowahusu wazee wa Jadi,kuwa na nguvu ya kudhibiti uchafu huo ili kuondoa hofu inayotolewa na baadhi ya watu kwa wenzao]
16: Tishio la kutoweka kwa Amani
17: Misuguano ya mpasuko wa muungano wa Tanzania na Zanzibar
18: Kukosekana kwa Uzalendo
19: Taifa kuwa na Dila Vision za muda mrefu na fupi.
20: Mikataba ya wawekezaji wa sekta muhimu,madini,maliasili nk.[Swala zima la ubinafsishaji]
21: Utawala bora
22: Itikadi ya Taifa [Sio itikadi ya vyama vya siasa]
23: Uwezeshaji wa sekta binafsi hasa wa kimachini,yaani jua kali
24: Support dhidi ya Kilimo ambacho ndio uti wa mgongo
25: Miundo Mbinu
Na mengine mengi kuyataja
 
Mimi nimependa hiyo story ya Kina JFK na mdogo wake Boby Kennedy, nimeipenda coz mie pia ni mmoja ya watu ambao nimekuwa nikifatilia na kustudy siasa za marekani.. Siasa za bongo na maamuzi ya viongozi wetu huwa ni usanii sana!


Najiuliza viongozi wetu wanasoma kweli vitabu na kuangalia sinema au documentary kujifunza,watu wengine walifanikiwa vipi kufika hapo.ukitembelea facebook page ya Obama utakuta moja ya vitu obama alivyonavyo ni makusanyo ya hotuba na maandishi ya Abraham Lincoln [Father of the Nation].Yote hiyo ni kukusanya ujuzi na maarifa.

Baba wa Taifa Taifa alikuwa msomaji mzuri sana wa vitabu vya kada mbalimbali hasa filosofia [Philosophy] ambayo ndio taaluma yake ilipo lala.Na kweli maarifa ya uongozi mengi aliyapata uko.
 
Maraisi wa Tanzania wanapokua kwenye wakati mgumu huwa wanakimbilia kwa wazee wa Dar es salaam. Si unakumbuka JK badala ya kukutana na wafanyakazi kujibu hoja ya mishahara yeye alikimbilia kuongea na wazee wa Dar es salaam? Nilidhani atawapa wazee hao majibu ya malipo yao ya iliyokua EAC lakini wapi?

Kuunda task force kama hiyo kwa CCM ni kitendawili aisee, tabia ya wabunge wa CCM tena waliochaguliwa na wanannchi tunaziona bungeni sembuse hiyo Task force ya kuteuliwa?
 
Nimetafakari sana na kuona tunahitaji kikosi kazi kitakacho mshauri Rais jinsi ya kulivusha Taifa,katika kipindi hiki kinachohitaji busara kubwa sana.kwani Siku za nyuma Watanzania walipopita kwenye kipindi kama hiki Baba wa Taifa kwa uwezo binafsi [Personal or individual skills] kama ni Mchezo wa mpira wa mguu ni kiwango cha mchezaji mmoja kuwa na uwezo mahiri wa kucheza zaidi ya wenzie katika timu, mfano wake ni kama Pelle,Maradona na zama za kina JJ Okocha, na Ronaldo de Lima,kwa kiwango cha sasa tunasema Messi.

Lakini kuna ubishi unaendelea kuwa Ronardo De Lima ni mzuri zaidi ya Messi kwa zama ma enzi zake.Kwa hilo mimi nakubaliana nao wote wanaokubali Ronaldo ni mzima kwenye mchezo wa soka kwenye zama zake, kuliko Messi wa sasa kwa kulingana na mazingira na nyakati zetu za sasa,kulinganisha na mazingira ya Ronaldo ya zama hizo.Uwezo wa Ronaldo kucheza na mabeki wenye misuri mizito duniani wakati huo nabado akaweza kupenya na kutikisa nyavu basi ni mcheza bora zaidi ya kiwango cha Messi cha sasa.Vivyo hivyo katika siasa za nyumbani Tanzania Mwalimu kwa zama zake,ukilinganisha na watawala wetu wa sasa kiwango cha Mwalimu kwa Taifa hili ni sawa na Pelle japo wapo wakina Messi wa leo katika siasa za sasa.Na Messi amezaliwa akakua na kujua kuwa hata acheze vipi bado hatomfikia Pelle mfalme wa Soka.

Kwenye siasa zetu hapa nyumbani tunaitaji wakina Ronaldo kuhimili mikiki ya misuko suko kulingana na zama na nyakati tulizo nazo kwa sasa.Na kulivusha Taifa kama Mwalimu alivyoweza kupitia hatihati hizo nabado akalivusha Taifa toka kwenye majaribu hayo.Hivyo nakubali Mwalimu kwa zama hizo na alikua na kiwango cha juu wakati huo cha kuwavusha Watanzania katika kuelewa siasa na maswala mazima ya maendeleo yao kama Taifa,ukilinganisha na zama hizi tulizo nazo [Pelle v/s Messy].

Maamuzi ya kitaifa na kimataifa mara nyingi yanahitaji mwamuzi, awe na busara na uthubutu wa kuweza kufanya dhidi ya hilo atakalo kufanya au kuamua hatima yake.

Nimejifunza vitu fulani vizuri sana kuusiana na Rais wa 35 [Rais wa Marekani mwaka 1961-1963], Mr John Fitzgerald Kennedy [JFK].Nimepata kuona sinema [Movie] ya Kennedy na ndugu yake Robert Francis ''Bobby'' kennedy [RFK]. Kupitia sinema hiyo nilijifunza na kuona ni jinsi gani kiongozi akisukumwa kufanya maamuzi magumu na mazito kwa Taifa kwa kasi na umakini mkubwa sana, na bado akafanya kazi hiyo kwa uamakini huo.

Kupitia kikosi kazi,[Taski Force] chake wakati huo wa vita baridi [Cold War] Viongozi wengi wa kijeshi na Serikali walikuwa wakitaka Marekani ingie vitani, kutokana na chokochoko za vita baridi kati ya USSR na Marekani ikiwemo na Cuba.Lakini kupitia JFK na Bobby ,wamarekani hawakuingia vitani na ukawa ndio mwisho wa vita baridi na hivyo,kuwa mtu muhimu sana kwa bidii binafsi aliepusha dunia kuingia kwenye vita ya TATU YA DUNIA.Hiyo yote pamoja na mapungufu yake kama binadamu katika kupenda wakina mama Warembo kama alivyodondoka kwa mcheza sinema maarufu na mrembo wa wakati huo Marilyn Monroe.Lakini bado alibaki kuwa kiongozi wa kupigiwa mfano kwa maamuzi binafsi ya kielevu na uthubutu [Intellecutal and Braveness decisions].

Aikuishi hapo Rais wa 42 [Mwaka 1993-2001] Taifa hilo Kubwa Duniani Mr William Jefferson ''Bill" Clinton nae kama waliomtangulia akafuata nyayo kwa kuwa na maamuzi yaleyale ya busara na welevu mkubwa kiasi kuhufanya uchumi wa Taifa hilo kuwa mkubwa sana Dunia na kuongeza umaarufu wa Taifa ilo kufahamika sana Duniani kote kama Super Nation,nae pamoja na hayo bado akabaki kuwa binadamu asiekamilka na kupata doa dogo la kupenda wanawake warembo kama vile Monica Samille Lewinsky.

Kwa sasa wataalamu wanaendelea kufanya utafiti kuona kuna uhusiano gani ,kwa watu aina hiyo wenye uwezo mkubwa wa kutoa majibu yanayotatiza jamii kitaifa na kidunia, wanakuwa na ugonjwa wa kupenda wakina mama warembo [JFK v/s Monroe na Bill v/s Monica] .Bado wanaendelea kwa kuwa utafiti ni kitu endelevu uenda siku moja watatwambia majibu sahihi ya utafiti wao juu ya watu hawa wenye uelevu na uthubutu [Intellectual and Braveness] inakuwaje wanakuwa na kaugonjwa haka kakupenda wakina dada warembo.

Nikilejea kwenye hoja halisi kama ningepewa nafasi nani amsaidie Rais wetu kwa ushauri wa kupata mambo ya msingi yawe Dila [Vision] kutuvusha,ningependa kumuomba Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Jakaya Mrisho Kikwete,kuunda kikosi kazi [Task Force] ya kutuvusha kutoka kwenye misukosuko ya kitaifa,kikosi kazi hicho kitachompa ushauri wa nini kifanyike ili tuvuke.Kuna mambo mengi ya msingi yamelizongo Taifa na yanahitaji majibu na maamuzi makali na yenye uthubutu,kama alivyosema swahiba wake Edward Lowasa.


Kama ningepata fursa hiyo timu yangu ya kumshauri Rais wetu katika mambo ya msingi ambayo Taifa linataka majibu,Panel kama kikosi kazi cha ushauri bila kujali chama,itikadi ya kisiasa,dini ili kulitoa Taifa katika kipindi hiki kigumu,kilichogubikwa na wingu la sintofahamu nyingi.Na maamuzi yatakayopatikana hapo yamuongoze Rais katika kutoa mwafaka wa majibu jamii inayoyategeme ili kulivuka daraja hilo.

KIKOSI KAZI [TASK FORCE]
1: Waheshimiwa Marais wote wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania
A: Mhe: Ali Hassan Mwinyi
B: Benjamini William Mkapa
2: Marais wote wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar
3: Mjane wa Baba wa Taifa

4: Mawaziri Wakuu Wafuatao
A: Salim Mohamed Salim
B: Judge: Joseph Sinde Warioba|
C: David Cleopa Msuya
D: John Marecela

5: Wakuu wa Jeshi na Wanadhimu Wakuu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania [JWTZ],waliopo Madarakani na Wastaafu.

6: Wakurugenzi wa Usalama wa Taifa [DG] wastaafu na walioko madarakani.

7: Viongozi wa Kisiasa
A: DK Wilbrod Slaa
B: Maalim Seif Sharif Hamad
C: Pro Ibrahim Lipumba
D: DK Wilson Mukama
E: Mchungaji Mtikila
F: Freeman Mbowe

8: Viongozi wa Kidini
A: Kaldinali Polycarp Pengo na katibu wake Tanzania Episcopal Conference [TEC]
B: Sheikhy Issa Shaban Simba na Katibu wake wa BAKWATA
C: Mkuu wa Jumuiya ya Wakristo na Katibu wa Jumuiya hiyo Christian Council of Tanzania [CCT] na Katibu wa Jumuiya hii.
D: Mkuu wa Kanisa la Kiinjiri la Kilutheri la Tanzania Askofu DK Alex Malasusa
E: Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana la Tanzania Mchungaji Mokiwa
F: Askofu wa Kanisa la Wasabato Mchungaji Joshua Kahula.
G: Mkuu wa Kanisa la Assemblies of God Dk Barnabas
H:Wazee wa Jadi [Nikimaanisha wazee wa kimila toka pande zote za Tanzania ]
I: Viongozi wa madhhebu ya Hindu na bohara.

9: Wanataaluma kada muhimu.
A: Prof Issa Shivji [Sheria na Katiba UDSM]]
B: Xavier Lwetama [UDSM]
C: Renatus Mkinga [Dar es
D: Pro Baregu [Mwanza]
E: Wakuu wa Vyuo vya UMMA,kama [UDSM,DODOMA,IFM,CBE,MZUMBE n,k]
F: Tindu Lissu [Sheria na Mambo ya Mikataba]
G: ZitoKabwe [Elimu na Changamoto kwa vijana wa sasa]
H: Viongozi Mwenyekiti na katibu wa Jumuiya ya Serikali za ya wanafunzi wa vyuo Elimu ya juu na chuo kikuu.

10: Viongozi wa Serikali ni kama ifuatavyo
A:John Pombe Magufuri [Waziri]
B: Samweli Sitta [Waziri]
C: DK Harrison George Mwakyembe [Naibu Waziri]
E: Anna Tibaijuka. [Waziri].

11: Taasisi
A: Mkurugenzi wa Takukuru Mr Edward Hosea
B: Mkurugenzi wa Mtandao wa Jinsia Nchini [TNGP ] Usu Mallya
C: Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake [TAMWA]
D: Katibu mfuko wa Mwalimu Nyerere foundation.[Joseph Butiku]
E: Mkurugenzi wa HAKI ELIMU Tanzania.

12: Wazee waliotukuka katika utumishi wa umma ndani ya Serikali na nje ya Serikali
A: Peter Kisumo
B: Sir George Kahama
C: Judge Mark Bomani
D: Edwin Mtei
E: Reginald Mengi
Angalizo;
Mkapa ni mshauri mzuri sana, ila kwenye mambo ya ubinafsishaji tu au uuzaji wa rasilimali za nchi kwa kutumia kivuli cha serikali!

Viongozi wa dini:
Wangetakiwa kuwa involved kutoka katika kila dini na katika kila dhehebu. Unaanza na wakuu wa dini husika kwanza k.v. Hindu, Uislamu, Ukristo, n.k. halafu unaingia tena katika kila dhehebu unachukua wakuu wa madhehebu wote.

Wakuu wa taasisi za elimu ya juu:
Wanatakiwa kushirikishwa wote bila kujali chuo ni cha Umma, au ni cha binafsi, sababu hata kama chuo ni cha binafsi, manufaa yake ni ya umma, ni kwa ajili ya Tanzania. In actual fact, fixed assets tu pamoja na cash in hand ndiyo zinakuwa za binafsi, the rest ni mali ya umma, including ardhi ambayo wametumia kwa ajli ya kusimika majengo yao.

I like your idea, it is superb!
 
hilo si litakuwa bunge jingine mkuu!

Mkuu hili si Bunge hiki ni kikosi kazi kazi [Task Force] timu hii ni watz kutoka kada tofauti tofauti za kijamii zenye uelewa.kukutna kwao na kukaa pamoj na Rais kuwasikiliza kila mmoja na kisha wote kwa pamoja kukubaliana na Mheshimiwa Rais kuwa Jambo hili kati ya haya ambayo wananchi wanataka majibu yake basi ili ni bora kwa manufaa na faida ya Taifa letu.Kwa kwa kuwa hawa waliotajwa hapa na watu wenye heshiima zao kwenye jamii.Kila mmoja akiwa na uzoefu wa maswala ya jamii toka upande yeye aliopata kuutumikia.

Hiki ni kitu kinachoweza kuchukua wiki moja tu ya mazungumzo,kama tunavyoona summit zinafanyika pakle Dar es Salaam.Ila kwa kuwa ili litakua ni kwa maslahi ya Taifa si vyema likaonyeshwa bali tupate maazimio ya makubaliano katika matatizo ambayo watanzania wanataka majibu yake na kuwa majibu yapatikane on spot kwa yale yanayowezekena na yale yenye kuitaji muda basi yapewe muda na ultimatum yake.
 
Maraisi wa Tanzania wanapokua kwenye wakati mgumu huwa wanakimbilia kwa wazee wa Dar es salaam. Si unakumbuka JK badala ya kukutana na wafanyakazi kujibu hoja ya mishahara yeye alikimbilia kuongea na wazee wa Dar es salaam? Nilidhani atawapa wazee hao majibu ya malipo yao ya iliyokua EAC lakini wapi?

Kuunda task force kama hiyo kwa CCM ni kitendawili aisee, tabia ya wabunge wa CCM tena waliochaguliwa na wanannchi tunaziona bungeni sembuse hiyo Task force ya kuteuliwa?

Task force ile ya wazee wa Dar natumaini ilikuwa ni moja ya vitu vilivyoongeza ufa wa maswali mengi ya kujiuliza.
 
mkuu kwanza tunahitaji utayari wa mkuu wa nchi kwanza kabla ya kuja na Task force. hata ukiwa na task force 200 kama mkuu wa nchi hana utayari ni kazi bure. zipo tume ngapi zilizoundwa kumshauri rais kuhusu mambo mbalimbali kama tume za madini na zote zimetiwa kapuni. Dawa ni kubadilisha katiba ili tuwe na serikali iliyo wazi na yenye kugawanya madarka vizuri ndipo tuje na task force.kwa sasa itakuwa kutumia vibaya kodi za wananchi bure maana ****** ashauriki
 
mkuu kwanza tunahitaji utayari wa mkuu wa nchi kwanza kabla ya kuja na Task force. hata ukiwa na task force 200 kama mkuu wa nchi hana utayari ni kazi bure. zipo tume ngapi zilizoundwa kumshauri rais kuhusu mambo mbalimbali kama tume za madini na zote zimetiwa kapuni. Dawa ni kubadilisha katiba ili tuwe na serikali iliyo wazi na yenye kugawanya madarka vizuri ndipo tuje na task force.kwa sasa itakuwa kutumia vibaya kodi za wananchi bure maana ****** ashauriki

Ni vyema ajue kuwa kama kuna kipindi nchi inahitaji Task Force ni sasa,na kuwa huko ni kuheshimu umma ,ambao yeye anautumikia.Mwalimu yeye kama yeye alikuwa tayari ni task force tosha kwa kuwa tayari aliwafuata aina hiyo ya watu na kuongea nao.

Ukifuatilia hotuba za Mwalimu,ameongea na watu wengi sana,Maaskofu, Masheikh, wachungaji,wanafunzi wa vyuo,wafanyakazi, wakulima, watanzania kwa ujumla na hata mataifa makubwa na madogo.Na kupitia hotuba zake nyingi ambazo si za kuandikwa bali maneneo yanayotoka kichwani kupitia Hints alizozitayarisha kuwa ataongelea niini na nini katika hotuba hiyo.

Wengine wanakwenda mbali kwa kusema Mwalimu alikuwa anaagiza mtu fulani anayemjua yeye aletwe ikulu na kuwa anashida naye.Wanikulu wataingia kumtafuta mtu huyo,ili kumchua watamwambia Mwalimu anakuitaji,wakimfikisha kwake,unajua tena na hofu manake waliotumwa hawakuambiwa anamtakia nini,watamchukua twende Mwalimu anakuhitaji waungwana wengine watamdokeza atajua akifika kwake.Akifika yuko full mahofu vijana wasikuizi wanasema full majotooo.Mwalimu ndio huyo kajaa tele anakusubili protocol imezingatiwa wawili mmebaki mwalimu anasema nimekuita tucheze soro.

Mwenyewe umekuja full majoto presidar ananiita unafika presidar anataka tucheza soro [bao],la kiswahili au la kikabila chako inategemea unatoka kabila gani.Du kama unajua maana ya Bao kwa waliobahatika kuwaona wazee au vijana wanacheza mchezo huo, waheshimu sana hata kama unamadegree yako kama Tuntemeke Sanga, wale wanayo madgree mia ya maisha, kupitia mazungumzo ya mchezo wa bao,japo wanaweza kuwa na elimu ndogo ya dalasani.Kucheza mchezo huo kunataka busara japo vijana wa sasa hawajaambiwa wala kufundishwa umuhimu wa mchezo huo.Kwa wanao jua mchezo wa CHESS,hauna tofauti sana na BAO.Sema CHESS umekuwa na Dunia nzima na pia unatumia akili nyingi zaidi.Kwa kiwango chetu waafrika BAO ndio nafasi yetu kama wazungu na CHESS.Na kwa wazungu kama wewe ni bingwa wa CHESS akika wewe ni kifaa.

Mwalimu anakukaribisha kwenye soro [BAO],na kwa desturi ya bao wakati unacheza linanoga likisindikiziwa na stori kuu zianazoendelea kwenye maisha ya jamii,uku likichombezewa na utani.[utani mwingine ukiwa si mcheza bao unaweza ulushe ngumi,kumbe basi wacheza bao ni majasiri kupita].Kupitia kucheza kwako bao na Mwalimu mtaongea habari nyingi zinazoendele kitaa bila kuingiza siasa katika stairi tulivu yenye kumuacha mtoaji wa habari akipangilia akili yake kucheza na kutoa habari anayozungumzia huku pia anachombezea na utani.Hivyo ndani ya wacheza bao kuna mambo matatu kwenye akili yanayofanya kazi at a go.|
1: Kuendesha Mchezo wenyewe
2: kutoa habari ya matukio ya habari zinazojiri mtaani [yaani maisha ya jamii kwa wakati huo,jamii inazizungumziaje]
3: Kutoa matani au mdhaha wa nia njema ya kukughafilisha wewe mchezaji mwenzie apoteze uwezo wa kupangilia mchezo na kukushinda.

Unapata picha ya uwezo wa Mwalimu katika kukusanya Task Force kwa namna nyingi.Hivyo basi kupitia mchezo wa soro habari mwalimu atakayoipata itakuwa ni sahihi kupitia uwezo wa mtoaji ambae alikuwa anata ndani ya akili yenye kutenda mambo matatu kwa pamoja.Kwa intellecuals hicho ni kipimo kikubwa sana cha uwezo.

Kwa waliopata kupiga story na Rais wa Marekani walikuwa wanastaajabu uwezo wa William "Bill" Clinton kuweza kufanya mambo karibia manne kwa wakati mmoja,nayo ni anasoma gazeti,anasikiliza luninga na anaongea na bado anauwezo huo kutopoteza topic ya mada mnayoongelea japo anaconcentration kwenye mambo matatu hayo kwa mpigo likiwemo la nne kuanalyes hayo matatu yanayaondelea.

Tukikosa hayo basi tuuunde kikosi kazi kituopoe kwenye hicho wataoto wa ubongo wa full ever wanamwambia mtoto wa Prezidar please tell your daddy[Mr President] things are not ok as he think its. Riz 1 report hii usipuuze kitaani noma.
 
Nimekubali kweli watu na uchungu na hii nchi, lakini sijamwona Dr. Wilbroad Sila kwenye hii orodha au nime-misslook.
 
Nimekubali kweli watu na uchungu na hii nchi, lakini sijamwona Dr. Wilbroad Sila kwenye hii orodha au nime-misslook.

Kweli umemiss look ni kiongozi wa kwanza kisiasa,angalia kwenye orodha hapo juu.Manake kisiasa huyo ndio mdau halisi kupitia Protocal baada ya kikwete na uchaguziii wa mwaka huooo.Bila huyo mchanganyiko ninaona mimi binafsi kuwa unastahiki kutuvusha utakuwa sio timilifu kwangu.
 
Back
Top Bottom