Lissu vs Kabudi: Ngoma Inogile...

Mindi

JF-Expert Member
Apr 5, 2008
3,523
4,991
Mastratejisti wa Serikali ya Magufuli watakuwa walifurahi sana na kujipongeza, baada ya hotuba ya kwanza bungeni ya Profesa Palamagamba Kabudi, waziri mpya wa Sheria na Katiba. Nderemo, vifijo, na makofi yaliyokuwa yanapigwa, pamoja na vibwagizo, na wabunge wa CCM siku hiyo, ni ushahidi tosha.

Katika hotuba hiyo, Profesa Kabudi alionekana hatimaye kuja kama mkombozi wa serikali ya CCM kule Bungeni, kutokana na kuwa chini ya utawala wa Tundu Antipas Mughwai Lissu, ambaye alikuwa anawapeleka puta maspika, wenyeviti na wabunge wa CCM kwa ujumla.

Licha ya lugha yake kali, iliwabidi wapokee hoja zake na kutumia ujuzi wake wa sheria. Kumleta naibu spika ambaye ni mahiri wa sheria, Dakta Tulia, inaweza pia kuwa kwa ajili ya kuwadhibiti wapinzani wakiongozwa na Tundu Lissu katika uwanja huu.

Mhariri Mkuu wa Gazeti la Raia Mwema, Godfrey Dilunga, alikuwa na haya ya kusema kuhusu mtanange huu:

Swali la kujiuliza, ataendelea kuachiwa mwanya huu? Katika kutafakari swali hili, kule bungeni sasa kuna Waziri mpya wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi, msomi wa kiwango cha juu, mwepesi katika kumbukumbu za matukio ya kisheria, kisiasa, kijamii na hata kiuchumi, unaweza kusema siri ya uimara wa Lissu katika zama hizi ndio maisha ya kawaida ya kisomi ya Profesa Kabudi (huu ni mjadala mwingine wa siku zijazo).” [ Gazeti Raia Mwema, Toleo la Mei 4, 2017.] Tujadili

1. Kwa maoni yangu, Tundu Lissu ana nafasi kubwa ya kujipambanua na kumwacha kwa mbali Profesa Kabudi, kwa sababu zifuatazo:

2. CV ya Lissu. Pamoja na kwamba kisomi, Profesa Kabudi yuko juu sana zaidi kuliko Lissu katika uwanja wa Sheria, lakini Lissu ana faida ya kuishi yale aliyosoma, kusoma zaidi katika yale anayolazimika kupambana nayo. Karibu maisha yake yote baada ya kuhitimu, ameyatumia katika kupambana na mifumo ya sheria kandamizi na nyonyaji.

Amepambana na makampuni ya madini yanayovuruga mazingira na kubambikiza kesi kwa wananchi “vidomodomo”. Kwa hiyo Lissu ana uzoefu mkubwa sana katika field na ana data nyingi sana kwenye “finger tips” kuliko Profesa Kabudi, ambaye pamoja na kuwa ameshiriki kwa namna moja ama nyingine katika kupambana na mifumo, kama alivyodokeza kwenye hotuba yake Bungeni, wakati anahitimisha mjadala wa wizara yake bungeni 25 April 2017, lakini sehemu kubwa hasa ni katika kushughulika na nadharia katika tafiti na kufundisha darasani.

3. Passion ya Lissu. Hiki ndicho huonekana wazi kila mara Lissu anapokamata maiki. Kwa jinsi anavyoongea, uchaguzi wake wa maneno, tone yake, lugha yake ya mwili, Lissu hurusha ngumi nzito sana kwa wale anaowasema, kiasi kwamba wanakuwa katika wakati mgumu sana wamsikilizapo.

Hurusha makombora mazito sana yenye nguvu. Hii ni kutokana na kwamba toka ameanza kupambana, hajabadilisha kambi wala kubadili msimamo. Anaishi anayoyasema. Hii binafsi huwa inanishangaza sana kwa sababu najua kwamba makampuni ya Madini yana uwezo mkubwa wa kifedha na yamewa “garagaza” wengi waliojaribu kuyapinga, kwa kuwavuta mashati.

Wakati Profesa Kabudi mwanzo alionekana kama mtetezi wa wanyonge na mpinga ukandamizaji, baadaye alionekana “kuvutwa shati”, hasa mwanzoni mwa mijadala ya “Katiba Mpya”. Hapo akawa mtu wa kuisemea serikali, na serikali ikawa inamtumia “kutoa semina kwa wabunge”, ambazo zilioneshwa moja kwa moja na TBC.

Lakini baadaye Tume ya Katiba ya Warioba ilipochezewa rafu na serikali, wakanyang’anywa magari njiani, ambapo akina Polepole walianza kuzunguka nchi nzima wakiiandama serikali na kutetea rasimu ya katiba, Kabudi akageuka na kuwa mwiba kwa serikali. Hivi karibuni amevutwa tena shati na sasa ni mtetezi wa serikali katika mambo ya kisheria.

Kwa maoni yangu, si rahisi Kabudi kuwa na Passion ya kiwango cha Lissu. Anaweza kweli ku-summon passion kwa kiwango fulani, kama ilivyoonekana kwenye hotuba yake Bungeni, kwa kukumbusha aliyofanya miaka ya nyuma sana, lakini si kwa muda mrefu, na si kwa kiwango cha Lissu.

4. Historia. Historia iko upande wa Lissu. Ni kweli kwamba serikali ya CCM imesimamia uundwaji na usainiwaji wa mikataba mibovu kuwahi kutokea katika Historia ya wizi wa madini duniani. Hata Chifu Mangungu katika ujinga wake wote, hafikii rekodi ya CCM. Katika awamu mbalimbali za marais chini ya CCM, uwekezaji katika madini uliasisiwa, baada ya kuwekwa pembeni na Baba wa Taifa, Rais Nyerere. Mkapa ndiye alifungulia mbwa, na kuanzia hapo Tanzania imepigika vibaya sana kwa mfululizo wa mikataba ya wizi wa mchana.

Kuanzia mikataba ya umeme (IPTL, Net Group Solutions, Richmond, Dowans, Aggreko, Songas), mikataba ya madini, mikataba ya Gesi na mafuta, ni nchi inaliwa kulia, kushoto, juu na chini. Achilia mbali Ufisadi kupita Kagoda, na dada yake Meremeta, Rada, Escrow, Loliondo, bila kusahau wizi mkubwa kupitia ukwapuaji wa nyumba za Serikali.

Kwa rekodi kali ya wizi na ufisadi mkubwa wa kiwango hicho, mtu anayesimama kuibeba serikali ya CCM, atahitajika kuwa na ubavu wa pekee kubeba tani zote hizo za kashfa, wizi na ufisadi. Kitu ambacho sidhani Profesa Kabudi anaweza kufanya. Hiyo haihitaji uprofesa wa Chuo Kikuu, labda Uprofesa wa aina ya Maji Marefu.

Katika kudhihirisha hili, katika mjadala wa sasa kuhusu mchanga wa dhahabu, Lissu ameng'ara sana kwa sababu anaweza kueleza kwa uwazi na ufasaha, historia yake ya mapambano. ni mtu anaelewa vizuri tatizo liko wapi na hivyo kama kweli nchi inataka kushughulikia matatizo haya, ianzie wapi.

Ushauri: CCM iwe mpole, ichape kazi. Irejeshe nyumba za serikali, hapo angalau Rais Magufuli atakuwa na ile “moral high ground” ya kushughulika na mambo mengine. Washughulike na kurekebisha mikataba mibovu. Wasijali hata kujikata miguu na mikono, ali mradi mwili mzima upone kansa hii.

Waache kupambana na upinzani. Hata kama wapinzani wanawakumbusha wananchi mambo ambayo kwa CCM ni mwiko kuyakumbusha, wao wasijali. Waache Bunge live ili wananchi wasiwafikirie kwamba wana mambo ya kuficha. Hapo Mastratejisti wala hawatakuwa na kibarua cha kuwatafuta “magicians” wa kuiokoa Serikali ya CCM.
 
Labda sijakuelewa lakini kama umeweka hili bandika kumsifu Lissu kwa kile anachokisimamia naona umeji contradict, Lissu katika masuala mengi hapo juu yenye utata hakusita kuishauri serikali iwachukulie hatua watuy waliokosea hadi kumshinikiza waziri mkuu aachie ngazi japo hakuna mahakama yeyoote iliyothibitisha ufisadi wa Mheshimiwa Lowasa.
Lissu aliunga mkono kamati ya bunge iliyoleta uchunguzi wa EPA na ushauri wa Kamati kuhusu kuchukuliwa hatua kwa wahusika, Lissu aliunga mkono Escrow japo pia wawekezaji walikuwepo hapo pia, Na kubwa zaidi Lissu aliunga mkono kamati ya Richmond, sasa sijui kuna tofauti gani ya hizo kamati zilizopita na hii ya rais. Kama aliunga mkono kamati iliyomtuhumu mtu bila kumuuliza ama kufanya mahojiano naye iweje leo aionee huruma Tanzania sababu tu kamati imeundwa na rais ati tutafika pabaya?

Wewe huoni hapo anacheza na siasa zaidi kuliko utaalamu wake kama mwanasheria mwanasiasa? Ndiyo maana kugeuka geuka huko kunawafanya watanzania wasiwaamini wanasisasa wa sampuli ya Lissu japo wanachokiongea kina maana lakini wanaongea wakati ambao si muafaka ama wanachokisema hakitoka mioyoni mwao.

Nilishasema huko nyuma Taifa hili lingeweza kukombelewa na watu kama kina Zitto, Lema, Lissu, Bashe, Nassari na wengine wengi sana vijana ambao wapo hata CCM lakini tatizo kubwa ni kwamba hawaaminikia. Ukimtoa Bashe hakuna hata mbunge mmoja kati ya hao niliowataja hapo juu mwenye uthubutu wa kuwahoji wakubwa wao kama kina Mbowe ama Magufuli kwa CCM. Bashe pekee ndiye kijana anayejiamini kukikosoa hata chama chake. Lissu umemsikia lini anakisema chama chake kwa kupotoka kutuletea mtu ambaye alituhumiwa na bunge kwa kulipotezea taifa pesa nyingi????

Jaribu kuwa mkweli na kumwambia Lissu pamoja na ujasiri wake wa kumchamba mpaka Nyerere lakini anafyata mkia wake ulio katikati ya mapaja yake likija jambo kuhusu viongozi wake wa CDM. Na mimi ninayesema hivi ni critical wa Magufuli lakini sipendi kila mara kusikia watu wakimlaum Magufuli kwa masuala ya nyumba wakati kuna wenzake tunataka mpaka kuwaweka Ikulu alishirikiana nao. Kama tunawasamehe kina Mtei, Lowasa, Sumaye walioshika nyadhifa kubwa zaidi ya magufuli sioni sababu kwanini tuendelee kumsulubisha Magufuli kwa kosa kutimiza kazi yake kama waziri.
 
Hayo maneno ni mazito ambayo kibiblia tunaambiwa mwenye masikio na asikiye hekima hii ya mzee Sulemani. Lakini shida inakuja kwamba hawatakuwa tayari kiyakubali na kuyatenda. Na ninayo mashaka kwamba makirikiri na bash it tayari wananyoosha nguo zao kubrush mabiot yao na kuweka mafuta mbundijo zao kukusaka wewe. Kwa chonjo kwani umekuwa pale penyewe
 
Labda sijakuelewa lakini kama umeweka hili bandika kumsifu Lissu kwa kile anachokisimamia naona umeji contradict, Lissu katika masuala mengi hapo juu yenye utata hakusita kuishauri serikali iwachukulie hatua watuy waliokosea hadi kumshinikiza waziri mkuu aachie ngazi japo hakuna mahakama yeyoote iliyothibitisha ufisadi wa Mheshimiwa Lowasa.
Lissu aliunga mkono kamati ya bunge iliyoleta uchunguzi wa EPA na ushauri wa Kamati kuhusu kuchukuliwa hatua kwa wahusika, Lissu aliunga mkono Escrow japo pia wawekezaji walikuwepo hapo pia, Na kubwa zaidi Lissu aliunga mkono kamati ya Richmond, sasa sijui kuna tofauti gani ya hizo kamati zilizopita na hii ya rais. Kama aliunga mkono kamati iliyomtuhumu mtu bila kumuuliza ama kufanya mahojiano naye iweje leo aionee huruma Tanzania sababu tu kamati imeundwa na rais ati tutafika pabaya?

Wewe huoni hapo anacheza na siasa zaidi kuliko utaalamu wake kama mwanasheria mwanasiasa? Ndiyo maana kugeuka geuka huko kunawafanya watanzania wasiwaamini wanasisasa wa sampuli ya Lissu japo wanachokiongea kina maana lakini wanaongea wakati ambao si muafaka ama wanachokisema hakitoka mioyoni mwao.

Nilishasema huko nyuma Taifa hili lingeweza kukombelewa na watu kama kina Zitto, Lema, Lissu, Bashe, Nassari na wengine wengi sana vijana ambao wapo hata CCM lakini tatizo kubwa ni kwamba hawaaminikia. Ukimtoa Bashe hakuna hata mbunge mmoja kati ya hao niliowataja hapo juu mwenye uthubutu wa kuwahoji wakubwa wao kama kina Mbowe ama Magufuli kwa CCM. Bashe pekee ndiye kijana anayejiamini kukikosoa hata chama chake. Lissu umemsikia lini anakisema chama chake kwa kupotoka kutuletea mtu ambaye alituhumiwa na bunge kwa kulipotezea taifa pesa nyingi????

Jaribu kuwa mkweli na kumwambia Lissu pamoja na ujasiri wake wa kumchamba mpaka Nyerere lakini anafyata mkia wake ulio katikati ya mapaja yake likija jambo kuhusu viongozi wake wa CDM. Na mimi ninayesema hivi ni critical wa Magufuli lakini sipendi kila mara kusikia watu wakimlaum Magufuli kwa masuala ya nyumba wakati kuna wenzake tunataka mpaka kuwaweka Ikulu alishirikiana nao. Kama tunawasamehe kina Mtei, Lowasa, Sumaye walioshika nyadhifa kubwa zaidi ya magufuli sioni sababu kwanini tuendelee kumsulubisha Magufuli kwa kosa kutimiza kazi yake kama waziri.
Analysis nzuri japo imekosa tu mifano hai (references) but ni nzuri.
 
Analysis nzuri japo imekosa tu mifano hai (references) but ni nzuri.
Hakuna haja ya references maana kama ulikua mfuatiliaji wa habari hizo hapo juu utaelewa kabisa kuwa Lissu ni mmoja wa wabunge tuliowasifu sana kwa wakati ule wa hizo scandal na thread nyingi humu zilikua zinampamba siyo kama sasa.
 
Labda sijakuelewa lakini kama umeweka hili bandika kumsifu Lissu kwa kile anachokisimamia naona umeji contradict, Lissu katika masuala mengi hapo juu yenye utata hakusita kuishauri serikali iwachukulie hatua watuy waliokosea hadi kumshinikiza waziri mkuu aachie ngazi japo hakuna mahakama yeyoote iliyothibitisha ufisadi wa Mheshimiwa Lowasa.
Lissu aliunga mkono kamati ya bunge iliyoleta uchunguzi wa EPA na ushauri wa Kamati kuhusu kuchukuliwa hatua kwa wahusika, Lissu aliunga mkono Escrow japo pia wawekezaji walikuwepo hapo pia, Na kubwa zaidi Lissu aliunga mkono kamati ya Richmond, sasa sijui kuna tofauti gani ya hizo kamati zilizopita na hii ya rais. Kama aliunga mkono kamati iliyomtuhumu mtu bila kumuuliza ama kufanya mahojiano naye iweje leo aionee huruma Tanzania sababu tu kamati imeundwa na rais ati tutafika pabaya?

Wewe huoni hapo anacheza na siasa zaidi kuliko utaalamu wake kama mwanasheria mwanasiasa? Ndiyo maana kugeuka geuka huko kunawafanya watanzania wasiwaamini wanasisasa wa sampuli ya Lissu japo wanachokiongea kina maana lakini wanaongea wakati ambao si muafaka ama wanachokisema hakitoka mioyoni mwao.

Nilishasema huko nyuma Taifa hili lingeweza kukombelewa na watu kama kina Zitto, Lema, Lissu, Bashe, Nassari na wengine wengi sana vijana ambao wapo hata CCM lakini tatizo kubwa ni kwamba hawaaminikia. Ukimtoa Bashe hakuna hata mbunge mmoja kati ya hao niliowataja hapo juu mwenye uthubutu wa kuwahoji wakubwa wao kama kina Mbowe ama Magufuli kwa CCM. Bashe pekee ndiye kijana anayejiamini kukikosoa hata chama chake. Lissu umemsikia lini anakisema chama chake kwa kupotoka kutuletea mtu ambaye alituhumiwa na bunge kwa kulipotezea taifa pesa nyingi????

Jaribu kuwa mkweli na kumwambia Lissu pamoja na ujasiri wake wa kumchamba mpaka Nyerere lakini anafyata mkia wake ulio katikati ya mapaja yake likija jambo kuhusu viongozi wake wa CDM. Na mimi ninayesema hivi ni critical wa Magufuli lakini sipendi kila mara kusikia watu wakimlaum Magufuli kwa masuala ya nyumba wakati kuna wenzake tunataka mpaka kuwaweka Ikulu alishirikiana nao. Kama tunawasamehe kina Mtei, Lowasa, Sumaye walioshika nyadhifa kubwa zaidi ya magufuli sioni sababu kwanini tuendelee kumsulubisha Magufuli kwa kosa kutimiza kazi yake kama waziri.
Siku zote nawaambia pro CCM na serikali yake, ni vigumu sana Rais Magufuli kupambana na ufisadi na hata yeye mwenyewe alishasema hataki kufukua makaburi. Kama ubavu huo anao, aanzie kwenye mizizi, awashitaki marais wastaafu waliosimamia mikataba feki ya madini na viongozi wengine hata kama wamehamia Chadema.
 
Mastratejisti wa Serikali ya Magufuli watakuwa walifurahi sana na kujipongeza, baada ya hotuba ya kwanza bungeni ya Profesa Palamagamba Kabudi, waziri mpya wa Sheria na Katiba. Nderemo, vifijo, na makofi yaliyokuwa yanapigwa, pamoja na vibwagizo, na wabunge wa CCM siku hiyo, ni ushahidi tosha.

Katika hotuba hiyo, Profesa Kabudi alionekana hatimaye kuja kama mkombozi wa serikali ya CCM kule Bungeni, kutokana na kuwa chini ya utawala wa Tundu Antipas Mughwai Lissu, ambaye alikuwa anawapeleka puta maspika, wenyeviti na wabunge wa CCM kwa ujumla.

Licha ya lugha yake kali, iliwabidi wapokee hoja zake na kutumia ujuzi wake wa sheria. Kumleta naibu spika ambaye ni mahiri wa sheria, Dakta Tulia, inaweza pia kuwa kwa ajili ya kuwadhibiti wapinzani wakiongozwa na Tundu Lissu katika uwanja huu.

Mhariri Mkuu wa Gazeti la Raia Mwema, Godfrey Dilunga, alikuwa na haya ya kusema kuhusu mtanange huu:

Swali la kujiuliza, ataendelea kuachiwa mwanya huu? Katika kutafakari swali hili, kule bungeni sasa kuna Waziri mpya wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi, msomi wa kiwango cha juu, mwepesi katika kumbukumbu za matukio ya kisheria, kisiasa, kijamii na hata kiuchumi, unaweza kusema siri ya uimara wa Lissu katika zama hizi ndio maisha ya kawaida ya kisomi ya Profesa Kabudi (huu ni mjadala mwingine wa siku zijazo).” [ Gazeti Raia Mwema, Toleo la Mei 4, 2017.] Tujadili

1. Kwa maoni yangu, Tundu Lissu ana nafasi kubwa ya kujipambanua na kumwacha kwa mbali Profesa Kabudi, kwa sababu zifuatazo:

2. CV ya Lissu. Pamoja na kwamba kisomi, Profesa Kabudi yuko juu sana zaidi kuliko Lissu katika uwanja wa Sheria, lakini Lissu ana faida ya kuishi yale aliyosoma, kusoma zaidi katika yale anayolazimika kupambana nayo. Karibu maisha yake yote baada ya kuhitimu, ameyatumia katika kupambana na mifumo ya sheria kandamizi na nyonyaji.

Amepambana na makampuni ya madini yanayovuruga mazingira na kubambikiza kesi kwa wananchi “vidomodomo”. Kwa hiyo Lissu ana uzoefu mkubwa sana katika field na ana data nyingi sana kwenye “finger tips” kuliko Profesa Kabudi, ambaye pamoja na kuwa ameshiriki kwa namna moja ama nyingine katika kupambana na mifumo, kama alivyodokeza kwenye hotuba yake Bungeni, wakati anahitimisha mjadala wa wizara yake bungeni 25 April 2017, lakini sehemu kubwa hasa ni katika kushughulika na nadharia katika tafiti na kufundisha darasani.

3. Passion ya Lissu. Hiki ndicho huonekana wazi kila mara Lissu anapokamata maiki. Kwa jinsi anavyoongea, uchaguzi wake wa maneno, tone yake, lugha yake ya mwili, Lissu hurusha ngumi nzito sana kwa wale anaowasema, kiasi kwamba wanakuwa katika wakati mgumu sana wamsikilizapo.

Hurusha makombora mazito sana yenye nguvu. Hii ni kutokana na kwamba toka ameanza kupambana, hajabadilisha kambi wala kubadili msimamo. Anaishi anayoyasema. Hii binafsi huwa inanishangaza sana kwa sababu najua kwamba makampuni ya Madini yana uwezo mkubwa wa kifedha na yamewa “garagaza” wengi waliojaribu kuyapinga, kwa kuwavuta mashati.

Wakati Profesa Kabudi mwanzo alionekana kama mtetezi wa wanyonge na mpinga ukandamizaji, baadaye alionekana “kuvutwa shati”, hasa mwanzoni mwa mijadala ya “Katiba Mpya”. Hapo akawa mtu wa kuisemea serikali, na serikali ikawa inamtumia “kutoa semina kwa wabunge”, ambazo zilioneshwa moja kwa moja na TBC.

Lakini baadaye Tume ya Katiba ya Warioba ilipochezewa rafu na serikali, wakanyang’anywa magari njiani, ambapo akina Polepole walianza kuzunguka nchi nzima wakiiandama serikali na kutetea rasimu ya katiba, Kabudi akageuka na kuwa mwiba kwa serikali. Hivi karibuni amevutwa tena shati na sasa ni mtetezi wa serikali katika mambo ya kisheria.

Kwa maoni yangu, si rahisi Kabudi kuwa na Passion ya kiwango cha Lissu. Anaweza kweli ku-summon passion kwa kiwango fulani, kama ilivyoonekana kwenye hotuba yake Bungeni, kwa kukumbusha aliyofanya miaka ya nyuma sana, lakini si kwa muda mrefu, na si kwa kiwango cha Lissu.

4. Historia. Historia iko upande wa Lissu. Ni kweli kwamba serikali ya CCM imesimamia uundwaji na usainiwaji wa mikataba mibovu kuwahi kutokea katika Historia ya wizi wa madini duniani. Hata Chifu Mangungu katika ujinga wake wote, hafikii rekodi ya CCM. Katika awamu mbalimbali za marais chini ya CCM, uwekezaji katika madini uliasisiwa, baada ya kuwekwa pembeni na Baba wa Taifa, Rais Nyerere. Mkapa ndiye alifungulia mbwa, na kuanzia hapo Tanzania imepigika vibaya sana kwa mfululizo wa mikataba ya wizi wa mchana.

Kuanzia mikataba ya umeme (IPTL, Net Group Solutions, Richmond, Dowans, Aggreko, Songas), mikataba ya madini, mikataba ya Gesi na mafuta, ni nchi inaliwa kulia, kushoto, juu na chini. Achilia mbali Ufisadi kupita Kagoda, na dada yake Meremeta, Rada, Escrow, Loliondo, bila kusahau wizi mkubwa kupitia ukwapuaji wa nyumba za Serikali.

Kwa rekodi kali ya wizi na ufisadi mkubwa wa kiwango hicho, mtu anayesimama kuibeba serikali ya CCM, atahitajika kuwa na ubavu wa pekee kubeba tani zote hizo za kashfa, wizi na ufisadi. Kitu ambacho sidhani Profesa Kabudi anaweza kufanya. Hiyo haihitaji uprofesa wa Chuo Kikuu, labda Uprofesa wa aina ya Maji Marefu.

Katika kudhihirisha hili, katika mjadala wa sasa kuhusu mchanga wa dhahabu, Lissu ameng'ara sana kwa sababu anaweza kueleza kwa uwazi na ufasaha, historia yake ya mapambano. ni mtu anaelewa vizuri tatizo liko wapi na hivyo kama kweli nchi inataka kushughulikia matatizo haya, ianzie wapi.

Ushauri: CCM iwe mpole, ichape kazi. Irejeshe nyumba za serikali, hapo angalau Rais Magufuli atakuwa na ile “moral high ground” ya kushughulika na mambo mengine. Washughulike na kurekebisha mikataba mibovu. Wasijali hata kujikata miguu na mikono, ali mradi mwili mzima upone kansa hii.

Waache kupambana na upinzani. Hata kama wapinzani wanawakumbusha wananchi mambo ambayo kwa CCM ni mwiko kuyakumbusha, wao wasijali. Waache Bunge live ili wananchi wasiwafikirie kwamba wana mambo ya kuficha. Hapo Mastratejisti wala hawatakuwa na kibarua cha kuwatafuta “magicians” wa kuiokoa Serikali ya CCM.
Maneno ni mengi lakini ukweli ni vipaji hutoka kwa Mungu siyo darasani kwa wanadamu
 
Bavicha sijui wanavuta bange ya wapi.Yaa Tundu Lissu mnamlinganisha na Prof.Palamagamba Kabudi?
Tundu Lissu kiboko yake ni Tulia Acson,kabudi yupo juu sana.
Tulia alimtuliza Lissu ndani ya nusu saa tu.Tundu Lissu alikuja na mikoba mitano imejaa vitabu lakini alishindwa
 
Hivi Prof. Kabudi ameishas ema neno lolote juu ya sakata hili la makinikia?
Hawa madokta na maprofesa ndo hao wanaomdanganya Rais,kwa kifupi hawana jipya

Pitia huu uzi. Link Sheria yetu ya madini na wabunge wasioelewa dhima yao

Umeona lawama na mshangao wa mtoa mada hapo. Huyu Profesa "Kaputi" aka Kabudi ndio mtaalamu wa sheria, gwiji na mbobezi. Yeye ndiye kitovu cha "kutengeneza miswada ya siri-kali aka serikali na kuiwasilisha bungeni. Yeye na Magufuli wake wakiamua ndio wataacha kulalamika na kufanya maigizo ya "uzalendo" kwa kutengeneza miswaada ya sheria mpya za madini zitakazohakikisha "hatupigwi pia hatuibiwi".

Wasomi wa nchi hii ni tatizo kuu la Tanzania kuendelea kuwagawia umasikini wananchi wake. Wao ni 10% na nguvu mdomo aka kupayuka na kulalamika wakati wamekwapua au wamejitishwa mamlaka na madaraka ya kuwaongoza wadanganyika.

Mpaka hapa tulipofikia katika suala la "magangwala au makanikia" ni sinema tu, maigizo ya kuwafanya wadanganyika wasahau machungu ya kutumbuliwa kwa uchumi na machungu ya kugawiwa umasikini ambao unafanywa na siri-kali za CCM kwa miongo 4 plus sasa.

Wadanganyika wanatakiwa wavae "uzalendo" bila kutambua kuwa wanaowaomba kufanya hivyo ndio chanzo cha sheria zilizopitishwa kwa hati za dharura za kuridhia "tuibiwe" na ndio hao hao waliosaini "mikataba mibovu" inayotoa ruhusa kwa "wawekezaji aka wezi wateuliwa" watuibie na watuachie mashimo na umasikini.

Baya zaidi litakalofuata ni Tanzania kulipa fidia kwa kuwachelewesha wawekezaji kuendelea kutuibia. Hapa namaanisha "samaki wa Magufuli" phase 2.

Link Makinikia: Je, Vyombo Vya Habari Vifukue Makaburi ya Chanzo, Au Kushangalia Tuu Matokeo?.Jicho Letu.
 
Back
Top Bottom