Lissu umeshindwa kupindua meza? Kuna hujuma? Wananchi hawajakuelewa? Timu yako ya kampeni ndio imepwaya? Tatizo ni ukosefu wa fedha?
Kuna tatizo kubwa sana la ajira katika nchi hii. Umeshindwa kutumia gap hilo kuwafanya wananchi wakuone kama mkombozi wao katika hili? Licha ya ajira za uchaguzi zilizotangazwa na Tamisemi nafasi 13,000 kwa nini wewe usije na sera ya kuajiri watumishi zaidi ya 50,000 huku ukilitangaza kwa nguvu zote?
Kuna watu wanateseka sana kupata mafao yao hususani waliomaliza mikataba yao au kuachishwa kazi. Nani awasemee kwa nguvu zote kama sio wewe? Kwanini hulipigii kelele sana swala hili? Naamini wananchi watakuelewa.
Suala la elimu hususani vyuoni hujalitangaza kwa nguvu zote. Sisemi kwamba hujalitangaza kabisa, hapana. Tatizo ni kwamba watu hawajakuelewa bado
Pamoja na uwepo wa hospitali na vituo vingi vya afya bado ni changamoto kubwa sana kupata Huduma bora. Njoo na mkakati mzito wa kuwaaminisha wapiga kura wakuamini na wakuchague wewe
Tunaweza kupambana na kutukanana huku mitandaoni. Lakini ukweli ni kwamba BADO MEZA HAIJAPINDULIWA. Tulioko huku mitandaoni tunaweza kuwa tunapimana kwa mipasho kutokana na mahaba ya dhati tuliyo nayo kwa wagombea wetu but uhalisia uko hivyo kwenye field yenyewe.Mikakati mizito ifanywe ili kuwaaminisha wapiga kura kuwa Lissu ndiye jawabu la changamoto nyingi zinazowakabili wananchi
Wewe inawezekana huwa husikilizi na kuelewa....
Meza iko upside down kitambo sana.....
Cha ajabu wewe unaiona imekaa kawaida tu...
Yote hayo uyasemayo yamefungwa kwenye kifungasho kimoja tu...
Ni "...tutafumua mfumo wa
KISHERIA, KIKATIBA na KIUTAWALA ili kurudisha uhuru a mamlaka kwa watu wa namna wanavyoweza kuendesha shughuli zao za kiuchumi na kijamii kwa Uhuru na haki bila bughudha..."
Hii ndiyo "general statement" inayojibu kila hoja yako hapo...
Unachoweza kushauri na mimi nakuunga mkono kabisa, ni hili;
Kwamba, aendelee kuielezea na kuifafanua hii kwa ufasaha na kwa lugha rahisi kueleweka kwa watu. Aseme ni kwanini kwa namna gani ukosefu wa UHURU na HAKI imekuwa ndiyo kikwazo cha watu kujiletea maendeleo yao ya kiuchumi na kijamii....
Na yeye na wagombea wake wote kuanzia udiwani na ubunge waeleze kwa ufasaha na lugha rahisi kueleweka ni kwa nini na vipi hii ndiyo itakuwa suluhisho la matatizo yao...
In my opinion, mpaka sasa amefanya na anafanya vizuri sana kulielezea hili. Recently ilikuwa ni Press Conference ya jana trh 9/9/2020 kwa zaidi ya masaa matatu alizungumzia hii kitu....
Kumtaka Tundu Lissu aanze kumwaga ahadi hewa tu, tutakuwa tunarudi kulekule kwenye siasa za kiCCM zilizoshindwa...
Kuna maahadi maelfu tangu Uhuru hayajawahi kutekelezwa na tumeishi ktk uongo huu mpaka leo na Magufuli anaundeleza vivyo hivyo....
Ni wakati wa kufikiri na kutenda tofauti na kwa njia tofauti....