Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 118,276
- 219,514
Taarifa iliyovuja inadokeza kwamba Mikutano ya Chadema ya Oparesheni 255 Kanda ya Serengeti , iliyopangwa kuzinduliwa kesho 25/08/2023 Shinyanga Mjini imepangiwa kuhujumiwa kwa kupiga Mabomu , na ikibidi kuua Watu ili kutisha Wananchi wasihudhurie Mikutano ya Chadema .
Hofu ya Wapanga njama hao inatokana na Ukweli kwamba , Mikutano ya Chadema kote inakopita inahudhuriwa na Maelfu ya Watu ambao wanaelewa mno kila kinachoelezwa na Chama hicho , ikiwemo Katiba Mpya na Ubovu wa Mkataba wa Bandari .
Hata hivyo tulishasema mara kadhaa humu kwamba , hakuna popote kwenye Dunia hii ambako Shetani aliwahi kumshinda Mungu .
---
Katika ukurasa wake rasmi wa Twitter (X) Tundu Lissu anaandika yafutayo:
Tuna taarifa za njama zinazopangwa & maadui wa Chama chetu kushambulia mikutano yetu ya hadhara inayoanza mkoani Shinyanga kesho kwa mabomu ya kurushwa kwa mkono. Lengo lao ni kuua au kujeruhi watakaohudhuria & kuwatisha wananchi wengine ili wasihudhurie mikutano itakayofuata.
Hatuwezi kupuuzia taarifa hizi. Matukio ya kigaidi ya aina hii yalikwishatokea miaka ya utawala wa Rais Jakaya Kikwete. Mikutano ya hadhara ya CHADEMA ilishambuliwa kwa mabomu Nyololo wilayani Mufindi, na Soweto mjini Arusha, na watu wasio na hatia waliuawa na wengine kujeruhiwa.
Jeshi la Polisi halikuwahi kuchunguza matukio haya ya kigaidi na kuwachukulia wahalifu husika hatua zozote za kisheria. Kama ilivyokuwa wakati wa utawala wa Kikwete, vitendo hivi vya kigaidi havitapunguza nguvu ya mapambano ya kidemokrasia nchini kwetu, & wala havitatunyamazisha.
Hofu ya Wapanga njama hao inatokana na Ukweli kwamba , Mikutano ya Chadema kote inakopita inahudhuriwa na Maelfu ya Watu ambao wanaelewa mno kila kinachoelezwa na Chama hicho , ikiwemo Katiba Mpya na Ubovu wa Mkataba wa Bandari .
Hata hivyo tulishasema mara kadhaa humu kwamba , hakuna popote kwenye Dunia hii ambako Shetani aliwahi kumshinda Mungu .
Katika ukurasa wake rasmi wa Twitter (X) Tundu Lissu anaandika yafutayo:
Tuna taarifa za njama zinazopangwa & maadui wa Chama chetu kushambulia mikutano yetu ya hadhara inayoanza mkoani Shinyanga kesho kwa mabomu ya kurushwa kwa mkono. Lengo lao ni kuua au kujeruhi watakaohudhuria & kuwatisha wananchi wengine ili wasihudhurie mikutano itakayofuata.
Hatuwezi kupuuzia taarifa hizi. Matukio ya kigaidi ya aina hii yalikwishatokea miaka ya utawala wa Rais Jakaya Kikwete. Mikutano ya hadhara ya CHADEMA ilishambuliwa kwa mabomu Nyololo wilayani Mufindi, na Soweto mjini Arusha, na watu wasio na hatia waliuawa na wengine kujeruhiwa.
Jeshi la Polisi halikuwahi kuchunguza matukio haya ya kigaidi na kuwachukulia wahalifu husika hatua zozote za kisheria. Kama ilivyokuwa wakati wa utawala wa Kikwete, vitendo hivi vya kigaidi havitapunguza nguvu ya mapambano ya kidemokrasia nchini kwetu, & wala havitatunyamazisha.