minyoo
JF-Expert Member
- May 25, 2013
- 21,640
- 20,366
Hivi Chadema waliwezaje kuondoa ulinzi maeneo yote Yale? Hivi Chadema si ndio walimsindikiza hadi Nairobi? Kwanini hawakuchomoa madrip kwenye ndege akajifia, ile si ilikuwa nafasi ya pekee kukamilisha Mission? Hivi Chadema wanaweza kumshawishi mkuu asitoe kibali cha pesa za matibabu? Hivi hasa Chadema wamepeleka wapi CAMERA ya Kalemani halafu Kalemani akawaacha tu utadhani ni CCM kachukua? Kwanini Tundu Lisu aparamie serikali wakati wasiojulikana ni CHADEMA, huu si ni upotoshaji wa hali ya kiwango cha flyover? Inawezekana mbunge Mollel amekimbia wauwaji kwenda kwa watetezi wa wanyonge eti? Ngoja niendelee kutafakari!
Kuwasangizia chadema kwenye shambulio la Tundu inabidi kwanza uwe na Akili ndogo sana finyu mno kama za Dr mollel, Le mutuz, cyprian Musiba, Katibu mkuu wa CCM ndipo utengeneze propaganda kama hiyo lakini kwa mtu mwenye Akili timamu hata huko CCM hawezi kukubali kuwa sehemu ya propaganda ya kishamba kama hiyo