Kwa akili ndogo sana tu, hivi kesi ya Lissu, dunia nzima inajua, iko live kwenye mitandao mbali mbali, narudia nani adhubutu kumpa sumu ili afe? Hivi issue kubwa kama hii, alafu apewe sumu? Huu ni uongo mkubwa na wa wazi kuichafua Serikali ya CCM, na hata wafuasi na wana chama wa Chadema wanajua hilo haliwezekani, sababu kuu Lissu yupo chini ya Magereza na Magereza ipo chini ya Serikali ya CCM, sasa kwa lipi hasa serikali ijichafue kwa kiwango kikubwa hivyo eti kumuwekea sumu Lissu?
Na uzuri, Serikali imekanusha hizo habari, na kukataa, kuwa hakuna kitu kama hicho, nachosema hapa, hii ni mbinu ya CHADEMA kuichafua Serikali kwa nia ovu tu, basi kutafuta attention tu ya public