kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 16,252
- 16,171
Tatizo kubwa la wapinzani nchini wanahangaika zaidi na yanayotokea ndani ya CCM badala ya kuhangaika na mambo ya wananchi na yale yaliyoko ndani ya vyama vyao vya upinzani. Wapinzani wanajadili waliotangaza nia CCM badala ya kuanza mapema kuongelea nani anafaa kuwa mgombea wao 2015 dhidi ya mgombea atakaeteuliwa na CCM (Lowassa? Sitta? Membe? Pinda? Mwigullu? Sumaye? Wassira? Makamba? Nyarandu? Kigwangala?, Migiro? Makinda? au.....?). Ni vema hata vyama vya upinzani kuanza kujitokeza kutangaza nia ili watu waanze kuwajadili kidogokidogo.
Upinzani ina Professor LImbumba hadi sasa ambaye ana haiba ya kugombea urais 2015. Lipumba hana kashifa yoyote mbaya kwenye jamii itakayoweza kutumiwa na wagombea wengine kumpinga. Lipumba hana tamaa, hana ukabila wala udini ni mwislamu wa kawaida tu anayemcha mungu, ni msomi na mchumi, na hajawahi kunyang'anya mke wa mtu.
Kama UKAWA ikimuandaa vizuri Lipumba, kumpamba na kumuunga mkono kwa hali na mali anaweza kushindana na mgombea yeyote kutoka CCM.
Upinzani ina Professor LImbumba hadi sasa ambaye ana haiba ya kugombea urais 2015. Lipumba hana kashifa yoyote mbaya kwenye jamii itakayoweza kutumiwa na wagombea wengine kumpinga. Lipumba hana tamaa, hana ukabila wala udini ni mwislamu wa kawaida tu anayemcha mungu, ni msomi na mchumi, na hajawahi kunyang'anya mke wa mtu.
Kama UKAWA ikimuandaa vizuri Lipumba, kumpamba na kumuunga mkono kwa hali na mali anaweza kushindana na mgombea yeyote kutoka CCM.