Lipumba: Mimi bado ni Mwenyekiti wa CUF, sitambui kikao cha Zanzibar

Ameandika barua ya kutengua kujiuzuru kwake uwenyekiti. Alijivua uwenyekiti akaenda fanya biashara zake binafsi sasa amerudi na kuutaka uwenyekiti kama vile aliuweka store.
Prof anajidhalilisha sana na kudhalilisha academic credentials zake
 
Mtatiro kijana amekubali kutumiwa na Seif......


Huyu Seif amelaaniwa maana ana uzoefu wa fitna...alimfitini Jumbe
 
Lipumba... kwishaaaaa kwishaaaaaaa kabisaaaaaaaa.... kifo cha mende, mlalo wa chaliii, kwishaaaaaaa kwishaaaaaaa kabisaaaaaaaaa....!!!!


Lipumbaaa.. kwishaaaaaaa...!! kifo cha nyani..!!
 
Jamani, ngoma sasa inogile. Prof. leo kakomaa hataki kabisa kuambiwa amesimamishwa uanachama.

Hii safi sana maana maalim anaendesha chama kama mali yake.
===========

Akihojiwa na mtangazaji Spencer Lamerk wa ITV usiku huu, Prof. Ibrahim Haruna Lipumba amesema kuwa yeye bado ni Mwenyekiti halali wa CUF.

Prof. Lipumba amesema kuwa kufuatia kutengua barua yake ya kujiuzulu Uenyekiti, aliandika barua kwa Katibu Mkuu wake kutaka kurejea kazini kama Mwenyekiti. Katibu Mkuu alimjibu kuwa anatafuta ushauri wa kisheria.

Kuhusu kikao cha Baraza Kuu la CUF kilichomsimamisha uanachama, Profesa Lipumba amesema kuwa kikao hicho hakikuwa halali kwakuwa hakukuwa na akidi ya Wajumbe wa kutoka Tanzania Bara. Amesema kuwa Katibu Mkuu hamshirikishi Naibu Katibu Mkuu Bara na kuonekana akiendesha chama kiimla.

Prof. Lipumba amesema kuwa Katibu Mkuu asipotaja tarehe ya yeye kurejea kazini kama Mwenyekiti, atasubiri barua ya Msajili wa Vyama ili aanze kazi tena kama Mwenyekiti wa taifa wa CUF.


ukiwa unafikiria vizur ndugu yangu utagundua something is behind this ni kukaa kimyaaa watamalizana wenyewe
 
Safi sana Lipumba ,viongozi wenye asili za kibaguzi lazima wawekwe wazi
 
Miaka zaidi ya 20 ktk chama umeahindqa kukijenga,leo unataka tena tena kimabavu. Umesahau nini? Ulijiudhuru kwa ridhaa yako kisa UKAWA kumpokea Lowasa na ukawaacha ktk ya vita. Wewe si mwanaume shupavu ni wa kukataliwa kabisa,hukuombwa kujiudhuru bali yalikuwa matakwa yako na Lowasa aliyekukimbiza km hufahamu bado yupo ndani ya Ukawa. km umetumwa utashindwa daima.
 
Ushauri wa bure kwa Lipumba,maisha yanaendelea bila cuf,usishushe zaidi hadhi yako ktk jamii kwa kulazimisha kuwa mwenyekiti wa Cuf,mtafanyaje kazi na watu mnaolumbana?rudi Ccm/Act /au anzisha chama kama alivyofanya Zitto,hii unayotaka kufanya ni kujidhalilisha mchana kweupe.
 
Professor, it is not too late. Bado unaweza kujiuzulu siasa na kubakia na heshima kiasi fulani.
 
Anatumiwa na MACCM ili kudhoofisha CUF na hatimaye kudhoofisha UKAWA. Kauli zake zinaweza kusababisha shari na hata watu kupigana kuumizana, kutiana vilema na hata kuuwana, lakini hili polisiccm haliwahusu maana kama kitengo cha MACCM wanakaa pembeni ili kuangalia mtafaruku wa ndani ya CUF na huku wakimsaidia Lipumba kwa kila namna ili aendelee kuivuruga CUF.

Majanga..... Huyu mzee Kama sio professor vile...
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Alimtaarifu maalim Seif kwani yeye ndio mwenye maamuzi ya kumrudisha? Alimtaarifu kwa barua rasmi ama kwa mdomo?
Lipumba kapatwa na nini?

Aliandika barua ya kuomba kujiuzuru mwaka jana. CUF hawakujibu hiyo barua. Wanadai ilipaswa kujadiliwa ktk mkutano wa (wanachama/sijui kamati?) kwa mujibu wa katiba yao. Kosa la CUF ni kuchelewa kuijibu hiyo barua - na ndo upenyo anaojaribu kutokea Lipumba. Kwamba aliandika barua ya kutengua barua yake ya awali ya kujiuzulu kabla ya huo mkutano wa kujadili barua yake ya awali kufanyika. Siungi mkono wazo la Lipumba kutaka kurudi tena CUF, ni kutapatapa - maana hawamtaki tena, ila inaonekana anaweza kuwa na hoja kisheria. Na serikali/mahakama wakisimama upande wake atawasumbua sana CUF. Kwa kifupi kaamua kufanya vurugu ndani ya chama chake.
 
Back
Top Bottom