Lipumba: JK atamaliza urais vibaya

Saint Ivuga

JF-Expert Member
Aug 21, 2008
54,363
58,386
Lipumba: JK atamaliza urais vibaya Send to a friend Sunday, 20 March 2011 21:04 0diggsdigg

Burhani Yakub,Tanga
CHAMA cha Wananchi (CUF) kimesema Rais Jakaya Kikwete atamaliza muda wake akiwa ameshindwa vibaya kusimamia shughuli za Taifa la Tanzania.

Alisema endapo Rais Kikwete anataka kukumbukwa katika historia, atumie muda uliobaki katika kuhakikisha katiba inafanyiwa marekebisho na tume ya uchaguzi inakuwa huru.

Ushauri huo ulitolewa jana na Mwenyekiti wa CUF,Profesa Ibrahimu Lipumba wakati akizindua kitaifa oparesheni Zinduka katika viwanja vya Tangamano jijini Tanga.

Alisema kati ya marais waliomtangulia kuongoza Tanzania kuanzia awamu ya Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere hakuna rais aliyeshindwa vibaya kusimamia masuala ya kitaifa kama Rais Jakaya Kikwete, tofauti na matarajio ya wananchi ambao walikuwa na imani kubwa wakati wakimchagua mwaka 2005.

“Kikwete ameshindwa kusimamia elimu ameweka rekodi ya kufelisha wanafunzi wa kidato cha nne ambayo haijawahi kutokea tangu tupate uhuru,kwenye afya mambo ni magumu katika uchumi, huko hakusemeki
ameshindwa kuzuia mfumuko wa bei, mpaka sasa umeme ni ngonjera tu miaka 50 ya uhuru Tanzania iko gizani,”alisema Lipumba.

Mwenyekiti huyo ambaye pia ni mchumi alisema chanzo cha kuanguka kwa uchumi wa Tanzania ni baada ya Rais Jakaya Kikwete kushindwa kuwadhibiti mapapa wa rushwa na ufisadi nchini akiwaogopa na kuwaacha wafanye wanachotaka jambo ambalo limewakatisha tama wananchi.

“Utawala wa Kikwete unakabiliwa na ombwe la uongozi, na hii inatokana na mfumo wa CCM ambao ameshindwa kila kitu,lakini kwa ushauri wangu ni kuwa kama anataka akumbukwe na historia basi ajikite zaidi katika kusimamia
marekebisho ya katiba na tume ya uchaguzi”alisema Lipumba.

Alisema jambo pekee ambalo Rais Kikwete ameanza kulisimamia ni kulivalia njuga suala la marekebisho ya katiba kwa kuhakikisha inabalishwa kulingana na matakwa ya Watanzania na si vinginevyo.

Lipumba alisema mchakato wa katiba unatakiwa uanze haraka ili kutoa fursa kwa Watanzania kuchangia maoni yao, lakini alisisitiza kuwa inatakiwa kwenda sambamba na kuunda tume ya uchaguzi ili huru na siyo kuwa na katiba ya sasa ambayo inafanya kazi ya kuchakachua kura na matokeo.

“Tume iliyopo haifai, hata kwenye tovuti yake haiandiki idadi halisi ya wapiga kura, imechakachua hadi daftari la wapiga kura, tunataka tume isiyowatumia watendaji wa Halmashauri wakiwamo wakurugenzi watendaji
na maofisa watendaji,”alisema Lipumba ambaye aaliambatana na Mbunge wa jimbo la Wawi Hamad Rashid Mohamed.

Aliwata wananchi kutumia fursa hiyo kwa kujitokeza kutoa maoni ya marekebisho ya katiba kwa kuwa ni haki yao na kwamba wahakikishe wanapendekeza masuala muhimu yenye kuligusa Taifa.

Kuhusu suala la kufanya maandamano na mikutano ya hadhara,Lipumba alisema ni haki ya vyama vya siasa na wananchi kuandamana kudai marekebisho ya katiba na kulalamikia mambo ambayo haendi sawa kutokana na uzembe wa viongozi wa Serikali ya CCM.

Aliwaasa wananchi kujihadhari na kauli zinazotolewa na baadhi ya viongozi wanaosema Tanzania haitatawalika na kwamba kinachotakiwa ni kufuata taratibu kwani Serikali iliyopo itang’olewa madarakani kwa kura na siyo vurugu.

“Msikubali kushabikia kauli zenye kuashiria vurugu,kama tusipoangalia tutasababisha CCM iendelee kushika dola,napenda kuwaeleza kuwa CCM imeshafikia mwisho tutaing’oa kwa kufuata taratibu”alisema Lipumba.
 
Wakati wa CCM umefika mwisho wakati ndo wanakula pamoja nchi huko Visiwani... Mbona Lipumba anatuchezea akili jamani...
 
lipumba *****,anatapatapa ka mwanamke mjamzto wa miezi 7! Haeleweki anamcmamo gani! Rabish lipumba
 
Sasa akimaliza vibaya inatusaidiaje sisi? Badala ya kutupa mwongozo wa kufanya unatabiri umekuwa shehe Yahya wewe? Tuambie kwa ugumu huu tufanye hivi au vile.
 
Wakati wa CCM umefika mwisho wakati ndo wanakula pamoja nchi huko Visiwani... Mbona Lipumba anatuchezea akili jamani...

Kwani huwezi kujadiri hoja?!‎؛‎, tazama key words from original post- huduma duni za afya, matokeo mabaya ya kidato cha nne kuliko yaliyo wahi kutokea toka tupate uhuru, mfumuko wa bei, ongezeko la mafisadi.............................. Bado tu hunacha kujadiri mpaka uanze kumjadiri mtoa hoja?!. Be a graet thinker and not sinker.
 
Uchochezi na uharibifu wa amani huo..... na yeye ajadiliwe na SISIEMU yao! Ikiwezekana akamatwe.
 
Kwani huwezi kujadiri hoja?!‎؛‎, tazama key words from original post- huduma duni za afya, matokeo mabaya ya kidato cha nne kuliko yaliyo wahi kutokea toka tupate uhuru, mfumuko wa bei, ongezeko la mafisadi.............................. Bado tu hunacha kujadiri mpaka uanze kumjadiri mtoa hoja?!. Be a graet thinker and not sinker.

Sijui kama unaijua siasa vizuri ndugu, siasa ni unafki. Ni lazma tujue kuhusanisha maneno na vitendo, huwezi kutamka vitu ambavyo hakuna mazingira ya kuvisimamia, halafu tuunge mkono. Back to CUF, hata watamke nini, hawana uwezo wa kuavocate wakati tayari kuna maridhiano kati yao na serikali ya CCM wanayoituhumu, na kama ni mfuatiliaji mzuri, matamko ya CUF yanakinzana, leo hili, kesho lile. Cant swallow that man...
 
Kwani huwezi kujadiri hoja?!‎؛‎, tazama key words from original post- huduma duni za afya, matokeo mabaya ya kidato cha nne kuliko yaliyo wahi kutokea toka tupate uhuru, mfumuko wa bei, ongezeko la mafisadi.............................. Bado tu hunacha kujadiri mpaka uanze kumjadiri mtoa hoja?!. Be a graet thinker and not sinker.

Gama una macho ila ukipofu ,unamasikio ila u kiziwi! Lipumba ukimfuatilia huoni mcmamo wake,cku chache alikua akiponda CDM na kumtukuza kikwete,kwenye hii thread yake anamwambia kikwete atamaliza vibaya! CDM Ilipita mikoani ikipinga ugumu wa maisha,kuilipa dowans na n.k,lipumba hakuliona hilo akadai wanataka kumpindua kikwete,leo hii anarudi kulekule kwa CDM,au yeye ndo anataka ampindue kikwete! gama acha uvivu wa kufikiria na acha ushabiki usio na maana! Ugumu wa maisha unazidi hvyo hatutaki kiongozi asie na msimamo kama lipumba!!
 
Ulimuona wapi huyo aiseeee!!!

Haa ha haaa, Yupo mitaa ya hapa kwetu alikua mpole alivyofika miezi 7 tu,mara nataka kuku,ukileta anazira na anakuambia amekinai hataki tena nlitee udongo! Ndo hali ya lipumba...CDM walipita mikoani kupinga mfumuko wa bei,kuilipa dowans,kufeli kwa 4m 4,kudai katiba mpya n.k,lipumba akadai wanataka kupindua nchi LEO hii anadai kikwete atamaliza vibaya na kupita mlemle mwa wanaCDM.Tumuelewe huyu ndie anaetaka kumpindua kikwete au anatuyeyusha!!
 
Back
Top Bottom