Lipumba 'ajirudisha CUF' kiaina

CUF hawana mtu wa kukiongoza Chama zaidi ya Lipumba, Uenyekiti ataupata.
Mi nimestuka kidogo pale aliposema kuwa viongozi wa Dini wamemuomba arudi madarakani, sasa sijui wa Dini gani!?
 
Mi nimestuka kidogo pale aliposema kuwa viongozi wa Dini wamemuomba arudi madarakani, sasa sijui wa Dini gani!?
Mkuu seriously hujui ni Dini gani?
MwanaCUF yoyote aje atuambie hapa ni nani ndani ya CUF atakuwa Mwenyekiti tofauti na Lipumba.
 
Mkuu seriously hujui ni Dini gani?
MwanaCUF yoyote aje atuambie hapa ni nani ndani ya CUF atakuwa Mwenyekiti tofauti na Lipumba.
Kweli mkuu, sijajua ni wa Dini gani viongozi hao wanaomtaka Lipumba arejee kwenye uenyekiti.
 
Chadema ndio wanaume..Tundu Lissu alimpa makavu rafiki yake Zitto ''tuambia kwanini tusikufuze uanachama kwa kosa la uhaini"...CUF haileweki ndo kina babu Duni anaesema chadema kila mtu anasharubu...hiyo ndo demokrasia lakini inapokuja suala la usaliti hakuna salia mtume
 
Aseme ukweli ni kipi kilichomfanya mpka akaondoka, na pia aseme pia ukweli kwanini anatamani kurudi, je zawadi aliyohaidiwa baada ya usaliti iliyeyuka au? Aweke mambo wazi , wengi tuliamini Prof aliondoka baada ya Lowasa kuingia katika UKAWA, lakin mpka sasa lowasa yupo Ukawa na sasa kwa nn anarudi , nafikiri kuna sababu kubwa , wanachama wa Cuf mwangalieni vizuri huyu mtu.
 
CUF hawana mtu wa kukiongoza Chama zaidi ya Lipumba, Uenyekiti ataupata.
Fikra za kijuha hizi,Lipumba ni mzigo CUF.Chini ya uenyekiti wake chama bara kilikuwa na wabunge wawili tu.Alipojiuzulu nafasi ya uenyekiti tena katikati ya uchaguzi mkuu CUF imeweza kuongeza idadi na kupata wabunge 9.Ninamshauri maalim asimrejeshe Lipumba kwa kupokea barua yake.Lipumba asubiri mpaka august 21 agombee tena nafasi ya uenyekiti wanachama waamue.

Maalim mwenyezimungu akuzidizie hekma.
 
Kweli mkuu, sijajua ni wa Dini gani viongozi hao wanaomtaka Lipumba arejee kwenye uenyekiti.
Kuna kikundi cha watu wachache ndani ya CUF kikiratibiwa na Abdul Kambaya ndio vinara wa kulazimisha kurejea kwa Lipumba CUF.
 
Wenyewe CUF wanamuita Profesa, wanamkubali sana. Akiongea kitu wanakichukulia kama point of reference. Hawezi kuachana na siasa.
 
Ujuha ni upi sasa? CUF walipata Wabunge 9 kwa mwavuli wa UKAWA siyo kwa sababu ya Mwenyekiti wa Chama.
 

Huyu ni sawa na Bwana Harusi kamkimbia Bibi Harusi siku ya Ndoa,baada ya miezi michache kusikia yule binti ameolewa anakimbia mbio ati turudiane.Huu mchezo kweli hauhitaji hasira,ni burdani mwanzo mwisho
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…