Lipumba 'ajirudisha CUF' kiaina

Lipumba 'ajirudisha CUF' kiaina

The Boss

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2009
Posts
49,320
Reaction score
117,611
Lipumba leo kazungumza na waandishi wa habari akiwa ofisi za CUF kasema mazungumzo yafanyike Zanzibar ili kupata suluhu na Magufuli kama yupo serious na rushwa aanze na walioiba pesa za Escrow kuwapeleka mahakamani...

..Wanachama wa CUF wamempokea vizuri Lipumba na wengi wamejitokeza.. Binafsi naona hata Lipumba 'hakutegemea' UKAWA wangefanya vizuri kiasi hiki na sasa anarudi 'kufaidika' na faida iliyopatikana<br>ya viti vya Ubunge na halmashauri tele

UKAWA walizoshinda.....Ukitazama uchaguzi ulivyotokea ni kama hata UKAWA hawakuwa ready kwa CCM kuondoka....sidhani kama

kuna hata mipango ya namna ya kuendesha manispaa zilizopatikana hasa za Dar...na hata walipoibiwa kura Mbagala na Kigamboni za ubunge sioni hata 'reaction' inayostahili.... watu wa Dar walipiga kura kuitoa CCM completely...

CCM ,UKAWA na kina Lipumba hawakuona this coming...

==================================

Dar es Salaam. Mwenyekiti wa zamani wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba amemwomba Rais Jakaya Kikwete kuiamuru Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC ) kumtangaza mshindi wa uchaguzi wa uliofanyika Zanzibar ili kuipusha nchi kuingia katika machafuko.

Jumatano iliyopita, Mwenyekiti wa ZEC, Jecha Salim Jecha alifuta matokeo ya uchaguzi uliofanyika Oktoba 25 mwaka huu akisema uchaguzi ulikuwa na kasoro nyingi.

Akizungumza leo kwa mara ya kwanza na waandishi wa habari tangu alipojiuzulu, Agosti 6, mwaka huu, Lipumba alisema amelazimika kutoa ushauri baada ya kuona hatari iliyo mbele kama wananchi wa Zanzibar watanyang'anywa haki yao.

"Ijumaa ijayo Dk John Magufuli ataapishwa kuwa Rais na Amiri Jeshi Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi na Usalama vya Tanzania, Kikwete usimwongezee Magufuli matatizo yaliyopo yanamtosha, " alisema.

Lipumba ambaye alipokelewa na wafuasi zaidi ya 100 kwenye ofisi za chama hicho zilizopo Buguruni, alisema Kikwete ahakikishe kabla hajamaliza muda wake wanaiamuru ZEC kuendelea kutangaza matokeo na kuwatangaza washindi wa uchaguzi huo.

Chanzo:
Mwananchi
 
hahahaaa,yani ametusaliti katkat ya safar sasa ndio anaona anarudi billion 3 alizopewa zimeisha binafsi napendekeza afutwe uanachama kabisa ameturidisha nyuma sana hakuna dhambi mbaya kama usaliti sitamsamehe lipumba na slaa hata siku moja.
 
Are you guys serious?Is he back?How did Cuf members react?Incredible!
 
Tatizo leprofeseri haaminiki inaonyesha ndo ilikua kazi yake kutumika na watawala. Kaona kukaa bila kuongea hawezi tena alikua na gundu huko cuf alipojiuzulu na wabunge wakaongezeka
 
Wamempokea kwa shangwe....
Hao waandishi wa habari (Mkapa aliwaita jina fulani hivi) hawakumtaka Prof. Lipumba afafanue "nafsi kumsuta " ni nini?

Au Je nafsi imemruhusu tena kushiriki kikamilifu kwenye siasa?

Je kwa kutangaza kuwa atabakia mwanachama wa CUF alitega kuvuna au kufaidika kupitia CUF baada ya uchaguzi (uchafuzi mkuu)?
 
Hii sasa shida kwa uhai wa UKAWA. Mbona anaongeza shida penye shida tayari
 
Aliyewaambi Lipu amejitoa CUF nani?yeye alipinga masuala kadhaa na kiungwana hatua alizochukua yeye ndizo hatua stahiki si kama walivyofanya akina mwafulani!aka mr hogo!
 
Wanachama wa cuf wanaokukubali uliwaacha njia panda..mh lipumba
 
Tatizo leprofeseri haaminiki inaonyesha ndo ilikua kazi yake kutumika na watawala. Kaona kukaa bila kuongea hawezi tena alikua na gundu huko cuf alipojiuzulu na wabunge wakaongezeka

gundu unalo wewe Lipumba alijiuzulu kwa sababu mawazo yake aliona hayasikilizwi .Subir sasa kuhusu viti maalumu na ruzuku ndio utajua Lipumba alimaanisha nini.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom