sammosses
JF-Expert Member
- Jan 24, 2011
- 1,682
- 1,110
Watanzania wanashindwa kuelewa ni lini bunge letu tukufu litakaa na kufanya kazi zake za kibunge!Ni mshangao ambao wananchi wana jiuliza kila siku kwa bunge letu kuacha kufanya kazi zake za kibunge na kuwa chombo cha utetezi dhidi ya tuhuma mbalimbali za kifisadi zinazo iandama serikali ya CCM.
Ina tia uchungu kuona kiti cha spika kina tumika vibaya kuhakikisha serikali haibanwi na bunge kwa hoja zenye kuleta tija na mapinduzi ya kiuongozi ndani ya serikali.Hali kama hii imekuwa ikipelekea kila anaye chaguliwa kupitia mfumo huu wa kulindana kuchafuka na kupoteza haiba yake kutokana tu na kulinda mfumo ambao ameukuta.
Kibaya zaidi wanao umia ni wananchi ambao wanatumika kama chombo cha kupitishia watu wasio na maslahi kwa jamii husika kwa kuwachagua na kushindwa kutekelza ahadi walizo ahidi.Tumeona bunge letu linaelekea kumaliza kikao chake cha kupitisha bajeti za mapato na matumizi ya serikali kwa mwaka 2012/13,swali hapa ni je bajeti hizo zimemnufaishaje mwananchi wa kawaida kiasi cha kuweza kuliamini bunge na kuona ndiyo kimbilio pekee na chombo cha kumtetea mwananchi huyu.
Wabunge wanaelekea kuhitimisha vikao vyao vya kuongeza maslahi katika mifuko yao kwa posho za sleeping and dogging allowance,sasa ni zamu yetu wananchi kuhoji mara watakapofika majimbo kutuletea mrejesho wa waliyoyajadili na kuleta tija kwa mustakabali wa maendeleo ya nchi na watu wake.
Kikubwa zaidi tunachotegemea kutoka kwao ni uhamasishaji wa sensa ya kitaifa inayokwenda kufanyika muda mfupi ujao.Si ajabu wengine wasionekane hata majimboni kwa kigezo cha kamati za bunge.Ifike wakati wanaporudi kutoka mjengoni tuwaulize wametuwakilisha vipi ilihali wakulima wanazidi kunyanyasika kwa kushindwa kupatiwa bei nzuri ya mazao yao.
Mrejesho huu wa bunge toka bungeni ni sawa kabisa na Riwaya katika vitabu vya secondary pale Obi Okonkwo alipotumwa na jamii yake kwenda kusoma ili alete ukombozi na fikra kwa kusoma sheria ambayo itatumika kuepuka unyanyasaji katika jamii yake lakini yeye alipofika kwenye mjengo wa huko abroad aliamua kuachana na kilichompeleka na kusomea mambo yasiyo na tija kwa jamii yake,tena mbaya zaidi kwa kupuuza hata mila za kwao na kutukuza mila za kigeni.
Mfano huu hauna tofauti na wabunge wetu,tunachowatuma wanakiweka pembeni na kuendeleza ya kwao na kusahau kazi kubwa inayo wasababisha kuwa ndani ya mjengo.Wananchi tusipobadilika tutaendelea kuchezewa na kupoteza haki zetu za kuchagua watu tuwatakao kwa maslahi ya taifa na watu wake.
Kuchezewa huku ni pamoja na dhihaka zinazofanywa na wabunge wetu kwa kudai waongezewe posho kwa kuwa tu posho hizo haziishi hapo mjengoni bali huwa zinawafikia wapiga kura wao.Tuamke tufikirishe akili zetu na kuacha habari ya kutumiwa kama chombo cha manufaa kwa wachache na tujue haki zetu za kuwachagua zinatumika vizuri?
Ina tia uchungu kuona kiti cha spika kina tumika vibaya kuhakikisha serikali haibanwi na bunge kwa hoja zenye kuleta tija na mapinduzi ya kiuongozi ndani ya serikali.Hali kama hii imekuwa ikipelekea kila anaye chaguliwa kupitia mfumo huu wa kulindana kuchafuka na kupoteza haiba yake kutokana tu na kulinda mfumo ambao ameukuta.
Kibaya zaidi wanao umia ni wananchi ambao wanatumika kama chombo cha kupitishia watu wasio na maslahi kwa jamii husika kwa kuwachagua na kushindwa kutekelza ahadi walizo ahidi.Tumeona bunge letu linaelekea kumaliza kikao chake cha kupitisha bajeti za mapato na matumizi ya serikali kwa mwaka 2012/13,swali hapa ni je bajeti hizo zimemnufaishaje mwananchi wa kawaida kiasi cha kuweza kuliamini bunge na kuona ndiyo kimbilio pekee na chombo cha kumtetea mwananchi huyu.
Wabunge wanaelekea kuhitimisha vikao vyao vya kuongeza maslahi katika mifuko yao kwa posho za sleeping and dogging allowance,sasa ni zamu yetu wananchi kuhoji mara watakapofika majimbo kutuletea mrejesho wa waliyoyajadili na kuleta tija kwa mustakabali wa maendeleo ya nchi na watu wake.
Kikubwa zaidi tunachotegemea kutoka kwao ni uhamasishaji wa sensa ya kitaifa inayokwenda kufanyika muda mfupi ujao.Si ajabu wengine wasionekane hata majimboni kwa kigezo cha kamati za bunge.Ifike wakati wanaporudi kutoka mjengoni tuwaulize wametuwakilisha vipi ilihali wakulima wanazidi kunyanyasika kwa kushindwa kupatiwa bei nzuri ya mazao yao.
Mrejesho huu wa bunge toka bungeni ni sawa kabisa na Riwaya katika vitabu vya secondary pale Obi Okonkwo alipotumwa na jamii yake kwenda kusoma ili alete ukombozi na fikra kwa kusoma sheria ambayo itatumika kuepuka unyanyasaji katika jamii yake lakini yeye alipofika kwenye mjengo wa huko abroad aliamua kuachana na kilichompeleka na kusomea mambo yasiyo na tija kwa jamii yake,tena mbaya zaidi kwa kupuuza hata mila za kwao na kutukuza mila za kigeni.
Mfano huu hauna tofauti na wabunge wetu,tunachowatuma wanakiweka pembeni na kuendeleza ya kwao na kusahau kazi kubwa inayo wasababisha kuwa ndani ya mjengo.Wananchi tusipobadilika tutaendelea kuchezewa na kupoteza haki zetu za kuchagua watu tuwatakao kwa maslahi ya taifa na watu wake.
Kuchezewa huku ni pamoja na dhihaka zinazofanywa na wabunge wetu kwa kudai waongezewe posho kwa kuwa tu posho hizo haziishi hapo mjengoni bali huwa zinawafikia wapiga kura wao.Tuamke tufikirishe akili zetu na kuacha habari ya kutumiwa kama chombo cha manufaa kwa wachache na tujue haki zetu za kuwachagua zinatumika vizuri?