Nikilewa mniache
JF-Expert Member
- Aug 8, 2015
- 19,276
- 51,858
Sajil-2: Kombora hatari la Iran linalofika Israel kwa 'dakika 7'
Chanzo cha picha: Getty Images
Maelezo ya picha: Jaribio la kwanza la mafanikio la kombora hili lilifanyika mwaka 2008
Mzozo wa hivi karibuni wa kijeshi kati ya Israel na Iran umekuwa jaribio la uwezo wa mapigano wa nchi zote mbili, pamoja na silaha zao.
Wakati Iran ilipoishambulia tena Israel wiki moja na nusu iliyopita, ilidai kwa mara ya kwanza kwamba kombora la Sajil-2 la Iran lilitumika katika shambulio hilo. Hata hivyo, Israel inadai kuwa jeshi lake lilizuia shambulio la kombora la Sajil na kulinasua kwa mafanikio kwa msaada wa mfumo wa ulinzi.
Ingawa mapigano yamesimama kwa muda, kombora hili linaonekana kuwa sehemu muhimu ya nguvu ya Iran.
Walinda Mapinduzi wa Iran wamesema kuwa mashambulizi ya Jumatano ya wiki iliypita yalifanywa kama sehemu ya "Operesheni Ahadi ya Kweli 3."
Taarifa iliyotolewa na Walinda Mapinduzi ilisema kwamba "operesheni ya 12 ya kulipiza kisasi ya Operesheni Ahadi ya Kweli 3 imezinduliwa kwa kombora zito sana la masafa marefu la Sajil la hatua mbili." Taarifa hiyo, ikielezea sifa za kombora hili, inadai kwamba Sajil ni mojawapo ya silaha zenye nguvu na sahihi zaidi za kimkakati za Iran, zenye uwezo wa kuharibu malengo muhimu ya adui.
Nguvu ya Kombora la Sajil
Chanzo cha picha: Getty Images
Maelezo ya picha,Kombora la Sajil lina urefu wa takriban mita 18 nalinalotumia mafuta, jambo linalolifanya kuwa hatari.
Sajil ni kombora la balistiki la masafa ya kati lenye uwezo wa kufikia maeneo lengwa hadi kilomita 2,000. Kwa masafa haya, kombora hili linaweza kulenga Mashariki yote ya Kati, ikiwemo Israel, kusini mashariki mwa Ulaya, na sehemu za Asia ya Kati, likirushwa kutoka Iran. Ikiwa litarushwa kutoka mji wa Natanz nchini Iran, linaweza kufika jiji la Tel Aviv nchini Israel kwa dakika saba tu.