Lift/elevator mbovu sasa basi

Nina maswali machache mkuu.....
1 - Hizi lift elevator, mnazi fabricate wenyewe na kuzi install kwenye jengo la mteja, ama ninyi mna import kutoka ng'ambo na kisha mnafanya kuzi install kwa wateja?
2 - Zipi safety precautions ikiwa itatokea lift elevator imekwama kati ya jengo na jengo (namaanisha kabla ama baada ya kufika kwenye exist & entry)?
3 - Ni aina ipi ya lifting mechanism mnayo tumia kwenye lift elevator zenu?

Ebu tuanzie haya kwanza, kisha ukisha jibu kwa faida ya wana jf wote, nitakupa some connections ya hizi mambo.
 
Mkuu hata sijajua ila naona hakuna ubaya hapo..
Mkuu be careful,trade slowly you might be trading in dangerous zone! If u are single sawa,if u r married please be careful! NOTE;am not jealousy!
 
Asante sana mkuu kwa maswali yako mazuri sana na nitayajibu ili iwe kwa faida yako member wangine wa hapa Jukwaani.
1. Lift/Elevator zetu ni Brand ya MERIH ASANSOR ni Kiwanda kikubwa kabisa nchini Uturuki, Hawa tunafanya nao kazi na sisi ndio wasambazaji wao wakuu kwa Afrika mashariki na kati, Baada ya kukubaliana na mteja na kununua Lift toka kwetu sisi tunawapa order wao fabricate kisha sisi tunafanya Installation pamoja na maintenance.
2. Lift zetu ni za kisasa kabisa na zina card maalumu inaitwa ARD SYSTEM (AUTOMATIC RESCUE DIVICE) pamoja na backup, ikitokea tatizo la umeme kukatika basi hii system inafanya kazi ya kuipeleka Lift kwenye floor inayofuata na ikifika Lift inafungua milango na inazima mpka umeme urudi. Kwahiyo swala la kukwama kwenye Lift zetu hicho kitu hakuna.
3. Lift zetu ni za kisasa kabisa na zote ambazo tumefunga ni latest 2016 zote ni ARKEL ARCODE na hizi zinatumia remote kugundua tatizo kwenye lift
 
Swali # 2 sijakuelewa kuhusu hiyo card unayosema inatoa back up ikwa lift imekwama. Hapa ungeniambia kwamba mnatumia battery kama back up kwaajili ya kusogeza lift ikiwa imekwama kabla ama baada ya entry/exit.

Swali # 3 haujanipa jibu na kwamba na sehem umdanganya.
Kimsingi sijauliza kama lift zenu ni zakisasa ama ni toleo la mwaka gani.
Nimtaka kujua aina drive kwenye mechanical. Hapa naamisha mnatumia Gear and Rail or Rope and Drum/Motor kwenye up and down ya elevator zenu?
Pia naomba nikusahihishe kwamba hakuna Remote inayo tumika badala ya Sensors.
Kazi ya Think mote ni kufanya uelekeo/ kuenfesha (control).
 

hapa ni pale unapokutana na mteja anejua bidhaa yako kuliko wewe muuzaji!
 
hapa ni pale unapokutana na mteja anejua bidhaa yako kuliko wewe muuzaji!
Huyu hajui ninachomwambia anakuja kubisha tu, sasa anakataa hakuna Lift inatumia remote??? bila hiyo remote huwezi fanya chochote ila yeye analeta ubishi tu.
 
Mkuu hatuko hapa kubishana wala wala kudanganyana na usome vizuri maelezo yangu vizuri, nimesema kuwa tunatumia ARD system hii nipamoja na backup yake amabyo ni betri zote zinafanya kazi sambamba inapotokea tatizo la umeme Lift itasogea kituo kinachofuata na kufungua milango na milango haitofunga mpka umeme urudi.
Sijadanganya sehemu yeyote, nimezungumzia remote na nikakuwekea na picha yake ya control panel na remote yake, ngoja nikupe elimu kidogo kwa lift za Kituruki hasa hizi ambazo ni latest ARKEL ARCODE zinatumia remote maalumu na bila hiyo remote huwezi kujua tatizo kwenye hiyo Lift.
 
hapa ni pale unapokutana na mteja anejua bidhaa yako kuliko wewe muuzaji!
Hapana mkuu....[emoji12] [emoji12]
Natamani kupata uelewa/ulimu kutoka kwa mleta uzi.
Hii ni kwa faida ya jf nzima.
 
Huyu hajui ninachomwambia anakuja kubisha tu, sasa anakataa hakuna Lift inatumia remote??? bila hiyo remote huwezi fanya chochote ila yeye analeta ubishi tu.
Punguza povu mkuu...[emoji23] [emoji23] [emoji23]
Hapa tupingane kwa hoja tu...[emoji135]
Kwanza matumizi ya remote kwenye lift hii unayo izungumzia wewe ni unsafe kwa mtu anaekua ndani ya lift hiyo.
Lakini ninacho kijua kuhusu lift hii unayo isemea wewe ni inaongozwa na Sensors ili iweze kuhisi ama ku maintain mawasiliano kutoka ama kwenda kwenye kila kituo.
Na ninaanza kuamini kwamba yawezekana unauza kitu ambacho haukijui kwa kushindwa kutofautisha SENSOR na REMOTE
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…