Let's share: Uliwahi kusaidiwa na mtu usiyemfahamu kabla (msamaria mwema)? Kipi kilitokea?

Kuna mtu huku Jf alishawahi kunisaidia hata sura wala Nina sijui nafahamu I'd yake tuu
 
Miaka mingi imepita kama 25 hivi, nikiwa nmetokea arusha na uporipori wangu nikaingia jijini. Safari ilikuwa ya kuelekea mtwara shule kwa masomo ya A level, dar sikuwa na ndugu nnayemfahamu na isitishe mawasiliano wakati ule ilikuwa mbinde. Nikashuka zangu na basi la fresh ya shamba nikatua ubungo terminal. Kwa sababu sikuwa na mwenyeji dar nilala pale stand. Kwa Bahati mbaya nilipotoka arusha nilikuwa nmepewa taarifa zisizo sahihi hasa nauli ya nnakokwenda kutokea dar. Niliambiwa nauli in tsh 5000 ilhali ukweli nauli ilikuwa mara 3 yake. Nikaanza kuzungukia mabasi kutafuta nauli nafuu kuanzia akida hadi WiFi naye. Kumbe katika zunguka yangu wajanja wa Ubungo wakawa waneninasa na shida yangu, waninyemelea wakanipa tuketi kwa bei niliyokuwa nayo. Asubuhi naenda kituo walichoniambia wanapaki gari zao kumbe holaaaa...hakuna kitu. Niliangaika sana kituoni. Baadaye akatikea jamaa mmoja akaniuliza na mie nikamueleza yaliyonipata. Alinipa msaada mkubwa sana, akanikimbiza hadi Sudan ya temeke, akawaeleza makonda kilichonipata, hatimaye nikapewa tiketi yenye herufi 'KK' maanake kusimama! Gari ilikuwa inaitwa misungwi, nilifika masasi baada ya siku tatu nikiwa nmesimama tokea dar. Yule jamaa sikumuona tena, huwa natamani kukutana naye siku moja nimpe asante na nimuambie mm ndo niliyekuwa nalia na kuburuza begi miaka hiyo 29+ akanisaidia hadi nauli ya dalaldala kufika Sudan.
 
Dah!! Kipindi niko o level shule moja iko upareni milimani huko nilipewaga suspension af pale ukipew suspension ni unaondoka hapo hapo,mfukon nlikuwa na ten tuu af inabid nifike daslam af ni saa 7 mchana

Kuna mdada mmoja alinisaidia siwez kuja msahau asee,km yupo Mungu amzidishie maradufu mana kila nilipojaribug kumtafuta sikuweza kumpata
 
Miaka mingi imepita kama 25 hivi, nikiwa nmetokea arusha na uporipori wangu nikaingia jijini. Safari ilikuwa ya kuelekea mtwara shule kwa masomo ya A level, dar sikuwa na ndugu nnayemfahamu na isitishe mawasiliano wakati ule ilikuwa mbinde. Nikashuka zangu na basi la fresh ya shamba nikatua ubungo terminal. Kwa sababu sikuwa na mwenyeji dar nilala pale stand. Kwa Bahati mbaya nilipotoka arusha nilikuwa nmepewa taarifa zisizo sahihi hasa nauli ya nnakokwenda kutokea dar. Niliambiwa nauli in tsh 5000 ilhali ukweli nauli ilikuwa mara 3 yake. Nikaanza kuzungukia mabasi kutafuta nauli nafuu kuanzia akida hadi WiFi naye. Kumbe katika zunguka yangu wajanja wa Ubungo wakawa waneninasa na shida yangu, waninyemelea wakanipa tuketi kwa bei niliyokuwa nayo. Asubuhi naenda kituo walichoniambia wanapaki gari zao kumbe holaaaa...hakuna kitu. Niliangaika sana kituoni. Baadaye akatikea jamaa mmoja akaniuliza na mie nikamueleza yaliyonipata. Alinipa msaada mkubwa sana, akanikimbiza hadi Sudan ya temeke, akawaeleza makonda kilichonipata, hatimaye nikapewa tiketi yenye herufi 'KK' maanake kusimama! Gari ilikuwa inaitwa misungwi, nilifika masasi baada ya siku tatu nikiwa nmesimama tokea dar. Yule jamaa sikumuona tena, huwa natamani kukutana naye siku moja nimpe asante na nimuambie mm ndo niliyekuwa nalia na kuburuza begi miaka hiyo 29+ akanisaidia hadi nauli ya dalaldala kufika Sudan.
Ulisimama for 3 days duh pole sana mkuu
 
mm nilipewa ada shiling 250000 na mtu nisije mjua nilkuwa sina na inabd niende A level nilipomwambia baada ya siku 2 akanipa bahati mbaya sanaa huyo mama alifariki kwa cancer kipind mm bado niko chuo iliniuma sanaa
 
Daah! Kuna jamaa pale Tunduma ,alinirudishia pochi yangu baada ya kuidondosha , ndani yake mlikua na drivers licence yangu na pesa za nchi mbalimbali zote zikiwa na thamani ya kama 3 million kama ningezibalidilisha kwa shillings, sikuamini , yule jamaa nilitaka kumpa pesa kidogo kama shukrani lakini huwezi amini,' alikataa!
Abuu bin Umar ni vibaya Sana mtu kakosea kutuma hela au kitu chochote kikakufikia wewe ukachukua Hali ukijua kuwa amekosea.. Last week nilitumiwa hela ya kupeleka rambirambi msibani namba ikakosewa ikaenda kwa jamaa mwingine pamoja na kumweleza ni hela ya nini bado aliichukua. Sasa najiuliza huyu si kama anajeletea laana kwa kujua? Kwangu naona ni uungwana kurudisha na si kukimbilia kwa wakala kuitoa
Kumbe na wewe ulikuwepo kwenye uvamizi ule saa 11 alfajiri munaturushia mawe kama mvua .
pole sana mkuu .

Kuna methali inasema asiyekujua hakuthamini. Hii sikubaliani nayo sana. Kuna wakati asiyekujua anaweza kukuthamini kuliko anayekujua. Yamenikuta mimi. Nilienda nchi za watu, watanzania walinikwepa ila watu kama waethiopia na wanaijeria ndo waliokua tayari kunisaidia. Nilishangaa mno

very touching mkuu, nahisi hapo ni milambo bila shaka
 
Mwaka 2000 nilikua Los Angels Calfonia kuna kitongoji kinaitwa bensen nakumbuka sikua naelewa lolote nikiwa nimetokea north Carolina 17 by age.
Nikiwa kwenye viunga flani naelekea kwa wenyeji wangu kuna mdada (black American) alinifata na kuniambia "cuz or blood? Nikajibu blood why akaniambia not with that look,Run you're about to be maggod" kuangalia huku nakuta kundi la watoto watukutu nilikimbia kuelekea kwa police officer akanisaidia mpaka jamaa zangu waliponifata.
Nilipewa taadhari kua kama sio mwenyeji si vyema kujichanganya na vikundi bila kuelewa
 
Mi nilimuokota majeruhi wa ajali ya gari Mandela Rd enzi hizo ni barabara moja!

Ilikuwa usiku, watu wakawa wanamgwaya, nikajitolea kupigania uhai wa dada yule.

Nikiwa na masela wa Kijiweni, tuliweka mabench ya saloon ili kufunga barabara kwani gari iliomgonga ilikimbia na gari nyingi zikawa hazitaki kusimama kutoa msaada.

Baada ya kufunga barabara kwa mabench, ilikuja Toyota nadhani STH ama SU, nikiwa nimetoka tu A level, nikapata ujasiri wa kuongea na dereva yule mtu Mzima kwa kifupi na huruma, akanipa mashart kuwa tumpeleke mgonjwa hospital pasi na kupita Police na vile vile yatakayojiri hospital hayamuhusu! Nikakubali.

Tulifika MUHIMBILI na mgonjwa wangu akahudumiwa baada ya KUKUBALI KUKUNJUA MKONO, of course (nilikuwa Mwl wa tuition so nilikuwa na vijihela kidogo) nilijiongeza baada ya kuambiwa eti mtu wa X-Ray kalala!

Dada yule alikuwa amevunjika mguu, pia alikuwa na maumivu ya mbavu! Police wa pale Super star walikuja na wakanihoji, kisha tukapata PF3.

Ndugu wa dada yule walikuja usiku kama Saa 7, wakanikuta bado napigwa nenda rudi ktk vicorrido vya muhimbili.

Kufika kama Saa 8 police walinchukua niwapeleke eneo la tukio ili wapate vipimo vya ajali!

Asubuhi nilienda muhimbili kumjulia hali manusra wangu na kiukweli alifurahi sana, ndugu zake walinisifu na kunishukuru sana!
Walitaka kunirudishia gjarama za matibabu, nikakataa.

Alihudumu mgonjwa wangu pale wodini kama siku 10 kisha akaruhusiwa, nikawa naenda kumjulia hali kwake Ubungo!

Nashukuru dada yule alipona, mara ya mwisho alijoin UDSM na mawasiliano yalishakufaga!

Dunia Mapito tu, ubinadamu ndio kila kitu!
 
Mie nakumbuka ilikuwa Mwaka 2015 nlienda Morogoro kikazi na ndo ilikuwa mara ya kwanza kufika Morogoro wakati nahangaika kutafuta hoteli nikaibiwa pochi,nkabaki napiga makelele ovyo, bahati nzuri kuna mkaka alikuwa anapita na aliona hilo tukio akaja akanipa pole akanambia dada unaenda wapi kwani nkamwambia mm ni mgeni nilikuwa natafuta hoteli akanichukua akanilipia hotel akanipeleka kula akanipa na pesa kidogo, alinisaidia sana , kesho nikampigia boss wangu nmepata matatizo akanitumia pesa nyingine, ni tukio ambalo kamwe sitalisahau maishani mwangu,amekuwa kama kakaang wa damu kabisaaaaa watoto wake likizo zingine wanakujaga kuniona, Mungu wa ajabu sana jamani
He
 
Mi nilimuokota majeruhi wa ajali ya gari Mandela Rd enzi hizo ni barabara moja!

Ilikuwa usiku, watu wakawa wanamgwaya, nikajitolea kupigania uhai wa dada yule.

Nikiwa na masela wa Kijiweni, tuliweka mabench ya saloon ili kufunga barabara kwani gari iliomgonga ilikimbia na gari nyingi zikawa hazitaki kusimama kutoa msaada.

Baada ya kufunga barabara kwa mabench, ilikuja Toyota nadhani STH ama SU, nikiwa nimetoka tu A level, nikapata ujasiri wa kuongea na dereva yule mtu Mzima kwa kifupi na huruma, akanipa mashart kuwa tumpeleke mgonjwa hospital pasi na kupita Police na vile vile yatakayojiri hospital hayamuhusu! Nikakubali.

Tulifika MUHIMBILI na mgonjwa wangu akahudumiwa baada ya KUKUBALI KUKUNJUA MKONO, of course (nilikuwa Mwl wa tuition so nilikuwa na vijihela kidogo) nilijiongeza baada ya kuambiwa eti mtu wa X-Ray kalala!

Dada yule alikuwa amevunjika mguu, pia alikuwa na maumivu ya mbavu! Police wa pale Super star walikuja na wakanihoji, kisha tukapata PF3.

Ndugu wa dada yule walikuja usiku kama Saa 7, wakanikuta bado napigwa nenda rudi ktk vicorrido vya muhimbili.

Kufika kama Saa 8 police walinchukua niwapeleke eneo la tukio ili wapate vipimo vya ajali!

Asubuhi nilienda muhimbili kumjulia hali manusra wangu na kiukweli alifurahi sana, ndugu zake walinisifu na kunishukuru sana!
Walitaka kunirudishia gjarama za matibabu, nikakataa.

Alihudumu mgonjwa wangu pale wodini kama siku 10 kisha akaruhusiwa, nikawa naenda kumjulia hali kwake Ubungo!

Nashukuru dada yule alipona, mara ya mwisho alijoin UDSM na mawasiliano yalishakufaga!

Dunia Mapito tu, ubinadamu ndio kila kitu!
Amini kwa namna ya ajabu sana kuna siku utalipwa kwa mema uliyofanya
 
Mimi mwaka 2010 nikiwa dodoma pale stand ilikuwa usiku ninatafuta gari ta kuja dar kesho yake magari yote yamejaa maana UDOM walikuwa wamefunga na st.john.
Sasa wakati nimekata tamaa akanifuata jamaa flani akaniambia kuna Yutong mpya nilikuwa na rafiki yangu tukakata tiketi zetu.
Then tukasema tukatafute sehemu ya kulala.
Wakati ninaondoka **** binti mdogo pale alikuwa kati ya miaka 15-17 hivi sema ana mwili mwili flani akanifuata.
Akaniambia kaka mimi nina shida, nikamuuliza shida gani.
Akasema kuwa alikuwa anatoka dar kwenye kesi ya mirathi ana mjomba wake pale dodoma alikuahidi akifika dodoma atampokea alale kwake ampe nauli ya kuelekea tabora maana alikuwa anaenda Tabora. Sasa toka amefika anampigia simu hapokei na hana mtu mwingine wa kunsaidia alikuwa na dada yake flani amempigia anememjibu kuwa hana ela.
Mida hiyo ilikuwa saa tatu usiku nikaona anazingua tu atakuwa anataka kuntapeli nikamwambia sina ela nikaondoka na jamaa yangu.
Jamaa yangu akaniuliza huyo dada alikuwa anakwambia nini nikamwambia, akasema ungemchukua ukalale naye mimi nikamwambia haa siko katika mood hiyo kama anamtaka akamfuate.
Baada ya kutafuta sehemu ya kulala tulikos maana wanafunzi walikuwa wamejaza nyumba zote za wageni ilabidi turudi pale stand tukaensa bar flan tukaanza piga urabu mpaka bar ilipogungwa.
Tukaenda lala kwenye lile basi nikamkuta yule binti amekaa na watu wengine ambao walikuwa nao wasafiri wanaolala stendi.
Nikamwita nikamwambia asubuhi nitamkatia tiketi ya kwenda Tabora.
Then nikamwambia kama anataka anaweza kulala kwenye basi maana tumeambiwa na wenye basi kuwa tunaweza lala mle.
Basi kutokana na urabu nikasinzia sa sijui mwenzangu na yule binti nini kiliendelea.
Asubuhi jamaa yangu ananiambia amemtongoza wamekuwa wapenzi nikimcheki binti namuona innocent nikamuuliza uko kidato cha ngapi akaniambia cha tatu.
To cut the story short nilimkatia tiketi bus lao liliondoka kabla yetu na nilimpa ela ya kula njianu hata namba yake sikuomba.
Baada ya week kama mbili nikapokea simu toka namba mpya mkumbe yule binti akaniambia kampigia yule rafiki yangu akamuomba namba yangu.
Toka siku hiyo akawa ananipgia mimi badala ya jamaa sema sikuwa namtafta na namba nikabadirisha.
 
Mimi mwaka 2010 nikiwa dodoma pale stand ilikuwa usiku ninatafuta gari ta kuja dar kesho yake magari yote yamejaa maana UDOM walikuwa wamefunga na st.john.
Sasa wakati nimekata tamaa akanifuata jamaa flani akaniambia kuna Yutong mpya nilikuwa na rafiki yangu tukakata tiketi zetu.
Then tukasema tukatafute sehemu ya kulala.
Wakati ninaondoka **** binti mdogo pale alikuwa kati ya miaka 15-17 hivi sema ana mwili mwili flani akanifuata.
Akaniambia kaka mimi nina shida, nikamuuliza shida gani.
Akasema kuwa alikuwa anatoka dar kwenye kesi ya mirathi ana mjomba wake pale dodoma alikuahidi akifika dodoma atampokea alale kwake ampe nauli ya kuelekea tabora maana alikuwa anaenda Tabora. Sasa toka amefika anampigia simu hapokei na hana mtu mwingine wa kunsaidia alikuwa na dada yake flani amempigia anememjibu kuwa hana ela.
Mida hiyo ilikuwa saa tatu usiku nikaona anazingua tu atakuwa anataka kuntapeli nikamwambia sina ela nikaondoka na jamaa yangu.
Jamaa yangu akaniuliza huyo dada alikuwa anakwambia nini nikamwambia, akasema ungemchukua ukalale naye mimi nikamwambia haa siko katika mood hiyo kama anamtaka akamfuate.
Baada ya kutafuta sehemu ya kulala tulikos maana wanafunzi walikuwa wamejaza nyumba zote za wageni ilabidi turudi pale stand tukaensa bar flan tukaanza piga urabu mpaka bar ilipogungwa.
Tukaenda lala kwenye lile basi nikamkuta yule binti amekaa na watu wengine ambao walikuwa nao wasafiri wanaolala stendi.
Nikamwita nikamwambia asubuhi nitamkatia tiketi ya kwenda Tabora.
Then nikamwambia kama anataka anaweza kulala kwenye basi maana tumeambiwa na wenye basi kuwa tunaweza lala mle.
Basi kutokana na urabu nikasinzia sa sijui mwenzangu na yule binti nini kiliendelea.
Asubuhi jamaa yangu ananiambia amemtongoza wamekuwa wapenzi nikimcheki binti namuona innocent nikamuuliza uko kidato cha ngapi akaniambia cha tatu.
To cut the story short nilimkatia tiketi bus lao liliondoka kabla yetu na nilimpa ela ya kula njianu hata namba yake sikuomba.
Baada ya week kama mbili nikapokea simu toka namba mpya mkumbe yule binti akaniambia kampigia yule rafiki yangu akamuomba namba yangu.
Toka siku hiyo akawa ananipgia mimi badala ya jamaa sema sikuwa namtafta na namba nikabadirisha.
mtafute huyo binti
 
mtafute huyo binti
Kitambo sana mkuu, mara ya mwisho kuwasiliana naye nadhan ni 2012 alikuwa kaja dar akanipigia kuwa yuko dar anaomba tuonane... mimi nilikuwa nimesafiri niko mkoabhuko kanda ya ziwa na nilibadiri namba...
Yani hata jina lake silikumbuki sikuwa na lengo lolote wala wazo lolote zaidi ya kumsaidia maana pale mikaa ilikuwa ashaanza kumlia timing.
 
Miaka kama 15 hivi iliyopita nililazwa Muhimbili. Nilikuwa nimetoka Koromije na sikuwa na ndugu wala jamaa Dar. Kila Jumatano kulikuwa na mzee hivi wa Kiislamu (kulingana na mavazi yake, midevu na Quran aliyokuwa akitembea nayo) alikuwa anakuja kuongea na wagonjwa. Basi nikamwona anakuja kitandani kwangu. Akaniambia kuwa nesi kamweleza kuwa nilikuwa sina ndugu waliokuwa wanakuja kuniona. Basi tuliongea sana na mwishoni akaniuliza kama nilihitaji blanketi (kulikuwa na baridi usiku) au cho chote kile. Pamoja na kumwambia kuwa nilikuwa sihitaji cho chote lakini aliondoka na aliporudi aliniletea blanketi jipya, shuka, matunda na hela kidogo. Aliendelea kuja kuniona kila Jumatano kwa wiki zote tatu nilizokuwa nimelazwa pale. Hata siku nilipofanyiwa operesheni kubwa ya masaa manne nilipofungua macho yeye ndiye alikuwa mtu wa kwanza kumwona. Niliporuhusiwa kuondoka ilikuwa Jumatano pia na nilimsubiri angalau nimuage lakini hakutokea. Wiki iliyofuata nilirudi pia na kujifanya kuwa naenda kusalimia wagonjwa ili nionane naye lakini hakuwepo. Niliulizia manesi wakasema alikuwa bado hajarudi tena. Na kuanzia siku hiyo sikuwahi kuonana naye tena. Sijui kama alikuwa malaika au nani ila kuanzia siku ile ndipo nikajifunza kuhusu wema wa binadamu nami huwa najitolea kusaidia wengine bila kinyongo wala kulalamika. Mzee yule aliyabadilisha kabisa maisha yangu na popote alipo basi Mungu Aendelee kumbariki na kama alishatangulia mbele ya haki basi Molla Ampe pumziko jema.
 
Mi nilimuokota majeruhi wa ajali ya gari Mandela Rd enzi hizo ni barabara moja!

Ilikuwa usiku, watu wakawa wanamgwaya, nikajitolea kupigania uhai wa dada yule.

Nikiwa na masela wa Kijiweni, tuliweka mabench ya saloon ili kufunga barabara kwani gari iliomgonga ilikimbia na gari nyingi zikawa hazitaki kusimama kutoa msaada.

Baada ya kufunga barabara kwa mabench, ilikuja Toyota nadhani STH ama SU, nikiwa nimetoka tu A level, nikapata ujasiri wa kuongea na dereva yule mtu Mzima kwa kifupi na huruma, akanipa mashart kuwa tumpeleke mgonjwa hospital pasi na kupita Police na vile vile yatakayojiri hospital hayamuhusu! Nikakubali.

Tulifika MUHIMBILI na mgonjwa wangu akahudumiwa baada ya KUKUBALI KUKUNJUA MKONO, of course (nilikuwa Mwl wa tuition so nilikuwa na vijihela kidogo) nilijiongeza baada ya kuambiwa eti mtu wa X-Ray kalala!

Dada yule alikuwa amevunjika mguu, pia alikuwa na maumivu ya mbavu! Police wa pale Super star walikuja na wakanihoji, kisha tukapata PF3.

Ndugu wa dada yule walikuja usiku kama Saa 7, wakanikuta bado napigwa nenda rudi ktk vicorrido vya muhimbili.

Kufika kama Saa 8 police walinchukua niwapeleke eneo la tukio ili wapate vipimo vya ajali!

Asubuhi nilienda muhimbili kumjulia hali manusra wangu na kiukweli alifurahi sana, ndugu zake walinisifu na kunishukuru sana!
Walitaka kunirudishia gjarama za matibabu, nikakataa.

Alihudumu mgonjwa wangu pale wodini kama siku 10 kisha akaruhusiwa, nikawa naenda kumjulia hali kwake Ubungo!

Nashukuru dada yule alipona, mara ya mwisho alijoin UDSM na mawasiliano yalishakufaga!

Dunia Mapito tu, ubinadamu ndio kila kitu!
Na ubarikiwe sana ndugu. Nadhani kwa msaada huo uliotoa ulizidi kubarikiwa zaidi na matunda yapo
 
Kuna tangazo la kazi lilitolewa katika moja ya taasisi kubwa nchini nami nikawa nimepeleka maombi yangu pale. Tulikuwa zaidi ya watu 600 na nafasi za kazi zilizotakiwa ni za watu 6 tu. Usaili ulikuwa ni wa nguvu na tulifanya takribani siku 3. Sikuwa na ndugu au mtu yeyote ninaemfahamu ktk taasisi hiyo ila alitokea kaka mmoja ambae nimfanyakazi hapo ambae mimi kwangu namuita Malaika maana alichonifanyia mpaka sasa siamini macho yangu. Nakumbuka siku moja nikiwa nina pesa ya nauli tu kuelekea kwenye usaili nilimuomba anisaidie japo pesa ya kula mchana maana ilikuwa balaa kama si aibu siku hiyo. Kaka wa watu hanijui wala mimi simjui ila alinipa elfu 50 na kuniambia neno moja tu "NITAKUSAIDIA". Niajabu na kweli ila ndo uhalisia wenyewe. Pamoja na kwamba ilinibidi niwe nasubira kutokana na mchakato wa kazi ulivyokuwa lakini kazi nilipata tena yenye mshahara mzuri ambao sikuwahi kuuota hata siku moja. Ni maombi yangu ya dhati kabisa toka moyoni mwangu kwamba Mungu amtunze na kumlinda huyu kaka pamoja na familia yake daima kwani ameondoa umasikini na aibu maishani kwangu.
 
Back
Top Bottom