Leo wivu umenicost

Leo wivu umenicost

Mwachie wa kusoma mavumba yake 50 kitu gani mkuu
 
Kama unachosema ni kweli basi ndugu ama una hela ya kuchezea au hauko makini kwenye maamuzi yako. Wewe namba hujui mwenyewe tena unahisi ni mchepuko wa wife halafu unatuma Tsh 50,000 eti kujaribisha???????

mi nawekaga milioni ishirini au au sh.tano
 
Story ya kweli au kutunga? Mpesa wanakuonyesha jina kabla ya kubonyeza 1 ili kuthibitisha
 
Hahaaaa! wivu bana, mwachie tu n shemeji yako ila uwe mwanhalifu ck nyingine
 
Hahahaa Ama kweli dunia n tambara bovu ukiliva mabo yt nje
Ilikuwa hivi,,kuna namba nilikuta kwenye simu ya wife . haina jina, jina alikuwa amesevu kwenye line nyingine. Hatuna mipaka kwenye simu,..sasa badala nimuulize, mi nikachukua hiyo namba, nikawa najaribu kuangalia jina kwa m-mpesa...yani unafanya kama unatuma hela halafu jina linatokea ili nimjue!

Nikajaribu kutuma 50,000. Mara jina likatokea, kumbe ni shemeji yangu wa kike mdogo wake na wife...,mbaya zaidi nilishasahau kumbe kwenye akaunt ya m-pesa kulikuwa na salio,, ile hela ikaenda kweli..sasa huyu binti badala hata anipigie kampigia dadaake, "shemej kantumia hela 50000"
nifanyeje manake naona aibu hata kumwambie arudishe istoshe ni mwanafunzi wa chuo..,

Halafu wife sijui ananielewaje, manake kuanzia jana namwambia sina hela!!

Ameshanuna sasa.
 
Jamani kujaribu jina ni nani ndo uweke kiwango chote hicho? Halafu jina huwa linakuja kabla hata ya kukubalikutuma! Walakini..ila pole haha
Elfu hamsini tu ndio kiwango chote hiko??? Kweli maisha yako tight
 
Ha ha ha ha mpigie cm shemeji yako mwambie nimekutumia hiyo pesa unichagulie nguo nzuri saiz ya dada yako nataka niimpe zawadi
 
Pole yk ndio ishakula kwako cku nyingne uwe makin, na kwann usahau kama cm inahela au la?huyo ni uzembe ww kakope kwa washikaji upate hata hela ya kula
 
mkuu si ungepiga huduma kwa wateja ukawaambia kuwa umetuma pesa kimakosa!!!au kashaitoa??
 
wakati mwingine inakuja namba tu. Jina linafuata baadae kwenye sms

Kuna wakati mwingine hata jina la uongo hutokea kabla hela haijatumwa, hivyo kigezo cha MPESA si sahihi kukitumia kumtambua mtu. Angalia utavunja ndoa kaka kwa wivu usio na maana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom