Aisee wivu hauna maana kabisa....! Sawa tu ukinicheka, lakini mi naamini kila mtu ana wivu.,..ila nilichojifunza wivu ni upuuzi mtupu, tuache!
Ilikuwa hivi,,kuna namba nilikuta kwenye simu ya wife . haina jina, jina alikuwa amesevu kwenye line nyingine. Hatuna mipaka kwenye simu,..sasa badala nimuulize, mi nikachukua hiyo namba, nikawa najaribu kuangalia jina kwa m-mpesa...yani unafanya kama unatuma hela halafu jina linatokea ili nimjue!
Nikajaribu kutuma 50,000. Mara jina likatokea, kumbe ni shemeji yangu wa kike mdogo wake na wife...,mbaya zaidi nilishasahau kumbe kwenye akaunt ya m-pesa kulikuwa na salio,, ile hela ikaenda kweli..sasa huyu binti badala hata anipigie kampigia dadaake, "shemej kantumia hela 50000"
nifanyeje manake naona aibu hata kumwambie arudishe istoshe ni mwanafunzi wa chuo..,
Halafu wife sijui ananielewaje, manake kuanzia jana namwambia sina hela!!
Ameshanuna sasa.