Setfree
JF-Expert Member
- Dec 25, 2024
- 5,601
- 7,218
Kwa zaidi ya wiki moja nimekuwa nikihisi kana kwamba kuna mdudu anatambaa tambaa kwenye bega langu la kushoto. Nikipapasa sehemu hiyo sioni kitu. Leo nikasema "enough is enough"(yatosha sasa). Nikaweka mkono sehemu hiyo na kuikemea hali hiyo kwa Jina la Yesu. Hivi sasa hali ya mdudu kutambaa tambaa imetoweka kabisa katika eneo hilo! Hakika Yesu hajabadilika. Miujiza aliyoitenda miaka 2000+ iliyopita bado anaitenda hata leo kwa kila aaminiye.
Kisayansi, wenye dalili kama hizo, huambiwa kwamba wana "paresthesia." Wanapoenda hospitali, madaktari huwauliza maswali mengi ili kujua chanzo cha hali hiyo na kupima nguvu za misuli (muscle strength), kupima hisia (sensation testing), au kufanya Nerve Conduction Study (NCS) kwa kutumia vifaa kama Electromyography (EMG), MRI (Magnetic Resonance Imaging), au CT Scan na Ultrasound (USG). Baada ya hapo, wagonjwa hufanyiwa fisiotherapi, au kupewa dawa za kupunguza mgandamizo wa mishipa, au wakati mwingine kufanyiwa upasuaji.
Namshukuru Mungu nimepona bure kwa Jina la Yesu, bila kuingia gharama ya kulipia vipimo hivyo na madawa!
Miujiza kama hii ni vigumu kuiona maishani mwako kama huamini kuwa Yesu ni Mungu, Mtenda miujiza.
Kisayansi, wenye dalili kama hizo, huambiwa kwamba wana "paresthesia." Wanapoenda hospitali, madaktari huwauliza maswali mengi ili kujua chanzo cha hali hiyo na kupima nguvu za misuli (muscle strength), kupima hisia (sensation testing), au kufanya Nerve Conduction Study (NCS) kwa kutumia vifaa kama Electromyography (EMG), MRI (Magnetic Resonance Imaging), au CT Scan na Ultrasound (USG). Baada ya hapo, wagonjwa hufanyiwa fisiotherapi, au kupewa dawa za kupunguza mgandamizo wa mishipa, au wakati mwingine kufanyiwa upasuaji.
Namshukuru Mungu nimepona bure kwa Jina la Yesu, bila kuingia gharama ya kulipia vipimo hivyo na madawa!
Miujiza kama hii ni vigumu kuiona maishani mwako kama huamini kuwa Yesu ni Mungu, Mtenda miujiza.