The Garang
JF-Expert Member
- Jan 16, 2018
- 2,890
- 4,865
Nawasalimu kwa jina la JamiiForum.
Miezi takribani mitatu kama sio miwili kuna dada nlitokea kumpenda, ni dada wa kichaga ambaye nilibahatika kukaa nyuma yake wakati tukifanya jaribio. Kufahamiana na huyu dada kulikuja wakati mie nikiwa nimeingia kwenye hall ya mtihani na kwakuwa niliingia late basi nikakaa nyuma na ndio nilikuwa mtu wa mwisho.
Nilifika moja kwa moja nikampa hi huyo dada kwa kumshika bega na kumuambia ntaangalizia kwako usifiche majibu kama unavojua kwenye chumba Cha paper lolote linaweza tokea mambo yakiwa magumu lazima ujue majirani mnasaidianaje, ilikuwa ni salamu tu na wala sio kama nilivomuambia.
Ikumbuke niliingia kwa mlango wa nyuma, kwahiyo sikuweza kumjuaa anasura gani, kupitiaa kumjulia hiyo hali akaweza geuka ndipo nlipoona uzuri wa yule binti.
Uzuri wa sura yake ni mithili ya kina Jokate Mwegelo, na alikuwa na bonge la tabasamu ,kichwani kaweka nywele za gharama na vidole vya mikono virefu na laini kwa kuvitazama
(vidole virefu ndo ugonjwa wangu kwa mdada).
Tuligawiwa paper, lilikuwa ni multiple choices, nikapiga chap ,karatasi la kusaini likaja nikaweza kuona na jina lake kwakuwa ye allikuwa mbele yangu na mie ndo full back Kama Yondani. Nikaenda kusanya paper langu huku nikiwa na shauku ya kutaka kujuana nae awe hata rafiki yangu tu kama Christian Bella alivoimba.
Nikaanza kuisaka namba yake kupitia majamaa zangu ambao niko nao programme tofauti, mwishowe nikaipata namba, nikaja kumtext na kujitambulisha , sikumbuki alijibu nini ila hakuwa na response nzuri kihivyo akidai kuwa hanikumbuki vizuri.
Nikamfungukia mtoto wa kichaga huku nikiamini, bora nitupie karata yangu mapema nione inakaaje. Mtoto akawa sio muelewa yani, sms anadelay kujibu, convo ya kawaida tu salamu mnaweza chati hata siku 3 haijaisha.
Basi nikamkumbuka Alikiba na song lake la kuforce mapenzi, nikaona isiwe mbaya dhahiri huyu binti hana interest na mie lakini pia nikakumbuka Bob Marley ashasema kama mwanamke ni wa thamani hutompata kirahici, ukimkatia tamaa inamaana hukuwa mtu sahihi kwake ..... .Nikajipa moyo ngoja nikomae nione inakuajee.
Katika pitapita zangu nikakutana na uzi unasema "Je ulishawahi kumlazimisha mtu abaki kwenye maisha yako, rafiki au mpenzi" nikachungulia humo nikakutana na nondo kinoma zikanijaza upepo , comments zilikuwa ziko kama hivi.
1.Mwanamme kukaa unambembeleza mwanamke huo ni unyonge.
2.Samaki baharini wako wengi kwann ukomaee na mmoja.
3.Ukiona hujibiwi sms kwa wakati ujue hupendwi hapooo nk
Hizo comments zikanijaza upepo lakini pia kulikuwa na comments kama hizi za kunifafiji.
1.Kuna mdada nimefukuzia ndani ya miaka miwili ndo amenikubalia majuzi.
2.Kabla ya kukata tamaa hakikisha umejarbu namna zote.
3.Mwanamke anaejiheshimu hawezi kukubali kiharaka asije onekana malaya.
Nilivopima kwenye mizani nikaona bora nimteme.
Inaendelea wakuu ndani ya dakika kadhaa.
Miezi takribani mitatu kama sio miwili kuna dada nlitokea kumpenda, ni dada wa kichaga ambaye nilibahatika kukaa nyuma yake wakati tukifanya jaribio. Kufahamiana na huyu dada kulikuja wakati mie nikiwa nimeingia kwenye hall ya mtihani na kwakuwa niliingia late basi nikakaa nyuma na ndio nilikuwa mtu wa mwisho.
Nilifika moja kwa moja nikampa hi huyo dada kwa kumshika bega na kumuambia ntaangalizia kwako usifiche majibu kama unavojua kwenye chumba Cha paper lolote linaweza tokea mambo yakiwa magumu lazima ujue majirani mnasaidianaje, ilikuwa ni salamu tu na wala sio kama nilivomuambia.
Ikumbuke niliingia kwa mlango wa nyuma, kwahiyo sikuweza kumjuaa anasura gani, kupitiaa kumjulia hiyo hali akaweza geuka ndipo nlipoona uzuri wa yule binti.
Uzuri wa sura yake ni mithili ya kina Jokate Mwegelo, na alikuwa na bonge la tabasamu ,kichwani kaweka nywele za gharama na vidole vya mikono virefu na laini kwa kuvitazama
(vidole virefu ndo ugonjwa wangu kwa mdada).Tuligawiwa paper, lilikuwa ni multiple choices, nikapiga chap ,karatasi la kusaini likaja nikaweza kuona na jina lake kwakuwa ye allikuwa mbele yangu na mie ndo full back Kama Yondani. Nikaenda kusanya paper langu huku nikiwa na shauku ya kutaka kujuana nae awe hata rafiki yangu tu kama Christian Bella alivoimba.
Nikaanza kuisaka namba yake kupitia majamaa zangu ambao niko nao programme tofauti, mwishowe nikaipata namba, nikaja kumtext na kujitambulisha , sikumbuki alijibu nini ila hakuwa na response nzuri kihivyo akidai kuwa hanikumbuki vizuri.
Nikamfungukia mtoto wa kichaga huku nikiamini, bora nitupie karata yangu mapema nione inakaaje. Mtoto akawa sio muelewa yani, sms anadelay kujibu, convo ya kawaida tu salamu mnaweza chati hata siku 3 haijaisha.
Basi nikamkumbuka Alikiba na song lake la kuforce mapenzi, nikaona isiwe mbaya dhahiri huyu binti hana interest na mie lakini pia nikakumbuka Bob Marley ashasema kama mwanamke ni wa thamani hutompata kirahici, ukimkatia tamaa inamaana hukuwa mtu sahihi kwake ..... .Nikajipa moyo ngoja nikomae nione inakuajee.
Katika pitapita zangu nikakutana na uzi unasema "Je ulishawahi kumlazimisha mtu abaki kwenye maisha yako, rafiki au mpenzi" nikachungulia humo nikakutana na nondo kinoma zikanijaza upepo , comments zilikuwa ziko kama hivi.
1.Mwanamme kukaa unambembeleza mwanamke huo ni unyonge.
2.Samaki baharini wako wengi kwann ukomaee na mmoja.
3.Ukiona hujibiwi sms kwa wakati ujue hupendwi hapooo nk
Hizo comments zikanijaza upepo lakini pia kulikuwa na comments kama hizi za kunifafiji.
1.Kuna mdada nimefukuzia ndani ya miaka miwili ndo amenikubalia majuzi.
2.Kabla ya kukata tamaa hakikisha umejarbu namna zote.
3.Mwanamke anaejiheshimu hawezi kukubali kiharaka asije onekana malaya.
Nilivopima kwenye mizani nikaona bora nimteme.
Inaendelea wakuu ndani ya dakika kadhaa.


