Hiyo ndoto yako ni matokeo ya kuamini na kutafakari sana porojo kama ambavyo zinaletwa na wana propaganda wA hawa boyz II men,hakuna kitu chochote kama bifu au kutokuelewana kati ya hawa jamaa wawili i.e JK na EL hilo nataka kukuhakikishia halipo.Kinachotengenezwa kionekane kama bifu ni mchezo wa kuigizwa ambalo lengo lake kuu ni kumbeaba Lowassa.Jk kafeli hakuna cha maisha bora kwa ari zaidi wala cha nini jamaa katota maisha ya watanzania yamekuwa from bad to worse.Na wao wanalijua hili.
Katika mazingira hayo sasa ni mbaya sana kwa Lowassa kuonekana yupo karibu sana na Kikwete kwa hiyo huo uadui wa kutengenezwa unampaisha EL ni janja ya nyani tu hiyo.
Ndo maana hawa kina Membe,Wassira,Pinda,Sitta na wengineo wote anaousaka urais kwa ticket ya ccm wanacheza makidamakida.Labda waanze kujipanga kwa mtindo mwingine lakini malengo ya hawa wajanja wawili ni kuachiana kiti,na kila kitu kinakwenda kama kilivyopangiliwa na ndiyo maana JK hawezi kufanya jambo lolote hata kama lipo ndani ya uwezo wake kufanya chochote ambacho kitamwekea usiku EL kwenye safari yake ya kwenda magogoni.
Mambo yote ya kampeni ambazo EL kimsingi keshazianza kitambo yana baraka zote za iku JK na msaada pia pale unapohitajika,na ndiyo maana utakuta viongozi wote wa chama Lumumba wanaongea hivi majukwaani lakini linapokuja suala kushughulikia masuala ya mipango ya EL katika kumsafishia njia wote wapo huko kwa EL.Kama miezi kadhaa imepita wabunge wastaafu toka maeneo mbalimbali nchini waliletwa Dar,kina Kirumbe Ng'enda ndo Hussein Bashe walikuwa mstari wa mbele kuwahudumia na kuwapeleka nyumbani kwa EL na kimsingi hicho tu ndo kilichokuwa kimewaleta,wazee wakaondoka na bahasha zao nene kurudi mkoa.
Sasa kumbuka wakati unaendelea kuota kumbuka kumchagua Lowassa wako ni kuirudisha nchi kwenye himaya ya akina Rostam Aziz,hivyo vi mia mbili miambili vyako vinavyokusukuma kupost huo upuuzi wako wa kijingajinga utakuja zitapika zote.Ustawi wa jamii nzima ya watanzania hautaletwa kamwe na mtu awaye yeyote kutoka ccm.JIPANGE.