Hamid Rubawa
Member
- May 23, 2018
- 72
- 202
Leo nilibahatika kukutana mjini London na Ahmed Rajab, Mohamed Abdullahi na Chama Omari Matata, waandishi maarufu barani Afrika na watangazaji wa zamani wa BBC. Kwa hakika ni nadhara kukutana na vigogo hao watatu mahali moja.
Nilivutiwa kwa mtangazaji na ndugu yangu mkubwa Mohamed Abdullahi na baadaye nikabatika kuanza kazi VOK ambapo alikuwa mwandishi muandamizi. Mohamed ndiye alinishauri na kunishawishi pakubwa nijitokeza na kupigania kitu cha ubunge cha Kamukunji.
Nilipokuja London kufanya kazi BBC nilimkuta ndugu Ahmed Rajab pamoja na Chama Omari Matatu huko Bush House. Rajab ambaye amenifundisha mengi juu ya uandishi wa habari na hata siasa za bara la Afrika ni rafiki mkubwa.
Pamoja na marehemu Mohamed Mlamali Adam tulibuni jarida la Africa Events, ambalo lilikuwa na umaarufu katika miaka ya themanini na tisaini kote barani Afrika.
Baadaye Mohamed Abdullahi alijiunga nasi katika BBC Bush House, na kupanda ngazi kwa haraka na kuwa mhariri mkubwa katika idhaa ya Kiswahili pamoja na ya Kisomali.
Nilivutiwa kwa mtangazaji na ndugu yangu mkubwa Mohamed Abdullahi na baadaye nikabatika kuanza kazi VOK ambapo alikuwa mwandishi muandamizi. Mohamed ndiye alinishauri na kunishawishi pakubwa nijitokeza na kupigania kitu cha ubunge cha Kamukunji.
Nilipokuja London kufanya kazi BBC nilimkuta ndugu Ahmed Rajab pamoja na Chama Omari Matatu huko Bush House. Rajab ambaye amenifundisha mengi juu ya uandishi wa habari na hata siasa za bara la Afrika ni rafiki mkubwa.
Pamoja na marehemu Mohamed Mlamali Adam tulibuni jarida la Africa Events, ambalo lilikuwa na umaarufu katika miaka ya themanini na tisaini kote barani Afrika.
Baadaye Mohamed Abdullahi alijiunga nasi katika BBC Bush House, na kupanda ngazi kwa haraka na kuwa mhariri mkubwa katika idhaa ya Kiswahili pamoja na ya Kisomali.