Leo ni kumbukumbu ya kifo cha Nyerere au Magufuli?

Tulimumu

JF-Expert Member
Mar 11, 2013
14,305
12,969
Wanasema leo ni kumbukumbu ya Kifo cha Nyerere lakini viongozi wote wakubwa wameenda kutembelea na kuweka mashada ya maua kwenye kaburi la Magufuli. Kwahiyo siku ya kumbulumbu ya kifo cha Magufuli watakwenda Butiama kuweka mashada ya maua kwenye kaburi la Nyerere? Au walitaka kutuonesha kuwa wamelijengea nyumba kaburi la Magufuli? Sijaelewa!
 
Binafsi nimeshangazwa pia
Umeshangazwa na Nini!?,mwal.anasheshma zake zote kwa kila mtz na tumekuwa tukimuenz kila kukicha Hadi leo,jpm alikuwa mbadala wa mwal. hivyo ni sawa pia katka kumbukiz za mwal.kumkumbuka pia jpm.hii ni meseji kwa mwal. ya kuwa baada ya wewe mwal. alitokea kijana wako ambae alitembea kwenye maono yako ya miaka mingi,bahati mbaya hatunae ,Ila ametufikisha mahali fulani pa kuanzia na kuendeleza.
 
Hii tafsiri yako


Sent from my SM-J730GM using JamiiForums mobile app
 
... Jpm aundiwe siku yake ya mapumziko; siku ya Mw. unamuenzi mwingine huku mwenye siku yake akiachwa tafsri yake nini? Mashada yalitakiwa yakawekwe Butiama kama yanavyowekwa Kisiwandui na sio Chato! Baba wa Taifa amekosewa heshima sana leo!
 
Hakika wakikujibu nistue , Hangaya badala ya kwenda kufagia kaburi la Nyerere anahangaika na mwendazake asiyehusika
 
Unashangazwaje kwa ufafanuzi ambao umekwisha kutolewa?!!!

Wameamua kuuzima mwenge Chato kwa ajili ya pia kumkumbuka hayati JPM....

HASTA LA VICTORIA EL COMANDANTE JKN🙏
 
Ni upumbavu wa Hali ya Juu, yaani leo hii Magufuli ndio achukue nafasi ya Mwalimu?

Hivi mama hawezi kufikiri kwamba timu ya Mwendazake inamuendesha inavyotaka?

Yaani kapigwa na kuaminishwa propaganda kwamba wasukuma ndio wanaamua Rais? Miaka yote kabla ya Uhuru walikuwa wanaamua Rais?

Magu alipata 58% za kubumba dhidi ya Lowassa kwa nini wasukuma hawakumpa aailimia zote? Huu ni upuuzi na dhihaka kwa Marehemu mwalimu Nyerere.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…