Freddie Matuja
JF-Expert Member
- Jul 21, 2018
- 1,484
- 2,890
Wanabodi,
Naomba ku-declare interest kuwa sina ugomvi binafsi na Naibu Waziri Hussein Bashe.
Nimekuwa namkubali kwa namna ambavyo alikuwa aki-analyse dhana ya mnyororo wa thamani hususan kwenye sekta ya KILIMO kwa michango yake "mjengoni"
Nadhani, sio sawa kutoa ruhusa kwa Wakenya kuingia kwenda kununua mahidi kwa wakulima. Pengine hatuja-set regulations za namna ya kufanya biashara ya mazao mchanganyiko. Jambo hili litutake tujenge mfumo rasmi wa manunuzi ya mazao mchanganyiko. Sio waje kwenda kununua mahindi moja kwa moja kwa wakulima.
Intermediaries wana sehemu yake kwenye biashara kama watasajiliwa. Kwenye bima kuna Brokers, na agents kama intermediaries. Hata bank ni intermediary ambae tukiweka mfumo bora wa mauzo banks zitakuwa na mifumo rasmi ya kugusa wakulima na TRA ana-access ya kodi kuoitia wigo utakaopanuka.
Huwezi kwenda Marekani ukanunua maziwa kwa wakulima then ukapaleka kiwandani wakufanyie packaging halafu usafirishe. Haiko hivyo.
Mhe. Naibu Waziri you can do the best kwa kushirikiana na Mhe. Hasunga na mtengeneza mifumo rasmi ili mahindi yaunuliwe, yakobolewe/kusagwa moja kwa moja na Kenya asubiri mahindi kule kwao. Ikiwa hivyo kwa haraka haraka itaongeza mzunguko wa fedha kwa Watanzania kwa mfumo wa mauzo, ulinzi kwenye maghala, bima za hifadhi kwenye maghala na vyanzo vya ajira kwa kujenga mfumo.
Kama ambavyokwenye madini (hatuuzi raw kwa wageni ili wakachakate makinikia kwenye refineries kwa wageni) na kwenye mahindi tuwe na mfumo wa soko maalum la finished products.
Tukisaga unga kwetu na ku-package sisi ni vema pia tuka-control logistics. Walau sio mbaya Kenya apokee mzigo mpakani kwake ili Magari ya Watanzania yahusike kusafirisha unga uliosindikwa. Hii ina akisi kutoa ajira na kuongeza wigo wa mzunguko nchini hali kadhalika kodi.
Kama ambavyo niliwahi kushauri hapa JF wakati wa zoezi la kupekeka mahindi Zimbabwe na Namibia; tunaposema tunajenga Tanzania ya viwanda kwa kuongeza thamani kwenye mazao ghafi na kupata tija kwa kuuza packaged final product, sasa tufanye kwa vitendo.
Mhe. Hasunga hakuona hiyo fursa, naomba pia mhe Bashe usianze vibaya.
Natoa ushauri mapema kabla mambo hayajaharibika. Kama mtasonga mbele na maamuzi hatuna namna ya kuwazuia ila tuna jukumu la kuwashauri namna gani mfanye vyema. Mnachokifanya kiwe na taswira ya kujenga uchumi na kukuza uchumi kupitia sekta ya viwanda.
Mungu Ibariki Tanzania
Naomba ku-declare interest kuwa sina ugomvi binafsi na Naibu Waziri Hussein Bashe.
Nimekuwa namkubali kwa namna ambavyo alikuwa aki-analyse dhana ya mnyororo wa thamani hususan kwenye sekta ya KILIMO kwa michango yake "mjengoni"
Nadhani, sio sawa kutoa ruhusa kwa Wakenya kuingia kwenda kununua mahidi kwa wakulima. Pengine hatuja-set regulations za namna ya kufanya biashara ya mazao mchanganyiko. Jambo hili litutake tujenge mfumo rasmi wa manunuzi ya mazao mchanganyiko. Sio waje kwenda kununua mahindi moja kwa moja kwa wakulima.
Intermediaries wana sehemu yake kwenye biashara kama watasajiliwa. Kwenye bima kuna Brokers, na agents kama intermediaries. Hata bank ni intermediary ambae tukiweka mfumo bora wa mauzo banks zitakuwa na mifumo rasmi ya kugusa wakulima na TRA ana-access ya kodi kuoitia wigo utakaopanuka.
Huwezi kwenda Marekani ukanunua maziwa kwa wakulima then ukapaleka kiwandani wakufanyie packaging halafu usafirishe. Haiko hivyo.
Mhe. Naibu Waziri you can do the best kwa kushirikiana na Mhe. Hasunga na mtengeneza mifumo rasmi ili mahindi yaunuliwe, yakobolewe/kusagwa moja kwa moja na Kenya asubiri mahindi kule kwao. Ikiwa hivyo kwa haraka haraka itaongeza mzunguko wa fedha kwa Watanzania kwa mfumo wa mauzo, ulinzi kwenye maghala, bima za hifadhi kwenye maghala na vyanzo vya ajira kwa kujenga mfumo.
Kama ambavyokwenye madini (hatuuzi raw kwa wageni ili wakachakate makinikia kwenye refineries kwa wageni) na kwenye mahindi tuwe na mfumo wa soko maalum la finished products.
Tukisaga unga kwetu na ku-package sisi ni vema pia tuka-control logistics. Walau sio mbaya Kenya apokee mzigo mpakani kwake ili Magari ya Watanzania yahusike kusafirisha unga uliosindikwa. Hii ina akisi kutoa ajira na kuongeza wigo wa mzunguko nchini hali kadhalika kodi.
Kama ambavyo niliwahi kushauri hapa JF wakati wa zoezi la kupekeka mahindi Zimbabwe na Namibia; tunaposema tunajenga Tanzania ya viwanda kwa kuongeza thamani kwenye mazao ghafi na kupata tija kwa kuuza packaged final product, sasa tufanye kwa vitendo.
Mhe. Hasunga hakuona hiyo fursa, naomba pia mhe Bashe usianze vibaya.
Natoa ushauri mapema kabla mambo hayajaharibika. Kama mtasonga mbele na maamuzi hatuna namna ya kuwazuia ila tuna jukumu la kuwashauri namna gani mfanye vyema. Mnachokifanya kiwe na taswira ya kujenga uchumi na kukuza uchumi kupitia sekta ya viwanda.
Mungu Ibariki Tanzania
