NI MTAZAMO TU
JF-Expert Member
- Feb 20, 2014
- 1,203
- 999
Vijana watatu kati ya kumi na mbili wauawa na wananchi wenye hasira kali baada ya kupita duka kwa duka wakiwa na silaha aina ya mapanga na visu kuvamia mtaa wa Kibo Rombo Ubungo.
Watu hawa walikuwa wanatoka mazishini kuzika mwenzao ambaye anasadikika aliuawa usiku wa juzi na wananchi kwa tulio la wizi maeneo ya Msewe Ubungo.
Wakiwa wanatokea kuzika wakatanda mtaa wa Rombo wakiwa na mapanga na visu ila baada ya kupora watu wengi simu na pesa,Wananchi waliwazingira na wakawamudu kwa kutumia mawe,baadhi yao wamefanikiwa kukimbia na watatu wakauawa papo hapo na kuchomwa moto.
Picha ya tukio haijapatikana kutokana na kukuta polisi wamefika na kuchukua miili ya marehemu.
Labda wenye picha na habari kamili watujuze...
Watu hawa walikuwa wanatoka mazishini kuzika mwenzao ambaye anasadikika aliuawa usiku wa juzi na wananchi kwa tulio la wizi maeneo ya Msewe Ubungo.
Wakiwa wanatokea kuzika wakatanda mtaa wa Rombo wakiwa na mapanga na visu ila baada ya kupora watu wengi simu na pesa,Wananchi waliwazingira na wakawamudu kwa kutumia mawe,baadhi yao wamefanikiwa kukimbia na watatu wakauawa papo hapo na kuchomwa moto.
Picha ya tukio haijapatikana kutokana na kukuta polisi wamefika na kuchukua miili ya marehemu.
Labda wenye picha na habari kamili watujuze...