Leo 03/06/17 Panya Road 12 waitingisha Rombo ya Ubungo, 3 wauawa

NI MTAZAMO TU

JF-Expert Member
Feb 20, 2014
1,203
999
Vijana watatu kati ya kumi na mbili wauawa na wananchi wenye hasira kali baada ya kupita duka kwa duka wakiwa na silaha aina ya mapanga na visu kuvamia mtaa wa Kibo Rombo Ubungo.

Watu hawa walikuwa wanatoka mazishini kuzika mwenzao ambaye anasadikika aliuawa usiku wa juzi na wananchi kwa tulio la wizi maeneo ya Msewe Ubungo.

Wakiwa wanatokea kuzika wakatanda mtaa wa Rombo wakiwa na mapanga na visu ila baada ya kupora watu wengi simu na pesa,Wananchi waliwazingira na wakawamudu kwa kutumia mawe,baadhi yao wamefanikiwa kukimbia na watatu wakauawa papo hapo na kuchomwa moto.

Picha ya tukio haijapatikana kutokana na kukuta polisi wamefika na kuchukua miili ya marehemu.

Labda wenye picha na habari kamili watujuze...
 
Vijana watatu kati ya kumi na mbili wauwawa na wananchi wenye hasira kali baada ya kupita duka Kwa duka wakiwa na silaha aina ya mapanga na visu kuvamia mtaa wa Kibo Rombo Ubungo.

Story kamili watu hawa walikuwa wanatokea mazishini kuzika mwenzao ambaye anasadikika aliuwawa usiku wa juzi na wanchi Kwa tulio la wizi maeneo ya msewe Ubungo.

Wakiwa wanatokea kuzika wakatanda mtaa wa Rombo wakiwa na mapanga na visu ila baada ya kuporwa watu wengi simu na pesa,Wananchi waliwazingila na wakawamudu Kwa kutumia mawe,baadhi yao wamefanikiwa kukimbia na watatu wakauwawa hapo hapo na kuchomwa moto.

Picha ya tukio haijapatina kutokana na kukuta police walisha fika na kuchukua miili ya marehemu.

Labda wenye picha na habari kamili watujuze.
safi
 
Matusi ya rejareja si mazuri

Unafikri hapa kuna panya road atae toka ?

wanaume wa dar.jpg
 
Wangewaua angalau nusu dazeni haki ingetamalaki
Hili tukia la saa hii mchana kulianza kama utani huku mtaani na mama wemepigwa na mabapa ya upanga. Na ilikuwa kama taharuki kwakuwa wanaingia dukani wanachukua zao na kila mpita njia unaacha simu la sivyo unakula panga
 
Back
Top Bottom